Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/96 uku. 1-3
  • Nani Anayestahili Kuhubiri?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Nani Anayestahili Kuhubiri?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Ninastahili Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • “Hubiri Neno”
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 9/96 uku. 1-3

Nani Anayestahili Kuhubiri?

1 Je! umekwisha kuhisi maoni ya moyoni kama yale yale ya Musa kuhusu huduma? Alisema: “Ee [Yehova], mimi si musemaji, wala zamani wala tangu uliposema na mutumishi wako; kwa maana mimi ni polepole kwa kusema, na mwenye ulimi muzito.” (Kut. 4:​10, ZSB) Ikiwa unakubaliana na maoni hayo ya moyoni, labda yanakomesha mahubiri yako. Hata hivyo, Yesu “alituagiza sisi tuwahubiri” watu na kutoa ushahidi kamili. (Mdo. 10:​42, NW) Jinsi gani basi kuwa wahubiri wenye kustahili wa habari njema?

2 Si kiwango chetu cha elimu kinachotufanya tustahili kwa ajili ya huduma. Paulo alisema kwamba “si wengi wenye hekima katika njia ya kimwili walioitwa” na kwamba “hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu.” (1 Kor. 1:26; 3:​19, NW) Yesu aliwachagua mitume wake kati ya watu wa tabaka ya chini; yapata wanne hivi kati yao walikuwa wavuvi mastadi. Viongozi wa kidini wenye kiburi walikuwa wakiwaona kwa dharau kama “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” Wakihukumiwa kulingana na viwango vya ulimwengu, mitume hawakuwa wenye kustahili kuhubiri. Hata hivyo, hotuba maalumu ambayo Petro alitoa siku ya Pentekote ilichochea watu 3,000 kubatizwa!​—Mdo. 2:14, 37-41; 4:13.

3 Yehova Anatufanya Tuwe Wenye Kustahili Kuhubiri: Paulo alisema: “Uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu.” (2 Kor. 3:​5, HNWW) Yehova, Chanzo cha hekima, alifundisha mamilioni ya wanadamu ili kwamba wahubiri kwa wengine ukweli kuhusu Ufalme. (Is. 54:13) Kazi hiyo ni yenye matokeo na inazaa matunda mengi: ushuhuda ni mwaka wa nyuma (1995) wapya waliobatizwa 338,491 ambao ni “barua za pendekezo” zilizo hai. (2 Kor. 3:1-3, NW) Yote hayo yanatusadikisha kuhubiri kwa uhodari na imani yale Yehova alitufundisha.

4 Tengenezo la Mungu liliweka programu ya ulimwenguni pote ya mazoezi kwa wahudumu wake. Kwa njia ya Maandiko na kwa vichapo mbalimbali vya kibiblia, tunafundishwa na kuzoezwa ili kuwa ‘wenye kustahili kikamili, waliovalia kabisa vifaa’ kwa ajili ya kuhubiri. (2 Tim. 3:16, 17, NW) Watu wengi walishangazwa na akili ya juu inayoonyeshwa na vichapo vya Sosaiti. Angalia, kwa mfano, yale tuliyosoma katika gazeti la Kiswidini: “Imani ambayo Mashahidi wa Yehova huhubiri inaonyesha akili kubwa ya Biblia na inashuhudia utafiti wa ajabu wa ulimwenguni pote.”

5 Pamoja na maagizo ambayo tunapokea wakati wa mikutano mitano ya kila juma, programu yetu ya usomaji na funzo la Biblia, mashauri ambayo tunafaidika nayo kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, msaada wa kibinafsi ambao tunaletewa na wahudumu wengine wenye ujuzi na, zaidi ya yote, tegemezo la roho takatifu ya Yehova, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova anatuona kuwa wenye kustahili kikamili kuhubiri. ‘Ndiyo, kama waliotumwa kutoka kwa Mungu, chini ya mwono wa Mungu, kwa ushirika na Kristo, tunasema.’​— 2 Kor. 2:​17, NW.

6 Ikiwa tunafaidika kikamili na mazoezi ya kitheokrasi ambayo Mungu anatutolea kwa njia ya tengenezo lake, hatuna sababu yoyote ya kusimamisha au ya kuogopeshwa. Tuwahubirie wengine kwa shangwe, tukiwa hakika kwamba Yehova atabariki jitihada yetu.​—1 Kor. 3:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine