Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/05 uku. 3-4
  • Barua Kutoka Baraza Linaloongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Barua Kutoka Baraza Linaloongoza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Barua Kutoka Baraza Linaloongoza
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Wahubiri wa Ufalme Wapendwa:
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 3/05 uku. 3-4

Barua Kutoka Baraza Linaloongoza

KWA kuwa tupo kwenye mlango wa mfumo mpya wa mambo unaokuja, ni jambo la haraka kwamba tuendelee kumtarajia Yehova. (Sef. 3:8) Nabii Danieli alisema kwamba ‘Mungu ni Mfunuaji wa siri, naye amejulisha mambo yatakayotokea katika siku za mwisho.’ (Dan. 2:28) Ni pendeleo kabisa kuishi mwisho wa kipindi hicho kilichotabiriwa na kuelewa siri za kimungu ambazo Yehova anajulisha sasa.

Kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” Yehova alifunua hatua kwa hatua kusudi lake la kukusanya “mkutano mkubwa” wa kimataifa wa waabudu wake mnamo “siku za mwisho” hizi zenye misukosuko. (Mt. 24:45; Ufu. 7:9; 2 Tim. 3:1) Andiko la Isaya 2:2, 3 linafafanua tendo hilo la ulimwenguni pote kuwa linatukia “katika siku za mwisho.” Kila mwaka, kukusanywa huko kunaendelea katikati ya msukosuko na jeuri vinavyoenea katika ulimwengu huu.

Mnamo 2004, tumesaidia watu watii zaidi maneno haya ya Yesu: “Endeleeni kukesha . . . Iweni tayari.” (Mt. 24:42, 44) Kwa kweli, yale yanatokea katika ulimwengu yana maana kubwa kwa Wakristo, wanaotambua “ishara za nyakati” na kutenda kulingana nazo. (Mt. 16:1-3) Katika kutimiza Neno lake, Yehova ataendelea kuwa na watu wake ambao amepanga kitheokrasi ili wafanye kazi yake ijapokuwa upinzani wowote wanaopambana nao.

Ijapokuwa jitihada za watu fulani ili kuzuia au kusimamisha utangazaji wa Ufalme, ndugu zetu wanaendelea kusema juu ya ile kweli na kukusanyika pamoja. (Mdo. 5:19, 20; Ebr. 10:24, 25) Katika Urusi, mnamo Juni 2004, mahakama moja ya rufani katika Moscow iliunga mkono uamuzi wa mahakama ya chini ili kupiga marufuku utendaji wa Mashahidi wa Yehova na kulivunja shirika lao la kisheria katika Moscow. Hata hivyo, ndugu hawavunjiki moyo; wanajua kile ambacho Mungu anataka wafanye, na wanamtii kuwa Mtawala kuliko wanadamu. (Mdo. 5:29) Tuna uhakika kwamba Yehova ataongoza watumishi wake ijapokuwa upinzani wa kisheria.

Katika Jamhuri ya Georgia mnamo miaka michache iliyopita, ndugu walipoteza mali zao, wakashambuliwa na vikundi vya watu wenye jeuri, na kushuhudia kuunguzwa kwa vichapo. Lakini hakuna silaha iliyofanywa juu yao iliyofanikiwa. (Isa. 54:17) Mnamo mwaka wa utumishi wa 2004, Mashahidi wa Yehova walijulikana tena kisheria katika Georgia. Mikusanyiko ilifanywa bila kukatizwa, na vichapo kuingia kwa uwingi katika nchi bila magumu. Kumeripotiwa vilele vipya katika hesabu ya wahubiri na hudhurio kwenye Ukumbusho.

Katika Armenia, Eritrea, Jamhuri ya Korea, Rwanda na Turkmenistan, ndugu wamefungwa gerezani kwa sababu ya imani yao. Ingawa wanatendewa vibaya, wao wanajua sababu ya Kimaandiko kuhusu majaribu yao, hilo linawasaidia wadumishe utimilifu wao wanapongojea wokovu kutoka kwa Yehova.—1 Pet. 1:6; 2 Pet. 2:9.

Utakapoichunguza Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2004 katika Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 2005, utafurahia wema wa Yehova. (Zab. 31:19; 65:11) Tunatumaini kwamba ripoti hii itakutia moyo ili kuendelea kutembea katika njia inayompendeza Mungu.—1 The. 4:1.

Jitihada kubwa zinaendelea kufanywa ili kufikishia watu wa namna zote kweli. Kwa mfano, vidio, DVD na vyombo vingine katika lugha ya ishara na vichapo katika maandishi ya vipofu vimetayarishwa ili kusaidia kiroho vipofu na viziwi. Wahubiri wengi wa Ufalme wamejifunza lugha zinazosemwa na wageni wanaoishi katika eneo la kutaniko lao.

Kwa kuongezea, mamia ya vikundi vya mbali vimeundwa katika maeneo ambamo inakuwa vigumu kufikia watu. Tawi moja lina zaidi ya vikundi 300 vya mbali vyenye kuwa na wahubiri zaidi ya 7,000. Huo ni uwezekano mkubwa kabisa wa kuundwa kwa makutaniko mapya! Zaidi ya hilo, kati ya watu 16,760,607 waliohudhuria Ukumbusho mwaka huu wa utumishi, zaidi ya watu milioni 10 si Mashahidi wa Yehova. Jambo hilo ni alama yenye kuonyesha kwamba inaelekea kuna mavuno yaliyokomaa ambayo yanapaswa kuvunwa.

Tunamshukuru Yehova kwa ajili ya baraka yake yenye kutajirisha na njia ya upendo ambayo katika hiyo anatuhangaikia siku baada ya siku. (Met. 10:22; Mal. 3:10; 1 Pet. 5:7) Tunaposonga mbele kwa umoja mnamo hizi “siku za mwisho,” tumaini letu na imani yetu ni katika Yehova. Haidhuru tupambane na magumu gani, acheni tufikirie moyoni andiko letu la mwaka wa 2005: “Msaada wangu unatoka kwa Yehova.” (Zab. 121:2) Tafadhali, iweni hakika na upendo wetu na sala zetu kwa ajili yenu.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine