UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 4-5
Umutolee Yehova Kitu ya Muzuri Zaidi
Umaskini haukuzuia Waisraeli kufurahia pendeleo la kufanya amani pamoja na Yehova. Hata Waisraeli wenye walikuwa maskini sana, walimutolea Yehova toleo; na Yehova alikubali ile toleo kama tu ilikuwa njo kitu ya muzuri kwao. Walitoa unga, lakini Yehova aliwaomba unga “muzuri,” wenye ulitumiwa wakati wa kukaribisha wageni wenye kuheshimika. (Mwa 18:6) Leo, Yehova anakubali “zabihu ya sifa” ya muzuri zaidi, yenye tunamutoleaka hata kama tunaweza kujikuta mu hali zenye zitafanya tusitoe vile tulipenda kutoa.—Ebr 13:15.
Hii habari inaweza kukutia moyo namna gani, kama hauna tena uwezo wa kutumika sawa vile zamani mu kazi ya Yehova, pengine juu hii wakati afya yako haiko muzuri?