MAISHA YA MUKRISTO | UJIWEKEE MIRADI KWA AJILI YA MWAKA MUPYA WA UTUMISHI
Upainia
Tunatumikisha nguvu yetu kwa hekima wakati tunajiwekea miradi ya kiroho. (1Ko 9:26) Kujiwekea miradi kunatusaidia tutumikishe muzuri sana wakati wenye unabakia mbele mwisho ufike. (Efe 5:15, 16) Mu ibada yenu ya familia, munaweza kujiwekea miradi fulani kwa ajili ya mwaka wa utumishi wenye kuya. Juu muweze kufanya vile, mu hii buku ya mukutano muko habari mbalimbali kuhusu miradi yenye munaweza kufikiria katika sala.—Yak 1:5.
Kwa mufano, munaweza kupatana nyie wote mu familia yenu juu ya kusaidia hata mumoya wenu akuwe painia wa kawaida. Ikiwa unaona kama hauwezi kueneza saa zenye zinaombwa, unaweza kuongea na mapainia wenye kuwa mu hali sawa yako. (Mez 15:22) Pengine, unaweza kualika hata painia moya wakati wa ibada yenu ya familia na kumuuliza maulizo fulani. Kisha unaweza kuandika programu mbalimbali. Kama ulikuwaka painia zamani, unaweza kuona ikiwa hali zako zinaweza kukuruhusu ukuwe tena painia.
Inawezekana wamoya mu familia yenu wakuwe mapainia wasaidizi kwa mwezi moya ao zaidi? Kama hauna nguvu mingi, unaweza kuwa painia musaidizi kwa kuhubiri wakati kidogo tu kila siku. Kama uko na wakati kidogo ya kuhubiri katikati ya juma juu unatumikaka wakati wote ao unaendaka ku masomo, pengine unaweza kuchagua mwezi fulani wenye uko na siku yenye unapumuzikaka ao unaweza kuchagua mwezi wenye uko na Siku ya Posho tano na Siku ya Yenga tano. Uandike ku kalenda wakati wenye unapanga kuwa painia musaidizi, kisha uandike programu yako.—Mez 21:5.
MUANGALIE VIDEO UKUWE HODARI . . . PAINIA, NA KISHA MUJIBIE HII ULIZO:
Namna gani mufano wa Dada Aamand unaonyesha kama Yehova anapenda na kuhangaikia wale wenye wanajitolea ili kuwa mapainia?