Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w21 Mwezi wa 7 uku. 26-29
  • Maisha Yangu Yenye Furaha mu Utumishi wa Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maisha Yangu Yenye Furaha mu Utumishi wa Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAENDA AFRIKA YA KUSINI!
  • NDOA NA MUGAO MUPYA
  • TUNARUDIA KU BETELI
  • NARUDIA KU KAZI YA UCHAPISHAJI
  • MUGAO INGINE!
  • Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Je, Unaweza Kujitoa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
w21 Mwezi wa 7 uku. 26-29
John na Laura Kikot.

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Maisha Yangu Yenye Furaha mu Utumishi wa Yehova

JOHN KIKOT ANAELEZA MAISHA YAKE

KAZI yangu ya kwanza ku Beteli ya Kanada ilikuwa kusafisha fasi kwenye kazi ya kuchapisha ilikuwa inafanywa. Ilikuwa mu 1958, na nilikuwa na miaka 18. Mambo ilikuwa inaenda muzuri, na bila kukawia nilianza kutumia mashine yenye ilikuwa inakata sehemu za mwisho-mwisho za magazeti kisha kuchapwa. Nilifurahi sana kuwa ku Beteli!

Mwaka yenye ilifuata, walitangazia familia ya Beteli kama kulikuwa lazima ya wajitoleaji ili kutumikia ku tawi ya Afrika ya Kusini, juu ile tawi ilipata mashine ya mupya ya kuchapishia. Nilipeleka jina yangu, na nilifurahi sana wakati walinichagula. Wanabeteli wengine tatu wa Kanada walichaguliwa pia. Majina yao ni Dennis Leech, Bill McLellan, na Ken Nordin. Na walituambia kama tungekawia mu Afrika ya Kusini!

Nilimuita mama yangu na kumuambia hivi: “Mama, niko na habari ya muzuri. Niko naenda Afrika ya Kusini!” Mama alikuwa mwanamuke mutulivu, mwenye imani sana na mutu wa kiroho kabisa. Hakusemaka mambo mingi, lakini nilijua kama atanitegemeza. Baba na mama hawajapingaka hata siku moja uamuzi wangu, lakini walihuzunika juu ningekuwa sasa mbali nao.

NAENDA AFRIKA YA KUSINI!

Mu safari yetu kutoka Cape Town kuenda Johannesburg pamoja na Dennis Leech, Ken Nordin, na Bill McLellan mu 1959

Mu 2019, ku Beteli ya Afrika ya Kusini; miaka 60 kisha safari yenye tulifanyaka

Siye wote wa ine tulienda kwanza ku Beteli ya Brooklyn juu ya kupata mazoezi ya miezi tatu kuhusu namna ya kutumia aina fulani ya mashine ya kuchapishia. Kisha pale tukapanda mashua (bateau) ya kuenda Cape Town, Afrika ya Kusini. Njo nilikuwa tu nimeeneza miaka 20. Ilikuwa mangaribi wakati tulianza safari ya murefu sana kutoka Cape Town ili kuenda Johannesburg. Fasi ya kwanza kwenye tulisimama kidogo ilikuwa mu muji wa kidogo sana katika Karoo, eneo fulani yenye kuwa na jangwa kidogo. Tulifika pale asubui sana. Kulikuwa vumbi, moshi, na kifukutu. Siye wote wa ine tulichungulia ku madirisha na tulijiuliza kama njo fasi gani. Tulikuwa tunajiuliza kama mugao wetu ungekuwa wa namna gani. Mu miaka yenye ilifuata, wakati tulikuwa tunatembelea ile fasi tuliona kama vile vijiji vidogo-vidogo vilikuwa vyenye kupendeza na vyenye amani.

Kwa miaka kidogo, nilikuwa na mugao wa kutumia mashine fulani ya Linotype ya kushangaza na yenye kuwa nguvu kutumia, yenye ilisaidia kupanga muzuri mistari ya maandishi ili kuchapisha Munara wa Mulinzi na Amuka! Tawi ilikuwa inachapisha magazeti mu luga mingi za Afrika zenye zilizungumuziwa mu Afrika ya Kusini na mu inchi zingine za Afrika. Tulifurahi sana kuona kama mashine ya mupya ya kuchapishia yenye ilifanya tuende mu Afrika ya Kusini ilikuwa inatumiwa sana!

Kisha, nilitumika mu Biro ya Uchapishaji yenye ilisimamia mambo ya uchapishaji, kusafirisha vichapo, na kazi ya kutafsiri. Nilikuwa na kazi mingi ya kufanya na maisha yangu ilikuwa na furaha sana.

NDOA NA MUGAO MUPYA

Miye na Laura, tukiwa mapainia wa pekee mu 1968

Mu 1968, nilioa dada moja painia mwenye anaitwa Laura Bowen. Alikuwa anaishi karibu na Beteli. Tena, alikuwa anafanya kazi ya kuandika mu Idara ya Kutafsiri. Mu ile wakati, hakukuwa mupango wowote wa kubakia ku Beteli kwa wale wenye walioana. Kwa hiyo, Beteli ilitupa mugao wa kuwa mapainia wa pekee. Niliogopa kidogo. Kisha kupitisha miaka kumi ku Beteli, kwenye nilikuwa napata chakula na nyumba, sasa namna gani tungeweza kutumia makuta kidogo yenye walikuwa wanapatia mapainia wa pekee ili kuuza kila kitu yenye tulikuwa nayo lazima? Ile wakati kila mutu alikuwa anapata rand 25 (zamani ilikuwa dolare 35) kila mwezi kama tu angeeneza kiasi ya saa, marejeo, na kiasi ya magazeti yenye iliombwa. Kisha, tulipaswa kutumia ile makuta juu ya kulipia nyumba, kuuza chakula, transport, matunzo, na juu ya garama zingine za kipekee.

Tulitumwa mu kikundi kidogo karibu na muji wa Durban, kwenye Bahari ya India. Kule tulikuta Wahindi, wengi kati yao walikuwa watoto wa Wahindi wenye walikuyaka mu Afrika ya Kusini juu ya kutumika mu izine ya sukari, mu 1875 hivi. Sasa walikuwa wanafanya kazi zingine, na hawakubadilisha desturi yao, namna yao ya kupika chakula, bila kusahau chakula ya butamu sana yenye inaitwa curry. Tena, walikuwa wanasema Kiingereza, ile ilifanya mambo ikuwe mwepesi kwetu.

Zamani, mapainia wa pekee waliombwa kuhubiri saa 150 kila mwezi, kwa hiyo Laura na miye tulipanga kuhubiri saa sita siku ya kwanza. Kulikuwa kifukutu. Hatukukuwa na marejeo wala mafunzo ya Biblia, ni kusema tulipaswa kuhubiri saa sita nyumba kwa nyumba. Lakini, wakati kidogo tu kisha kuanza kuhubiri, niliangalia saa yangu na nikaona kama tulikuwa tulishafanya tu dakika 40! Nilijiuliza kama tungeweza kabisa kazi ya upainia wa pekee.

Bila kukawia, tulijipanga muzuri zaidi. Kila siku, tulitayarisha sandwiches na tulibeba supu ao café. Wakati tulikuwa na lazima ya kupumuzika, tulitia gari yetu fasi kwenye kulikuwa kivuli, karibu na muti na wakati fulani tulizungukwa na watoto fulani Wahindi wenye kutushangala! Kisha siku kidogo, tuliona kama kisha kuhubiri saa mbili ao tatu za kwanza, muchana ilipita mbio sana.

Tulifurahi sana kuletea watu wakarimu wa mu ile eneo kweli ya Biblia! Wahindi wanaheshimia wengine, wanatendea wengine kwa wema, na wanamuogopa Mungu. Watu wengi wa dini ya Wahindu walikubali ujumbe wenye tuliwaletea. Walipenda kujifunza juu ya Yehova, Yesu, Biblia, dunia mupya yenye amani yenye kuja, na juu ya tumaini ya wafu. Kisha mwaka moja, tukakuwa na mafunzo ya Biblia 20. Kila siku, tulikuwa tunakula chakula na moja kati ya familia zenye tulikuwa tunajifunza nao. Ile ilitufurahisha sana.

Bila kukawia, miye na bibi yangu tulipata mugao ingine: Kazi ya muzunguko katika sehemu za pembeni-pembeni za Bahari ya India. Kila juma, tulipangishwa na familia moja wakati tulikuwa mu ziara na tulitumika pamoja na wahubiri wa kutaniko ili kuwatia moyo. Tulizoeshana kabisa na familia zao, watoto wao, na hata wanyama wao. Tulipitisha miaka mbili ya muzuri sana mu ile kazi. Kisha kwa kushitukia, biro ya tawi ikatuita ku telefone. Walituambia hivi: “Tulikuwa tunawaza kuwarudisha ku Beteli.” Nikawaambia: “Tunafurahi sana kuwa hapa kwenye tuko.” Lakini kusema kweli, tulikuwa tayari kutumwa fasi yote kwenye wangetuomba kuenda.

TUNARUDIA KU BETELI

Ku Beteli, nilikuwa na mugao wa kutumika na Idara ya Utumishi, kwenye nilipata pendeleo ya kutumika na ndugu wengi wakomavu na wenye uzoefu. Ile wakati, kila kutaniko ilikuwa inapata barua kisha mwangalizi wa muzunguko kutuma ripoti wakati alimaliza kutembelea kutaniko fulani. Kusudi ya zile barua ilikuwa kutia moyo na kutoa muongozo fulani wenye ulihitajiwa. Ile ilikuwa kazi sana kwa waandishi wenye walitafsiri barua kutoka mu luga ya Xhosa, Zulu, na luga zingine ili kuzitia mu Kiingereza na kutoka mu Kiingereza ili kutafsiri mu luga za Afrika. Nilikuwa nasamini sana wale watafsiri wenye bidii, wenye pia walinisaidia kuelewa muzuri magumu yenye ndugu na dada zetu weusi walipata.

Ile wakati, Afrika ya Kusini ilikuwa chini ya utawala wa apartheid. Kila kikundi ya watu wa rangi fulani ya ngozi ilikuwa inaishi mu eneo yake, na ile ilifanya ikuwe nguvu sana kwa watu wa rangi tofauti kupitisha wakati pamoja. Ndugu zetu weusi walikuwa wanasema luga yao, kuhubiri mu luga yao, na kukusanyika mu makutaniko ya luga yao.

Sikujua sana ndugu wengi weusi, juu nilitumikia mu maeneo ya makutaniko ya Kiingereza. Lakini, nilipata sasa nafasi ya kujua ndugu weusi na desturi zao. Nilijua magumu yenye ndugu zetu walipata kwa sababu ya kukatala kufuata desturi na mafundisho ya dini ya mu eneo yao. Walikuwa na uhodari sana! Walikatala desturi zenye zilipingana na Maandiko, desturi zenye ziliunga mukono mambo ya kishetani, na walikuwa tayari kupambana na upinzani mukali kutoka kwa watu wa familia zao na wa vijiji vyao. Mu maeneo ya mashamba, kulikuwa umaskini sana. Hata kama watu wengi hawakusoma ao walisoma kidogo waliheshimia Biblia.

Nilipata pia pendeleo ya kuwa kati ya wale wenye walitetea uhuru wetu wa ibada na wa kuepuka kujiingiza mu mambo ya politike. Imani yetu ilitiwa nguvu sana wakati tuliona uaminifu na uhodari wa vijana Mashahidi wenye walifukuzwa ku masomo juu walikatala kufanya sala za dini na kuimba nyimbo za kidini.

Ndugu zetu walipata pia magumu ingine mu inchi moja ya kidogo ya Afrika, yenye ile wakati iliitwa Swaziland. Wakati Mufalme Sobhuza wa Pili alikufa, waliomba raia wote wafanye desturi fulani za kilio. Wanaume walipaswa kukata nywele zote, na wanamuke kuacha tu nywele za mufupi-mufupi. Ndugu na dada wengi waliteswa juu walikatala kuunga mukono ile desturi yenye ilihusiana na ibada ya wazazi wa zamani. Uaminifu wao kwa Yehova ulitugusa sana! Ndugu zetu weusi walitufundisha uaminifu, uvumilivu, na walijenga imani yetu.

NARUDIA KU KAZI YA UCHAPISHAJI

Mu 1981, waliniomba nisaidie mu kazi ya kutumia ordinatere ili kufanya uchapishaji. Basi, nikaitika. Ile ilikuwa wakati ya muzuri sana! Namna ya kuchapisha vichapo mu dunia ilikuwa ilishabadilika. Mwanaume moja alipatia tawi mashine moja hivi ya mupya juu tupime kuitumia, tena kwa bure. Ile ilifanya tubadilishe mashine kenda za Linotype zenye tulikuwaka nazo na kutia tano za mupya. Tuliweka pia mashine ya mupya ya kuchapishia. Ile ilifanya kazi ya kuchapisha iende mbio sana!

