Tutumie Nguvu Zetu kwa Hekima Tunapohubiri
1. Namna gani maneno ya 1 Wakorintho 9:26 yanaweza kutumiwa kuhusiana na kazi yetu ya kuhubiri?
1 Mutume Paulo aliandika hivi: “Jinsi ninavyokimbia si bila uhakika; jinsi ninavyoelekeza ngumi zangu ni ili nisiwe nikipiga hewa.” (1 Kor. 9:26) Katika andiko hili, Paulo alikuwa akizungumuzia namna alivyokazia akili yake juu ya miradi ya kumutumikia Yehova vizuri zaidi. Lakini, maneno hayo yanaweza kutumiwa kuhusiana na kazi yetu ya kuhubiri. Sisi tuna nia ya kuelekeza “ngumi,” ao nguvu zetu kwa hekima ili tuweze kutimiza kazi nzuri zaidi. Namna gani?
2. Namna gani tunaweza kumuiga Paulo na wahubiri wengine wa wakati wake kuhusu kuchagua wakati na mahali pa kuhubiri?
2 Tuende Mahali Watu Wako: Paulo na wahubiri wengine wa wakati wake walikuwa wakitafuta mahali watu wako ili kuwahubiria. (Mdo. 5:42; 16:13; 17:17) Kwa hiyo, ikiwa watu wengi katika eneo letu wanapatikana nyumbani kwao mangaribi, huo unaweza kuwa ndio wakati muzuri zaidi wa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ikiwa mahali pa kungojea motokari ao treni panajaa watu asubui wakati watu wanaenda kazini na mangaribi wakati watu wanarudi, hizo ndizo saa nzuri zaidi za kufanya mahubiri ya barabarani mahali hapo. Ni vizuri kujua pia wakati ambapo mahali pa biashara panajaa watu ili kufanya mahubiri ya barabarani.
3. Jinsi gani tunaweza kutumia nguvu zetu kwa hekima kuhusiana na jinsi tunavyotumika katika eneo letu?
3 Tutumike kwa Hekima Tunapohubiri Katika Eneo: Tunapaswa pia kutumia nguvu zetu kwa hekima kuhusiana na jinsi tunavyotumika katika eneo letu. Kwa mufano, kuliko kwenda katika eneo moja tukiwa kikundi cha watu wengi, ni vizuri zaidi kuwagawanya watu hao. Kufanya hivyo kutasaidia tusipoteze wakati mwingi na nguvu ili kushugulikia kikundi hicho. Ni vivyo hivyo tunapoenda kuhubiri katika eneo lililo mbali na muji wetu ao kijiji, inaomba kupanga wahubiri vizuri ili eneo lote lihubiriwe kwa haraka na kila muhubiri apate nafasi ya kuzungumuza na watu. Pia unaweza kuomba eneo lako la kuhubiri karibu na mahali unapoishi ili kupunguza muda wa safari.
4. Ni nini itakayotusaidia kuwa “wavuvi wa watu” wenye matokeo?
4 Yesu alifananisha wahubiri na “wavuvi wa watu.” (Marko 1:17) Muradi wa muvuvi ni kunasa samaki wala si kutupa tu wavu ndani ya maji. Ndio sababu wavuvi wenye matokeo wanaenda kuvua wakati na mahali ambapo samaki wanaweza kupatikana. Wanapofika huko, wanaanza kuvua samaki bila kukawia. Kwa kufanya hivyo, wanatumia nguvu zao kwa hekima. Sisi pia tuonyeshe bidii hiyohiyo katika kazi yetu ya kuhubiri.—Ebr. 6:11.