MAISHA YA MUKRISTO
Upendo Unatambulisha Wakristo wa Kweli—Tulinde Umoja Wetu
SABABU GANI NI LAZIMA: Usiku wenye ulitangulia kifo chake, Yesu alisali ili wanafunzi wake “waunganishwe kikamili” (Yoh 17:23, maelezo ya chini) Ili tuendelee kuwa katika umoja tunapaswa kuonyesha upendo wenye “Hauweke hesabu ya ubaya”—1Ko 13:5.
NAMNA YA KUFANYA:
Tumuige Yehova kwa kukazia uangalifu sifa za muzuri za wengine
Tukuwe tayari kusamehe
Kisha kumaliza matatizo, tusiizungumuzie tena.—Mez 17:9
MUANGALIE VIDEO “MUKUWE NA UPENDO KATI YENU”—USIHESABIE MAKOSA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Mu sehemu ya kwanza ya video, namna gani Hélène alionyesha kama ‘anasehabia makosa’?
Mu sehemu ya pili ya video, namna gani Hélène aliweza kuachana na mawazo yake ya mubaya juu ya wengine na kuwa tena na mawazo ya muzuri?
Mwishowe, namna gani Hélène alichangia ili kutaniko likuwe na umoja?
Ni nani tunakosea sana wakati tunaendelea kuhesabia makosa?