Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/13 uku. 1
  • Tuige Mufano wa Manabii—Amosi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Mufano wa Manabii—Amosi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 9/13 uku. 1

Tuige Mufano wa Manabii​—Amosi

1. Sababu gani mufano wa Amosi unaweza kututia moyo?

1 Je, umekwisha kujisikia haustahili kuhubiri kwa sababu haukusoma mingi ao kwa sababu ulizaliwa katika familia maskini? Ikiwa ni hivyo, mufano wa Amosi unaweza kukutia moyo. Alikuwa muchungaji wa kondoo na alifanya kazi ya kulima wakati fulani​-fulani katika mwaka, lakini Yehova alimutia nguvu ili atoe ujumbe wa maana. (Amo. 1:1; 7:14, 15) Katika siku zetu pia, Yehova anatumia watu wanyenyekevu na ambao wanaishi maisha ya kawaida. (1 Kor. 1:27-29) Mufano wa nabii Amosi unaweza kutufundisha mambo mengine gani kuhusiana na kazi yetu ya kuhubiri?

2. Sababu gani tunaweza kubaki imara tunapopambana na upinzani katika mahubiri?

2 Tubaki Imara Tunapopambana na Upinzani: Wakati Amazia, kuhani wa ibada ya sanamu ya kitoto cha ngombe katika ufalme wa kaskazini wa yale makabila kumi ya Israeli, alisikia unabii wa Amosi, ni kama vile alijibu: ‘Rudi kwako! Utuache huru! Sisi tuna dini yetu!’ (Amo. 7:12, 13) Amazia alimushitaki kwa uongo nabii huyo alipomuomba Mufalme Yeroboamu azuie kazi ya Amosi. (Amo. 7:7-11) Lakini Amosi hakuogopa. Leo pia, viongozi wa kidini wanatafuta musaada wa viongozi wa serikali ili kuwatesa watu wa Yehova. Hata hivyo, Yehova anatuhakikishia kwamba silaha yoyote itakayofanywa juu yetu haitafanikiwa kwa wakati murefu.​—Isa. 54:17.

3. Ujumbe tunaotangaza una sehemu mbili gani?

3 Tutangaze Hukumu ya Yehova na Baraka za Wakati Ujao: Hata ikiwa Amosi alitabiri hukumu juu ya ufalme wa kaskazini wa yale makabila kumi ya Israeli, alimalizia kitabu chake kwa kuzungumuzia ahadi ya Yehova ya kurudishwa kwa watu wake na kuwatolea baraka nyingi. (Amo. 9:13-15) Sisi pia tunazungumuzia ‘siku ya Mungu ya hukumu’ inayokuja, lakini hiyo ni sehemu tu ya “habari njema ya ufalme” ambayo tunapaswa kutangaza. (2 Pet. 3:7; Mt. 24:14) Yehova atawaharibu waovu kwenye Armagedoni, na kisha dunia itakuwa paradiso.​—Zab. 37:34.

4. Sababu gani tuko hakika kwamba tunaweza kuendelea kufanya mapenzi ya Yehova?

4 Bila shaka, kuhubiri ujumbe wa Ufalme katika dunia iliyo na wapinzani wengi kunatia azimio letu la kujitoa kwa Yehova na kufanya mapenzi yake katika jaribu. (Yoh. 15:19) Hata hivyo, tuko hakika kwamba Yehova ataendelea kututolea mambo tunayohitaji ili kufanya mapenzi yake, kama alivyomufanyia Amosi.​—2 Kor. 3:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine