MAISHA YA MUKRISTO
Fuatia Elimu ya Yehova
SABABU GANI NI LAZIMA: Yehova, Mufundishaji Mukubwa, anatoa elimu yenye inapita yote. Anatufundisha namna ya kufanya maisha yetu ikuwe muzuri na anatutayarisha kwa ajili ya maisha ya muzuri ya wakati weye kuja—na anatupatia ile elimu yote kwa bure! (Isa 11:6-9; 30:20, 21; Ufu 22:17) Elimu yenye Yehova anatupatia inatusaidia tujue namna ya kuhubiria wengine ujumbe wenye unaweza kuokoa uzima wao.—2Ko 3:5.
NAMNA YA KUFANYA:
Komalisha sifa ya unyenyekevu na upole.—Zb 25:8, 9
Faidika na mazoezi yenye Yehova iko anakupatia tangu sasa, kwa mufano, kwa kukubali kufanya vipindi vyenye wanakupatia ku mukutano Utumishi na Maisha
Ujiwekee miradi ya kiroho.—Flp 3:13
Ujinyime mambo fulani kusudi ufikie kupata mazoezi zaidi.—Flp 3:8
MUANGALIE VIDEO TUMEKUWA MATAJIRI KIROHO KWA SABABU YA MAFUNDISHO YA YEHOVA, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ni vizuizi gani wahubiri fulani walishinda juu wahuzurie Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme?
Ni mazoezi gani yenye watu wanapewa ku Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme?
Wakati wanafunzi wenye walisoma Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme walifika mu migao yao ya mupya, namna gani ndugu na dada waliwasaidia?
Ni mambo gani mutu anapaswa kutimiza juu aalikwe ku Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme? (kr uku. 189)
Unaweza kujiwekea muradi wa kuhuzuria masomo gani ingine mu tengenezo la Yehova?
Ni baraka gani utapata kama unafuatia elimu ya Yehova?