Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 15/12 uku. 15-16
  • Umushukuru Yehova kwa Ukarimu Wake

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Umushukuru Yehova kwa Ukarimu Wake
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUFANO MUZURI ZAIDI WA UKARIMU
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mashahidi wa Yehova Wanatosha Feza Wapi?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 15/12 uku. 15-16
Mwanamuke anaingiza karte ya benki katika chombo cha kielektroniki

Umushukuru Yehova kwa Ukarimu Wake

YEHOVA ni Mungu mwenye kuonyesha ukarimu. (Yakobo 1:​17) Kila kitu chenye aliumba kinaonyesha kwamba yeye ni mukarimu. Alitia nyota nyingi sana katika anga, na aliumba miti na majani mazuri sana katika dunia.—Zaburi 65:12, 13; 147:7, 8; 148:3, 4.

Mwandikaji wa Zaburi ya 104 alimushukuru sana Yehova kwa sababu ya vitu vyote vyenye ameumba, ndiyo sababu aliandika wimbo ili kumusifu. Wakati unasoma zaburi hiyo, unamushukuru Yehova kama mwandikaji huyo? Alisema hivi: ‘Nitamuimbia Yehova katika maisha yangu yote; nitamupigia Mungu wangu muziki maadamu nipo [kadiri nitaendelea kuishi].’ (Zaburi 104:33) Unapenda kufanya hivyo pia?

MUFANO MUZURI ZAIDI WA UKARIMU

Yehova anapenda tuige ukarimu wake. Na anatutolea sababu nzuri za kuonyesha ukarimu. Alitumia roho yake ili kumuongoza mutume Paulo aandike hivi: ‘Uwapatie maagizo wale walio matajiri katika mufumo wa mambo wa sasa wasitake makubwa, na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika, bali katika Mungu, ambaye anatupatia sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie. [Uwaambie] wafanye mema, wakuwe matajiri katika matendo mazuri, wakuwe wakarimu, tayari kushiriki, wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina ya musingi muzuri kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.’—1 Timotheo 6:17-19.

Katika barua yake ya pili kwa Wakorintho, mutume Paulo alieleza nia yenye tunapaswa kuwa nayo wakati tunatolea wengine. Alisema hivi: ‘Kila mumoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutoaji muchangamufu.’ (2 Wakorintho 9:7) Wakati tunaonyesha ukarimu, ni nani mwenye anapata faida? Mutume Paulo alisema kwamba tunasaidia wengine kwa kuwatolea mambo yenye wako nayo lazima, lakini pia tunajisaidia sisi wenyewe kwa sababu Yehova atatubariki.—2 Wakorintho 9:11-14.

Mutume Paulo alizungumuzia mufano muzuri zaidi wa ukarimu wa Mungu wakati alisema hivi: “Shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” (2 Wakorintho 9:15) ‘Zawadi ya bure’ ya Yehova ni mambo yote mazuri yenye anatutolea kupitia Yesu Kristo. Hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kuonyesha kwamba zawadi hiyo ni ya maana sana.

Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani kwa ajili ya mambo yote yenye Yehova na Yesu wametufanyia na yenye watatufanyia? Njia moja ni kuwa wakarimu wakati tunatoa wakati, nguvu, na vitu vyetu vya kimwili kwa ajili ya ibada ya Yehova na kusaidia wengine wajifunze kumujua. Tunaweza kufanya hivyo iwe tuko na vitu vingi ao vidogo.—1 Mambo ya Nyakati 22:14; 29:3-5; Luka 21:1-4.

NJIA MBALIMBALI ZA KUTOA MICHANGO

Kama vile Wakristo wa wakati wa mitume, leo ndugu na dada wengi wanaweka pembeni feza za kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote na kuzitia katika visanduku vya michango katika kutaniko lao. (1 Wakorintho. 16:2) Kila mwezi, makutaniko inatuma feza hizo kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova yenye kusimamia kazi ya kuhubiri katika inchi yao. Unaweza pia kutuma wewe mwenyewe michango yako kwenye shirika lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu. Ili kujua shirika lenye kukubaliwa kisheria lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu, andikia biro ya tawi ya inchi yenu. Unaweza kupata adresi ya biro ya tawi kwenye www.jw.org.

KUKOPESHA BIRO YA TAWI FEZA

  • Unaweza kukopesha “Association Les Témoins de Jéhovah” feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote.

  • Wakati utakuwa na lazima ya feza zako, biro ya tawi itakurudishia feza hizo bila kukuongezea faida yoyote. Ili kupata habari zaidi unaweza kutumia namba hii ya telefone: 0998189791 ao 0815551000

MIPANGO MINGINE INAYOHUSU MICHANGO

Kuko njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Njia hizo ni:

Bima ao Asiranse: Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namna ya kufanya.

Akaunti za Benki: Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.” Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti yenye atatumia ili kutuma zawadi yake.

Nyumba ao Parsele: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakufa. Mbele ya kutoa zawadi kama hiyo unapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ya inchi yenu.

Zawadi: Ni mupango wa kutoa feza ao vitu vingine ili vikuwe mali ya shirika fulani lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia. Ule mwenye anapenda kutoa zawadi ili kutegemeza kazi ya Ufalme, anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi yenye anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

Wasia ao testama:Shirika la “Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo, mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango mingine inayohusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Broshua Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide katika Kihispania na Kiingereza, imetayarishwa ili kuwasaidia watu wenye wanapenda kutoa michango ili kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri ulimwenguni pote iendelee. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa, ao kama uriti wakati mutu anakufa. Kisha kusoma broshua hiyo na kupata mashauri ya washauri wao wa mambo ya kisheria ao kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wakati wanafanya hivyo. Ikiwa unapenda kupata broshua hiyo unaweza kuiomba kwenye biro ya tawi.

Ili kupata habari zaidi, unaweza kuzungumuza na biro ya tawi. Unaweza pia kutuma barua kwenye adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita namba zenye kupatikana hapa chini.

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-KINSHASA, République Démocratique du Congo.

Telefone: 0998189791 ao 0815551000

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine