Siku ya Posho, 30 Mwezi wa 8
Kufariji wengine . . . namna yoyote kupitia faraja yenye tunapokea kutoka kwa Mungu.—2 Ko. 1:4.
Yehova anafanyaka wale wenye kuwa na huzuni wajisikie muzuri na wafarijike. Kama Yehova, namna gani na siye tunaweza kusikilia wengine huruma na kuwafariji? Njia moja ya kufanya vile ni kukomalisha katika moyo wetu sifa zenye zinaweza kutusaidia tufariji wengine. Ni sifa gani? Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na upendo wenye utatuchochea “tuendelee kufarijiana” kila siku? (1 Te. 4:18) Tunapaswa kukomalisha sifa sawa vile kujitia pa nafasi ya wengine, kuwa na upendo wa kindugu, na fazili. (Kol. 3:12; 1 Pe. 3:8) Zile sifa zitatusaidia namna gani? Wakati tunakuwa na huruma na hizi sifa zingine, tutakuwa na hamu sana ya kufariji wale wenye kuwa mu magumu. Sawa vile Yesu alisema “kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo. Mutu muzuri anatosha mambo ya muzuri katika hazina yake ya muzuri.” (Mt. 12:34, 35) Kufariji ndugu na dada wakati wako na lazima kabisa ya faraja ni njia ya muzuri sana ya kuonyesha kama tunawapenda. w23.11 10 fu. 10-11
Siku ya Yenga, 31 Mwezi wa 8
Wale wenye kuwa na ufahamu wataelewa.—Da. 12:10.
Tunapaswa kuomba musaada kama tunapenda kuelewa maunabii yenye kuwa mu Biblia. Fikiria hii mufano. Wazia weye na rafiki yako muko naenda fasi fulani yenye haujue, lakini ule rafiki yako anajua ile fasi muzuri. Anajua muzuri kabisa kwenye muko na anajua muzuri fasi kwenye kila barabara inaishia. Bila shaka, utafurahi juu ule rafiki yako aliitika uende naye! Vilevile, Yehova anajua muzuri kipindi yenye tuko naishi na kwenye tuko naenda. Kwa hiyo, juu tuelewe maunabii yenye kuwa mu Biblia, tunapaswa kumuomba Yehova kwa unyenyekevu ili atusaidie. (Da. 2:28; 2 Pe. 1:19, 20) Sawa vile muzazi yeyote muzuri, Yehova anapenda watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuya. (Yer. 29:11) Lakini, tofauti na muzazi yeyote, Yehova anaweza kutuambia bila kukosea mambo yenye itafanyika wakati wenye kuya. Aliandikisha maunabii mu Neno yake ili itusaidie kujua matukio makubwa mbele hata itokee.—Isa. 46:10. w23.08 8 fu. 3-4
Siku ya Kwanza, 1 Mwezi wa 9
Mwangaza wa asubui utatufikia kutoka juu.—Lu. 1:78.
Mungu amepatia Yesu nguvu ya kumaliza magumu yote ya wanadamu. Miujiza yenye Yesu alifanya ilionyesha kama iko na nguvu ya kumaliza magumu yenye hatuwezi kumaliza siye wenyewe. Kwa mufano, iko na nguvu ya kutosha jambo yenye imefanya wanadamu wakuwe mu magumu, ni kusema, zambi yenye waliriti na pia matokeo yake, yenye ni magonjwa na kifo. (Mt. 9:1-6; Ro. 5:12, 18, 19) Kupitia miujiza yake, alionyesha kama iko na nguvu ya kuponyesha “kila namna ya” magonjwa na kama iko na nguvu ya kufufua wafu. (Mt. 4:23; Yoh. 11:43, 44) Tena, iko na nguvu ya kutuliza zoruba yenye upepo mukali na kufukuza pepo wachafu. (Mk. 4:37-39; Lu. 8:2) Inatia moyo kabisa kuona kama Yehova amepatia Mwana wake nguvu ya kufanya ile mambo yote! Tuko hakika kabisa kama ahadi zote za mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utaleta, zitatimia. Miujiza yenye Yesu alifanya wakati alikuwa mwanadamu hapa ku dunia, inatufundisha kama wakati ataanza kutawala dunia, atatufanyia mambo mingi sana ya muzuri. w23.04 3 fu. 5-7