Bandugu Bawili ba Mupya mu Baraza Yenye Kuongoza
TAREHE 5 Mwezi wa 10, 2024, tangazo ya pekee ilitolewa ku mukutano wa kila mwaka. Balitangaza kama bandugu bawili, ndugu Jody Jedele na Jacob Rumph bameongezwa mu baraza yenye kuongoza ya Mashahidi wa Yehova. Bote bawili bametumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi.
Jody Jedele na bibi yake Damaris
Ndugu Jedele alizaliwa Missouri, mu Amerika na alikomalia mu familia ya Mashahidi. Familia yake iliishi karibu na eneo yenye haikukuwa na Mashahidi mingi. Kwa hiyo alikutana na bandugu ba kutoka fasi mbalimbali benye balikuwa nakuya kusaidia kuhubiri mu ile eneo. Alibatizwa na angali kijana tarehe 15, Mwezi wa 10, 1983. Alifurahia mahubiri na wakati alimaliza masomo ya segondere alianza upainia mu Mwezi wa 9, 1989.
Wakati ndugu Jedele alikuwa kijana, bazazi yake balikuwa namubeba yeye na dada yake kutembelea Beteli. Ile ilichochea Jedele na dada yake bajitilie muradi ya kuenda ku beteli, na bote balifikia ile muradi. Ndugu Jedele alianza kutumikia ku Beteli ya Wallkill mu Mwezi wa 9, 1990. Alitumika kwanza mu usafi kisha mu mambo ya matunzo.
Ileile wakati, makutaniko ya Kihispania yenye ilikuwa karibu na Beteli ilikuwa naongezeko na balikuwa na lazima ya bandugu. Kwa hiyo ndugu Jedele alianza kukusanyikia mu kutaniko moya kati ya ile makutaniko na akaanza kujifunza Kihispania. Wakati kidogo kisha pale, ndugu Jedele alikutana na Damaris, dada painia wa mu muzunguko yabo. Balifikia kuoana na bakaanza kutumika pamoya ku Beteli.
Mu 2005 ndugu Jedele na bibi yake balitoka ku Beteli juu ya kuenda kuhangaikia bazazi yabo baaminifu. Ile wakati balikuwa mapaina wa kawaida. Ndugu Jedele alisaidia kufundisha Masomo ya Mapainia na alitumika mu Halmashauri ya Uhusiano na Hopitali na mu Halmashauri ya Eneo ya Ujenzi.
Mu 2013, Ndugu Jedele na bibi yake balialikwa tena ku Beteli juu ya kusaidia mu ujenzi wa Warwick. Tangu pale bametumikia pia Patterson na Wallkill. Ndugu Jedele ametumika pia mu LDC, na mu Biro ya Kutoa Habari Kuhusu Matunzo. Mu Mwezi wa 3, 2023, aliwekwa kuwa musaidizi wa Halmashauri ya Utumishi. Wakati anafikiria migao yake, anasema hivi: “Wakati unapata migao ya mupya, wakati fulani unaweza kuogopa. Lakini ile wakati njo unapaswa kukumbuka kumutegemea Yehova juu yeye njo anafanya kuwa.”
Jacob Rumph na bibi yake Inga
Ndugu Rumph alizaliwa Kalifornia, mu Amerika. Wakati alikuwa mutoto mama yake hakukuwa natenda, lakini alijikaza kumufundisha kweli za Biblia. Tena kila mwaka alikuwa natembelea tate yake mwanamuke mwenye alikuwa Shahidi muaminifu. Tate yake alimusaidia apende kujifunza kweli, na wakati alikuwa na miaka 13 aliomba funzo ya Biblia. Tarehe 27 Mwezi wa 9, 1992, wakati alikuwa angali kijana, alibatizwa. Jambo ya kufurahisha ni kama mama yake alianza tena kutenda na ba mwabo bote balifanya maendeleo na kubatizwa.
Wakati Ndugu Rumph alikuwa kijana aliona namna mapainia walikuwa na furaha. Kwa hiyo, wakati alimaliza masomo ya segondere alianza kufanya kazi ya upainia Mwezi wa 9, 1995. Mu mwaka wa 2000, alihamia Équateur kwenye kulikuwa lazima kubwa ya bahubiri. Kule alikutana na Inga, dada painia kutoka Kanada, na balifikia kuoana. Kisha ndoa yabo balianza kutumikia mu muji fulani wa Équateur kwenye kulikuwa kikundi ya kidogo ya bahubiri. Leo mu ile muji muko kutaniko yenye iko naendelea muzuri.
Kisha wakati fulani Ndugu Rumph na bibi yake baliwekwa kuwa mapainia wa pekee na kisha balitumikia mu muzunguko. Mu 2011 balialikwa ku darasa ya 132 ya Masomo ya Gileadi. Kisha kumaliza masomo balitumikia fasi mbalimbali mu Dunia na balifanya migao mbalimbali. Kwa mufano, balitumikia ku Beteli, balifanya kazi ya umisionere, na kazi ya muzunguko. Ndugu Rumph alipata pia pendeleo ya kufundisha ku masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme.
Juu ya ugonjwa wa Korona, Ndugu Rumph na bibi yake balirudia Amerika. Balialikwa ku Beteli ya Wallkill, kwenye Ndugu Rumph alipata mazoezi ya kutumika mu Idara ya Utumishi. Kisha balitumwa tena ku tawi ya Équateur kwenye Ndugu Rumph alitumikia mu Halmashauri ya Tawi. Mu 2023 balialikwa Warwick. Na mu Mwezi wa 1, 2024, Ndugu Rumph aliwekwa kuwa musaidizi wa Halmashauri ya Utumishi. Wakati Ndugu Rumph anafikiria kila fasi kwenye ametumikia, anasema hivi: “Kitu yenye inafanya mugao ukuwe ya pekee haiko fasi lakini ni batu benye tunatumika nabo.”
Tunapenda sana bale bandugu benye kutumika sana, na ‘tunaendelea kuheshimia watu wa namna hiyo.’—Flp. 2:29.