MAISHA YA MUKRISTO
Umusifu Yehova kwa Kufanya Kazi ya Upainia
Kuko mambo ya mingi yenye ilipaswa kuwachochea Waisraeli wamusifu Yehova. Aliwatosha Misri na aliharibu jeshi la Farao ili kuwakomboa! (Kut 15:1, 2) Yehova anaendelea kufanyia watu wake mambo ya muzuri. Tunaweza kufanya nini ili kumushukuru?—Zb 116:12.
Njia moja ya kumushukuru ni kuwa painia musaidizi ao painia wa kawaida. Unaweza kumuomba Yehova akupatie hamu na nguvu ya kuwa painia. (Flp 2:13) Watu wengi wanaanza kwanza na upainia musaidizi. Unaweza kuwa painia musaidizi kwa kuhubiri saa 30 ao 50 mu Mwezi wa 3 na wa 4, na mwezi wenye mwangalizi anatembelea kutaniko lenu. Wakati unaona kama kazi ya upainia musaidizi inakuletea furaha, pengine utapenda kujikaza sana ili kuwa painia wa kawaida. Hata ndugu na dada fulani wenye wanatumika saa mingi na wenye kuwa na matatizo ya afya wameweza kuwa mapainia wa kawaida. (mwb16.07 uku. 8) Kwa kweli, Yehova anastahili mambo yote yenye tunafanya ili kumusifu!—1Ny 16:25.
MUANGALIE VIDEO DADA WATATU WA INCHI YA MONGOLIA, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Wale dada watatu walipambana na magumu gani juu wakuwe mapainia?
Walipata baraka gani?
Kwa sababu walikuwa mapainia wa kawaida walipata mapendeleo gani ingine?
Mufano wao ulisaidia wengine namna gani?