Wahubiri wa Ufalme Wapendwa:
‘Mungu amefuliza kukuza.’ (1 Kor. 3:6) Limekuwa jambo lenye kusisimua kama nini kuona ukuzi katika shamba la Congo zote mbili! Mnamo mwaka wa utumishi wa 2003, zaidi ya mafunzo 100,000 mapya ya Biblia yalianzishwa. Hilo ni jambo la kusifiwa.
Yehova ni mwenye kubariki kazi katika shamba letu lenye lugha nyingi. Ili kuchochea zaidi utoaji wa vichapo katika lugha fulani-fulani za eneo letu, Baraza Linaloongoza limeamua kwamba ofisi mbili za tafsiri zifunguliwe. Ofisi moja inapatikana Lubumbashi, Katanga, R.D.C., kwa ajili ya watafsiri wa lugha ya Kiluba na Uruund, na ofisi nyingine huko Mbuji-Mayi, Kasai Mashariki, R.D.C., kwa ajili ya watafsiri wa lugha ya Otetela na Tshiluba. Ofisi hizo za tafsiri zinatumika kuwa upanuzi wa Betheli. Kusudi la kuhama huko ni ili kusaidia watafsiri wawe wakati wote pamoja na watu wanaosema lugha ambazo katika hizo wanatafsiri na hivyo kujua jinsi lugha hizo zinavyoendelea.
Ili kuandaa vichapo kwa ajili ya shamba la ulimwenguni pote lenye kuongezeka, Majengo ya kuchapishia vichapo ya Watchtower Farms, karibu na Wallkill, New York, ni yenye kupanuliwa. Maendeleo mazuri ni yenye kufanywa katika kuongeza sakafu yenye ukubwa wa hektari tatu na nusu. Hiyo ni sawa na Majumba ya Ufalme 30 yenye ukubwa wa kadiri! Mashine mbili kubwa na za kisasa za kuchapishia zinapangwa kufika mapema mnamo mwaka wa 2004. Kila mashine itakuwa na uwezo wa kutoa hata magazeti 25 kwa sekunde. Vifaa vya usafirishaji na vya kuunganisha mabuku ya vitabu vitawekwa pa nafasi yavyo mnamo 2004. Hilo litatokeza utoaji mkubwa zaidi wa vitabu bila kutumia watu wengi.
Tunapoanza mwaka wa utumishi wa 2004, tunashirikiana nanyi katika sala ili Yehova ‘afulize kukuza.’
Ndugu zenu,
fisi ya Tawi ya Congo (Kinshasa)