Ordinatere zilitusaidia kutokeza njia za mupya za kupanga maandishi ku ukurasa kwa kutumia MEPS (Système électronique d’édition multilingue). Zamani tulikuwa tunatumia Linotype zenye kula fasi bure tu, zenye kutumika polepole, na mashine zingine za zamani za kuchapisha. Njo mambo ilifanyaka siye Wanabeteli wa ine tutoke Kanada na kuya mu Afrika ya Kusini. (Isa. 60:17) Kisha wakati fulani, siye wote wa ine tulioa dada mapainia wazuri kabisa wenye walimupenda sana Yehova. Miye na Bill tulikuwa tungali ku Beteli. Ken na Dennis tayari walikuwa na familia, karibu tu na kwenye tulikuwa.

Ku tawi kazi ilikuwa inaongezeka sana. Vichapo vilikuwa vinatafsiriwa na kuchapishwa mu luga za mingi, na kupelekwa ku tawi zingine. Ile ilifanya kukuwe lazima ya majengo ya mupya ya Beteli. Ndugu walijenga Beteli ya muzuri sana, mangaribi mwa Johannesburg, na ikatolewa kwa Yehova mu 1987. Ilikuwa pendeleo kabisa kuchangia mu ile maendeleo na kutumika kama mushiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Afrika ya Kusini kwa miaka mingi.

MUGAO INGINE!

Mu 2001 tulishangala sana, wakati nilialikwa kuenda kutumika mu Halmashauri ya mupya ya Inchi ya Amerika, yenye ilikuwa imetoka tu kuwekwa. Hata kama tulihuzunika kuacha kazi na marafiki wetu wa Afrika ya Kusini, tulikuwa na hamu ya kuanza maisha ingine tukiwa sasa mu familia ya Beteli ya Inchi ya Amerika.

Lakini, tulikuwa na wasiwasi ya kuacha mama ya Laura, mwenye alikuwa alishazeeka. Hatungeweza kufanya mingi zaidi juu yake kama tungekuwa mu New York. Lakini dada watatu wa Laura walikuwa tayari kumutimizia mahitaji yake ya kimwili, kuhangaikia hali yake na kumutegemeza kifeza. Walituambia hivi: “Hatuwezi kuwa mu utumishi wa wakati wote, lakini kama siye tunamuhangaikia mama yetu, ile itawasaidia muendelee na mugao wenu.” Tunawashukuru sana.

Ku ngambo yangu, ndugu yangu na bibi yake, wenye walikuwa Toronto, kule Kanada, walikuwa wanamuchunga mama mwenye alikuwa sasa mujane. Mama aliishi nao kwa zaidi ya miaka 20. Tunasamini sana yote yenye walifanya kwa ajili yake mupaka wakati alikufa, siku kidogo tu kisha siye kufika New York. Ni baraka sana kuwa na watu wa familia wenye wako tayari kubadilisha maisha yao ili kuchukua madaraka fulani, yenye wakati fulani haiko mwepesi!

Kwa miaka fulani, kazi yangu ku Beteli ya Inchi ya Amerika ilikuwa mambo ya vichapo, yenye imekuwa ya kisasa na mwepesi kuliko zamani. Hivi karibuni, nilikuwa natumika mu Idara ya Mambo ya Kununua Vitu. Ni pendeleo kabisa kuwa mu hii familia ya Beteli ya mukubwa kabisa kwa muda wa miaka 20 yenye imepita. Sasa Beteli yetu iko na watu 5 000 hivi na pia wajitoleaji 2 000 hivi!

Mu miaka 60 hivi yenye imepita hakuna siku ningewaziaka kama ningekuwa hapa kwenye niko. Laura amenitegemeza sana kwa moyo wake wote mu hii miaka yote. Nimeishi maisha ya muzuri kabisa! Tunafurahia migao mbalimbali yenye tumepata na watu wazuri wenye tumetumika nao, bila kusahau wale wenye tulitembelea katika tawi mbalimbali mu dunia. Leo niko na zaidi ya miaka 80, na wamenipunguzia kazi, juu kuko ndugu vijana wengi wenye wamezoezwa.

Muandikaji moja wa zaburi aliandika hivi: “Lenye furaha ni taifa lenye Mungu wake ni Yehova.” (Zb. 33:12) Ile ni kweli kabisa! Niko mwenye shukrani sana juu nimepata nafasi ya kutumika na watu wa Yehova wenye furaha.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine