Siku ya Tano, 29 Mwezi wa 8
Nimewajulisha jina lako.—Yoh. 17:26.
Yesu hakuambia tu watu kama jina ya Mungu ni Yehova. Wayahudi wenye Yesu alifundisha, tayari walikuwa najua jina ya Mungu. Lakini Yesu alikuwa ule “mwenye . . . alieleza juu Yake.” (Yoh. 1:17, 18) Kwa mufano, Maandiko ya Kiebrania inaonyesha kama Yehova iko na rehema na huruma. (Kut. 34:5-7) Yesu alisaidia watu waelewe zaidi ile kweli wakati alieleza mufano wa mwana mupotevu na baba yake. Wakati tunasoma namna ule baba aliona mutoto wake “wakati alikuwa angali mbali,” namna alikimbia ili kukutana naye, namna alimukumbatia, na kumusamehe kwa moyo wote, tunaelewa muzuri zaidi rehema na huruma ya Yehova. (Lu. 15:11-32) Yesu alionyesha waziwazi Baba yake ni mutu wa namna gani. w24.02 10 fu. 8-9
Siku ya Posho, 30 Mwezi wa 8
Kufariji wengine . . . namna yoyote kupitia faraja yenye tunapokea kutoka kwa Mungu.—2 Ko. 1:4.
Yehova anafanyaka wale wenye kuwa na huzuni wajisikie muzuri na wafarijike. Kama Yehova, namna gani na siye tunaweza kusikilia wengine huruma na kuwafariji? Njia moja ya kufanya vile ni kukomalisha katika moyo wetu sifa zenye zinaweza kutusaidia tufariji wengine. Ni sifa gani? Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na upendo wenye utatuchochea “tuendelee kufarijiana” kila siku? (1 Te. 4:18) Tunapaswa kukomalisha sifa sawa vile kujitia pa nafasi ya wengine, kuwa na upendo wa kindugu, na fazili. (Kol. 3:12; 1 Pe. 3:8) Zile sifa zitatusaidia namna gani? Wakati tunakuwa na huruma na hizi sifa zingine, tutakuwa na hamu sana ya kufariji wale wenye kuwa mu magumu. Sawa vile Yesu alisema “kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo. Mutu muzuri anatosha mambo ya muzuri katika hazina yake ya muzuri.” (Mt. 12:34, 35) Kufariji ndugu na dada wakati wako na lazima kabisa ya faraja ni njia ya muzuri sana ya kuonyesha kama tunawapenda. w23.11 10 fu. 10-11
Siku ya Yenga, 31 Mwezi wa 8
Wale wenye kuwa na ufahamu wataelewa.—Da. 12:10.
Tunapaswa kuomba musaada kama tunapenda kuelewa maunabii yenye kuwa mu Biblia. Fikiria hii mufano. Wazia weye na rafiki yako muko naenda fasi fulani yenye haujue, lakini ule rafiki yako anajua ile fasi muzuri. Anajua muzuri kabisa kwenye muko na anajua muzuri fasi kwenye kila barabara inaishia. Bila shaka, utafurahi juu ule rafiki yako aliitika uende naye! Vilevile, Yehova anajua muzuri kipindi yenye tuko naishi na kwenye tuko naenda. Kwa hiyo, juu tuelewe maunabii yenye kuwa mu Biblia, tunapaswa kumuomba Yehova kwa unyenyekevu ili atusaidie. (Da. 2:28; 2 Pe. 1:19, 20) Sawa vile muzazi yeyote muzuri, Yehova anapenda watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuya. (Yer. 29:11) Lakini, tofauti na muzazi yeyote, Yehova anaweza kutuambia bila kukosea mambo yenye itafanyika wakati wenye kuya. Aliandikisha maunabii mu Neno yake ili itusaidie kujua matukio makubwa mbele hata itokee.—Isa. 46:10. w23.08 8 fu. 3-4