MAISHA YA MUKRISTO
Yehova Anapenda Watu Wenye Kuwa Safi
“Unawe mikono. Usafishe chumba chako. Ufagie mu nyumba. Utupe uchafu.” Wazazi wengi wanawafundisha watoto wao namna ya kuwa safi kimwili. Lakini, ile maagizo ya usafi inatoka kwa Mungu wetu mutakatifu. (Kut 30:18-20; Kum 23:14; 2Ko 7:1) Tunamufurahisha Yehova wakati tunajikaza ili mwili wetu na vitu vyetu viendelee kuwa safi. (1Pe 1:14-16) Tuseme nini juu ya nyumba yetu na inje ya nyumba yetu? Tofauti na watu wenye kutupa uchafu katika barabara na katika mabustani, wakristo wanajikaza kufanya dunia iendelee kuwa safi. (Zb 115:16; Ufu 11:18) Hata namna tunatupa vitu vya kidogo-kidogo sawa vile karatasi ya bonbon, chupa, ao sachet, inaweza kuonyesha mawazo yetu juu ya usafi. Katika kila sehemu ya maisha yetu, tunapenda ‘kujipendekeza sisi wenyewe kuwa watumishi wa Mungu.’—2Ko 6:3, 4.
MUANGALIE VIDEO MUNGU ANAPENDA WATU WENYE KUWA SAFI, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ni visingizio gani vyenye watu fulani wanaweza kutoa vya kukosa kuhangaikia usafi wa vitu vyao?
Namna gani sheria ya Musa ilionyesha mawazo ya Yehova juu ya usafi?
Tunaweza kufanya nini ili kutoa ushahidi juu ya Yehova bila kusema jambo lolote?
Namna gani ninaweza kuonyesha kama niko na mawazo ya Yehova juu ya usafi mu maisha yangu?