MUENDELEE KUKESHA!
Watu Milioni 6 Wamekufa na Coronavirus—Biblia Inasema Nini?
Kulingana na Shirika ya Afya Ulimwenguni (OMS), tarehe 23, Mwezi wa 5, 2022, hesabu ya watu wenye walikufa na Coronavirus ilikuwa milioni 6.27. Lakini, mu ripoti ya mupya yenye ilitolewa tarehe 5, Mwezi wa 5, 2022, Shirika ya Afya Ulimwenguni ilikadiria kama hesabu ya watu wenye walikufa na coronavirus inaweza kuwa kubwa zaidi. Ilionyesha kama mu mwaka wa 2020 na 2021, “hesabu ya watu wenye walikufa moja kwa moja ao mu njia yenye haiko ya moja kwa moja na Coronavirus . . . ilikuwa karibu milioni 14.9.” Biblia inasema jambo fulani kuhusu ugonjwa wa vile wenye kuhuzunisha sana?
Biblia ilitabiri kama kutakuwa magonjwa ya nguvu sana ya kuambukiza
Yesu alitabiri kama kutakuwa “magonjwa ya kuambukiza,” mu kipindi yenye inaitwa “siku za mwisho.”—Luka 21:11; 2 Timoteo 3:1.
Unabii wa Yesu uko natimia leo. Juu ya kujua mambo mingi zaidi, soma habari “Ni Nini Ishara ya “Siku za Mwisho?“
Biblia inatufariji
“Mungu wa faraja yote . . . anatufariji katika majaribu yetu yote.”—2 Wakorinto 1:3, 4.
Watu wengi wenye wamepoteza mupendwa wao wamefarijiwa na mambo yenye Biblia inasema. Jifunze mambo mingi kwa kusoma habari “Namna ya Kupambana na Huzuni—Mambo Yenye Unaweza Kufanya Leo“ na “Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa.“
Biblia inaonyesha namna ile hali itaishaka
“Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.”—Matayo 6:10.
Karibuni “Ufalme wa Mungu” utamaliza magumu yote na “hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’” (Marko 1:14, 15; Isaya 33:24) Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini? ili kujua mambo mingi juu ya Ufalme wa Mungu na mambo yenye utafanya.
Tunakuomba ujifunze zaidi kuhusu mambo yenye Biblia inasema juu mashauri yake ya hekima na ahadi za muzuri zenye inatoa zikuletee faida weye na familia yako.