MUENDELEE KUKESHA!
Kupigwa Masasi ku Masomo—Biblia Inasema Nini?
Tarehe 24, Mwezi wa 5, 2022, jambo fulani ya mubaya sana ilitokea mu muji mudogo wa Uvalde, Texas, Amerika. Kulingana na gazeti The New York Times, “mwanaume mwenye kubeba bunduki aliua watoto 19 na walimu wawili . . . ku Masomo ya Musingi ya Robb.”
Jambo ya kuhuzunisha, matukio ya vile imeenea sana. Gazeti USA Today ilisema kama mu Amerika peke yake, “kupigwa masasi ku masomo kulitokea mara 249 mwaka jana, ile hesabu inapita miaka ingine yote tangu 1970.”
Juu ya nini ile mambo ya mubaya ilitokea? Tunaweza kufanya nini juu ya kupambana na ile matendo ya mubaya sana? Jeuri itaishaka? Biblia inajibia ile maulizo.
Juu ya nini jeuri imeongezeka sana leo?
Biblia inaita kipindi yetu “siku za mwisho,” na inaonyesha kama mu hii kipindi watu wengi ‘hawatakuwa na upendo wa asili’ na watakuwa “wakali,” ni kusema, wenye kufanya mambo ya kukosa huruma. Wale wenye kuwa na tabia za vile “wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.” (2 Timoteo 3:1-5, 13) Juu ya kujua mambo mingi zaidi, soma habari “Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?”
Watu wengi wanajiulizaka, ‘Juu ya nini Mungu hazuie mambo ya mubaya sana sawa vile kuua watu na masasi ku masomo?’ Juu ya kupata jibu ya Biblia, soma habari “Mambo Mabaya Yanafikia Watu Wazuri—Sababu Gani?”
Nini njo inaweza kutusaidia kupambana na ile hali?
“Mambo yote yenye yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili . . . kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.”—Waroma 15:4.
Kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kupambana na jeuri yenye kuwa mu hii dunia. Juu ya kupata habari zaidi, ona gazeti Amuka! yenye kichwa “Je, Jeuri Itawahi Kwisha?”
Juu ya kupata mashauri kuhusu namna wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wajue namna wanaweza kupambana na habari za kuogopesha, soma habari “Je, Taarifa za Habari Zenye Kuogopesha Zinawaathiri Watoto Wako?”
Jeuri itaishaka?
“Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:14.
“Watafua panga zao kuwa majembe na mikuki yao kuwa miundu.Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”—Mika 4:3.
Mungu atafanya mambo yenye wanadamu hawawezi kufanya. Serikali yake ya mbinguni itaharibu silaha zote na kumaliza jeuri yote. Juu ya kupata habari zaidi kuhusu mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya, soma habari “Chini ya Ufalme wa Mungu ‘Amani Itakuwa Nyingi.’”