Kushoto: Hurricane Ian, Florida, Amerika, Mwezi wa 9, 2022 (Sean Rayford/Getty Images); katikati: Mama iko nakimbia na mutoto wake mwanaume, Donetsk, Ukraine, Mwezi wa 7, 2022 (Alex Chan Tsz Yuk/SOPA Images/LightRocket via Getty Images); kuume: Vipimo vya korona, Beijing, Chine, Mwezi wa 4, 2022 (Kevin Frayer/Getty Images)
MUENDELEE KUKESHA!
2022: Mwaka wa Wasiwasi—Biblia inasema Nini?
Mu 2022, vyombo vya habari vilizungumuzia sana mambo ya vita, magumu ya kupata makuta, na misiba. Ni Biblia tu njo inaonyesha maana ya ile matukio.
Maana ya matukio ya mu 2022
Matukio ya mwaka wenye karibuni utaisha inaonyesha kama tuko naishi mu kipindi yenye Biblia inaita “siku za mwisho.” (2 Timoteo 3:1) Ile kipindi ilianza mu mwaka wa 1914. Ona namna matukio yenye ilitokea hivi karibuni inapatana na mambo yenye Biblia ilisemaka kuhusu siku zetu:
“Vita.”—Matayo 24:6.
“Mu mwaka wa 2022 vita ilirudia tena mu Ulaya.”a
Ona habari “Urusi Inashambulia Ukraine.”
“Upungufu wa chakula.”—Matayo 24:7.
“2022: Mwaka wa njala yenye haiyatokeaka.”b
Ona habari “Vita ya Ukraine Imefanya Chakula Ikosekane mu Dunia Yote.”
“Magonjwa ya kuambukiza.”—Luka 21:11.
“Magonjwa ya polio, variole du singe na korona inaendelea kutesa watu. Ile ni magonjwa hatari na yenye kuambukiza na yenye ilionyesha ni kwa kiasi gani watu ni wazaifu.”c
Ona Habari “Watu Milioni 6 Wamekufa na Coronavirus.”
“Mambo yenye kuogopesha.”—Luka 21:11.
“Kifukutu sana, kipwa ya nguvu, moto wa pori, na kuyala kwa maji mingi ya mvua. Kusema kweli, tutaendelea kukumbuka wakati wenye ulikaribia kipindi ya joto ya mu 2022 juu ya matukio mingi sana na ya nguvu ya hali ya hewa yenye iliharibisha vitu mingi, yenye iliua maelfu ya watu, na yenye ilifanya mamilioni ya watu wapoteze nyumba zao.”d
Ona habari “Mu Dunia Yote Muko Kifukutu Sana Kupita Kawaida.”
“Machafuko [ao, “misukosuko,” maelezo ya chini].”—Luka 21:9.
“Watu walikasirika sana juu ya magumu ya kupata makuta, zaidi sana juu bei ya vitu ilipanda. Ile ilichochea watu wafanye maandamano ya nguvu sana ya kupinga serikali mu 2022.”e
Ona habari “Bei ya Vitu Imepanda mu Dunia Yote.”
Nini njo itatokea mwaka kesho?
Hakuna mutu mwenye anajua kabisa mambo yenye itatokea mu 2023. Tunajua tu kama hivi karibuni Ufalme wa Mungu ao serikali ya mbinguni njo italeta mabadiliko makubwa hapa ku dunia. (Danieli 2:44) Ile serikali itamaliza jambo yenye inafanya watu wateseke na itafanya mapenzi ya Mungu itendeke hapa ku dunia.—Matayo 6:9, 10.
Tunakuomba ufuate shauri ya Yesu Kristo ya ‘kuendelea kukesha’ ili kuona namna matukio ya mu dunia iko natimiza unabii wa Biblia. (Marko 13:37) Tafazali, unaweza kutuita ao kutuandikia kama unapenda kujua mambo mingi zaidi juu ya namna Biblia inaweza kukusaidia leo na namna inaweza kukupatia weye na familia yako tumaini ya kweli juu ya namna mambo itakuwa muzuri.
a AP News, ‘Mu mwaka wa 2022 vita ilirudia tena mu Ulaya,’ ilitolewa na Jill Lawless, tarehe 8 Mwezi wa 12, 2022.
b Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Ulimwenguni, ‘Mwaka wa njala yenye haiyatokeaka.’
c JAMA Health Forum, ‘Kuishi mu kipindi ya magonjwa ya kuambukiza—Kuanzia korona mupaka ku variole de singe, Polio, na magonjwa ingine ( Disease X),’ ilitolewa na Lawrence O. Gostin, JD, tarehe 22 Mwezi wa 9, 2022.
d Earth.Org, ‘Juu ya nini kulikuwa matukio makubwa ya hali ya hewa mu wakati wenye ulikaribia kipindi ya joto ya mu 2022?’ ilitolewa na Martina Igini, tarehe 24 Mwezi wa 10, 2022.
e Carnegie Endowment for International Peace, ‘Kasirani yenye ilisababishwa na magumu ya kupata makuta ilichochea watu wafanye maandamano ya kupinga serikali mu 2022,’ ilitolewa na Thomas Carothers na Benjamin Feldman, tarehe 8 Mwezi wa 12, 2022.