Manuel Reino Berengui/DeFodi Images via Getty Images
MUENDELEE KUKESHA!
Je, Kombe ya Dunia Inaweza Kabisa Kuunganisha Watu?—Biblia Inasema Nini?
Watu miliare tano hivi wanatazamiwa kuangalia Kombe ya Dunia (Coupe du Monde) ya FIFA yenye ilianza tarehe 20 Mwezi wa 11, 2022 mupaka tarehe 18 Mwezi wa 12, 2022. Watu wengi wanawaza kama ile michezo inaweza kuunganisha watu wenye wako naiangalia na kama inaweza pia kutimiza mambo ingine.
“Muchezo uko na nguvu ya kubadilisha dunia. Uko na nguvu ya kuchochea. Uko na nguvu ya kuunganisha watu mu njia ya pekee.”—Nelson Mandela, mwenye alikuwaka raisi wa Afrika ya Kusini.
“Muchezo wa kabumbu . . . Unaunganisha watu juu unawafanya wakuwe na tumaini, furaha, uchangamufu, upendo na wakuwe na jambo yenye inawapatanisha.”—Gianni Infantino, raisi wa FIFA.a
Kombe ya Dunia ao muchezo wowote unaweza kutimiza ile mambo yote? Kuko siku watu wataunganishwa na kuishi kwa amani?
Je, Kombe ya Dunia Inaweza Kabisa Kuunganisha Watu?
Kombe ya Dunia ya hii mwaka inafanya watu wawaze mambo mingi zaidi. Kuliko tu kuizungumuzia, wanaanza kuzungumuzia mambo ingine, sawa vile mambo ya maisha na mambo ya politike yenye inahusu haki za wanadamu, ubaguzi wa rangi, na kukosa usawa mu mambo ya uchumi.
Hata vile, watu wengi wameona kama matukio ya michezo ya mu dunia yote, sawa vile Kombe ya Dunia inafanyaka watu wajifurahishe. Lakini, hata kama wanaipenda namna gani, haiwezi kuwaunganisha milele. Kuliko kufanya vile, mara mingi inawatenganishaka na kuwafanya wakuwe na tabia zenye Biblia ilisemaka zamani kama watu watakuwa nazo mu kipindi yenye inaitwa “siku za mwisho.”—2 Timoteo 3:1-5.
Tumaini ya kweli kuhusu kuunganishwa kwa watu mu dunia
Biblia inazungumuzia tumaini ya kweli juu ya kuunganishwa kwa watu mu dunia yote. Inaahidi kama watu wote mu dunia wataunganishwa na serikali ya mbinguni yenye kuitwa “Ufalme wa Mungu.”—Luka 4:43; Matayo 6:10.
Yesu Kristo, Mufalme wa ule Ufalme, atafanya kukuwe kabisa amani mu dunia yote. Biblia inasema hivi:
“Mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi.”—Zaburi 72:7.
“Ataokoa maskini mwenye kulilia musaada . . . Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:12, 14.
Mafundisho ya Yesu ilishaunganisha mamilioni ya watu mu inchi 239 hata leo. Watu wamejifunza kuacha kuchukia wengine. Juu ya kujua mambo mingi zaidi, soma habari mbalimbali chini ya kichwa“Mambo ya Kufanya Juu ya Kuachana na Chuki.”
a Fédération Internationale de Football Association, the international governing body for association football (soccer).