Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 39
  • Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matibabu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matunzo?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Pinga Ibilisi na Njia Zake za Kudanganya
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?
    Amuka!—2017
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 39

Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?

Jibu la Biblia

Ndiyo. Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake wanaweza kutafuta matunzo ya kiganga aliposema kwamba ‘watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomuhitaji ni wale walio wagonjwa.’ (Mathayo 9:12, BIBLIA HABARI NJEMA) Biblia si kitabu cha kiganga, lakini inatoa kanuni zinazoweza kuwasaidia wale wanaotaka kumupendeza Mungu.

Maulizo unayopaswa kufikiria

1. Je, ninaelewa matunzo ambayo ninashauriwa kupata? Biblia inatushauri tutafute muongozo muzuri kuliko ‘kuamini kila neno.’—Methali 14:15.

2. Je, nitafute mashauri kwa waganga wengine? Ndiyo, kuwauliza “washauri wengi” kunaweza kukusaidia, zaidi sana ikiwa umegonjwa sana.—Methali 15:22.

3. Je, aina hii ya matunzo inapingana na sheria ya Mungu inayowaomba Wakristo “wajiepushe . . . na damu”?—Matendo 15:20.

4. Je, aina hii ya matunzo ina uhusiano na mambo ya uchawi? Biblia inakataza “mazoea ya kuwasiliana na pepo.” (Wagalatia 5:19-21) Ili kujua ikiwa inahusiana na uchawi, jiulize maulizo haya:

  • Je, muganga huyu wa kienyeji anazungumuza na mashetani?

  • Je, aina hii ya matunzo inategemea maoni ya kwamba magonjwa yanatokea kwa sababu miungu imekasirika ao kwa sababu ya maadui wanaotumia uchawi?

  • Je, zabihu, nyimbo za uchawi, ao desturi zingine za kupashana habari na mashetani zinatumiwa wakati wa kutengeneza dawa hiyo?

5. Je, nimeanza kuhangaikia afya yangu kupita kiasi? Biblia inashauri hivi: “Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Kuwa mwenye usawaziko kutakusaidia ukazie uangalifu “mambo yaliyo ya maana zaidi,” kama vile mambo ya kiroho.—Wafilipi 1:10; Mathayo 5:3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine