NAMNA YA KUJIFUNZA
Tumikisha Muzuri Kioo
Mutume Yakobo alilinganisha Biblia na kioo yenye inatusaidia kuona namna tuko ndani yetu. (Yak. 1:22-25) Namna gani tunaweza kutumikisha muzuri Biblia yenye kuwa sawa kioo?
Uisome kwa uangalifu. Kama tunajiangalia mbiombio mu kioo, pengine hatutaona jambo fulani ya maana yenye tunapaswa kutengeneza. Juu tuone kabisa mambo yenye tunapaswa kubadilisha ndani yetu, ni muzuri tusome kwa uangalifu kabisa Neno ya Mungu.
Ujiangalie kuliko kuangalia bengine. Kama tunapengamisha kioo tunaweza kuona mambo yenye haiendeke kwa mwingine. Vilevile tunaweza kuanza kutumia Biblia juu ya kuona makosa ya bengine. Lakini ile haitatusaidia kurekebisha makosa yetu.
Ukuwe na usawaziko. Kama tunakazia akili uzaifu wetu wenye tunaona mu kioo ya mufano, tunaweza kuvunjika moyo. Tunapaswa kuwa na usawaziko wakati tuko nasoma Neno ya Mungu. Hatupaswe kutazamia kufanya mambo mingi kupita yenye Yehova anatuomba.—Yak. 3:17.