UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 23-24
Hapana Kufuatilia Watu Wengi
Yehova aliambia waamuzi na watu wa kushuhudia kosa ku tribinali kama, hawapaswe kusukumwa na watu wengine ili kushuhudia mambo ya uongo na kuhukumu mu njia yenye haiko ya haki. Ile angalisho inaweza pia kutumika mu mambo ingine. Watu wanaendelea kukaza Wakristo wakuwe na mawazo kama yao na wafanye mambo ya mubaya yenye haimuletee Yehova heshima.—Ro 12:2.
Juu ya nini ni kukosa hekima kufuatilia watu mingi wakati
unasikia habari zenye hazijulikane kama ni za kweli?
uko unachagua nguo, unatengeneza nywele ao wakati uko unachagua mambo ya kujifurahisha nayo?
uko na watu wenye walitoka fasi ingine, wa rangi ingine, maskini ao matajiri?