Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/10 uku. 1
  • Je, Ninastahili Kuhubiri?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Ninastahili Kuhubiri?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Nani Anayestahili Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 1/10 uku. 1

Je, Ninastahili Kuhubiri?

1. Kwa nini hatupaswi kufikiri kwamba hatustahili kuhubiri?

1 Ikiwa siku fulani ulizo hilo linakuja akilini mwako, jipe moyo sana! Si kusoma masomo ao kuzaliwa na uwezo fulani kunakotufanya tustahili kuwa wahubiri. Kati ya wanafunzi wa karne ya kwanza, kulikuwa wale walioitwa “wasio na elimu na wa kawaida tu.” Hata hivyo, walikuwa wahubiri wa habari njema wenye matokeo mazuri kwa kuwa walikuwa na kusudi la kufuata mfano ambao Yesu aliwawekea.—Mdo. 4:13; 1 Pet. 2:21.

2. Mafundisho ya Yesu yalikuwa ya namna gani?

2 Jinsi Yesu Alivyofundisha: Mafundisho yake yalikuwa mepesi, yenye kufaa watu wa kawaida, na yenye kueleweka kwa urahisi. Maulizo yake, mifano yake na maneno yenye kueleweka kwa urahisi aliyotumia ili kuanzisha mazungumzo yalivutia watu waliomsikiliza. (Mt. 6:26) Alipendezwa kabisa na watu. (Mt. 14:14) Zaidi ya hiyo, Yesu alizungumza akiwa na uhakika na mamlaka, kwa kuwa alijua kwamba Yehova alimtuma na alimtia nguvu ili kutimiza kazi yake.—Luka 4:18.

3. Namna gani Yehova anatusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri?

3 Yehova Anatusaidia: Kupitia Neno lake na tengenezo lake, Mfundishaji wetu Mkuu anatutolea mazoezi tunayohitaji ili tuwe wenye matokeo mazuri katika kuhubiri habari njema. (Isa. 54:13) Kwa kuwa Yehova alifanya kwamba mambo yanayohusu njia za Yesu za kufundisha yaandikwe na kulindwa, tunaweza kuchunguza na kuiga njia za Yesu za kufundisha. Yehova anatupa roho yake takatifu na anatutolea mazoezi kupitia mikutano ya kutaniko. (Yoh. 14:26) Pia, anatutolea wahubiri wanaozoea kazi ya kuhubiri ambao wanaweza kutusaidia tuwe wahubiri wenye matokeo zaidi.

4. Kwa nini tuna sababu ya kujisikia kwamba tunastahili kuwahubiria wengine habari njema?

4 Tuna sababu nyingi za kutufanya tujisikie kwamba tunastahili kuhubiri, kwa sababu “kuwa kwetu na sifa za kustahili vya kutosha hutoka kwa Mungu.” (2 Kor. 3:5) Tunapomtegemea Yehova kwa kutumia vizuri na kwa uaminifu mambo anayotutolea kwa upendo, tutakuwa “na uwezo kamili, na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.”—2 Tim. 3:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine