Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr18 Mwezi wa 9 uku. 1-7
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 3-9/09
  • TAREHE 10-16/09
  • TAREHE 17-23/09
  • TAREHE 24-30/09
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
mwbr18 Mwezi wa 9 uku. 1-7

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 3-9/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 1-2

“Yesu Anafanya Muujiza Wake wa Kwanza”

w15 15/6 uku. 4 fu. 3

Kristo Nguvu za Mungu

Yesu alifanya muujiza wake wa kwanza ku karamu ya ndoa yenye ilifanyika Kana, kule Galilaya. Pengine watu wenye walifika walikuwa wengi zaidi kuliko wale wenye walialikwa. Ikuwe ni vile ao hapana, divai iliisha. Maria, mama ya Yesu, alikuwa kati ya watu wenye walialikwa. Ni wazi kama, kwa muda wa miaka mingi Maria alifikiria sana unabii wote wenye ulihusu mutoto yake, mwenye angeitwa “Mwana wa Aliye Juu Zaidi.” (Luka 1:30-32; 2:52) Maria aliamini kama ule mutoto alikuwa na nguvu fulani zenye alikuwa hajaonyesha? Mambo ilionekana wazi ku karamu ya ndoa kule Kana. Maria na Yesu walisikilia huruma wale wenye walikuwa wameoana, na walipenda kuwasaidia ili wasipate haya. Yesu alijua kama wale wenye walikuwa wameoana walipaswa kuonyesha ukarimu watu wenye walialika. Kwa hiyo, aligeuza kwa njia ya muujiza litre 380 ya maji kuwa “divai ya muzuri.” (Soma Yohana 2:3, 6-11.) Yesu alilazimishwa kufanya muujiza? Hapana. Alionyesha tu kama alihangaikia watu na kama alikuwa anamuiga Baba yake wa mbinguni kwa kuonyesha ukarimu.

jy uku. 41 fu. 6

Anafanya Muujiza Wake Wa Kwanza

Huu ndio muujiza wa kwanza wenye Yesu anafanya. Wakati wanafunzi wake wa kwanza wanaona muujiza huo, wanamuamini kabisa. Kisha hapo, Yesu, mama yake, na ndugu-nusu zake wanasafiri kuenda muji wa Kapernaumu upande wa kaskazini-mangaribi pembeni ya Bahari ya Galilaya.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 1:1

Neno: Ao “Logos.” Katika Kigiriki, ho loʹgos. Hapa neno ho loʹgos linatumiwa kama cheo, na linatumiwa pia mu Yoh 1:14 na Ufu 19:13. Yohana alionyesha kama mwenye hii cheo ni Yesu. Alikuwa nayo wakati alikuwa kiumbe wa roho kule mbinguni, wakati alikuwa mwanadamu mukamilifu katika dunia, na kisha kupata utukufu kule mbinguni. Yesu alikuwa Neno ao Musemaji mwenye Mungu alikuwa anatumia ili kutolea maagizo watoto wake wengine, ni kusema, viumbe wa roho na wanadamu pia. Kwa hiyo, ni jambo lenye kupatana na akili kusema kama, mbele Yesu akuje katika dunia, Yehova alizungumuza na wanadamu kupitia Neno, malaika musemaji Wake.​—Mwa 16:7-11; 22:11; 31:11; Kut 3:2-5; Amu 2:1-4; 6:11, 12; 13:3.

Pamoja na: Neno kwa neno, “kuelekea.” Hapa, neno la Kigiriki pros linatoa wazo la urafiki wa karibu sana na ushirikiano. Linaonyesha pia watu tofauti, ni kusema, Neno iko tofauti kabisa na Mungu wa pekee wa kweli.

Neno alikuwa mungu: Ao “Neno alikuwa wa kimungu [ao alifanana na Mungu].” Hii maneno ya Yohana inataja sifa ao kitambulisho cha “Neno,” ni kusema, Yesu Kristo (Kigiriki, ho loʹgos; ona kwa ajili ya funzo kuhusu Neno katika hii andiko.) Neno anaitwa “mungu; kufanana na Mungu, wa kimungu, wa aina ya Mungu” kwa sababu alikuwa na cheo ya juu sana, ni kusema, Mutoto muzaliwa wa kwanza wa Mungu mwenye kupitia yeye Mungu aliumba vitu vingine vyote. Watafsiri wengi wanapendelea kutafsiri “Neno alikuwa Mungu;” kwao, Neno ni Mungu Mweza-Yote. Lakini, kuko sababu nyingi zenye kuturuhusu kusema kama Yohana hakumaanisha kama “Neno” alikuwa Mungu Mweza-Yote. Kwanza, maneno yenye kutangulia na yenye kufuata inaonyesha wazi kama “Neno” alikuwa “pamoja na Mungu.” Tena, neno la Kigiriki the·osʹ linapatikana mara tatu mu mustari wa 1 na wa 2. Kwenye linapatikana mara ya kwanza na mara ya tatu, neno the·osʹ linaanza na kibainishi bayana (article défini) mu Kigiriki; kwenye linapatikana mara ya pili, halina kibainishi bayana. Wasomi wengi wanakubaliana kama kukosa kibainishi bayana kwenye neno the·osʹ linapatikana mara ya pili kuko na maana fulani. Wakati kibainishi bayana kinatumiwa, the·osʹ inamaanisha Mungu Mweza-Yote. Kwa upande mwingine, wakati kibainishi bayana hakitumiwe, kulingana na sarufi ya Kigiriki, the·osʹ inakuwa sifa, ni kusema, sifa yenye kutambulisha “Neno.” Ndiyo sababu tafsiri mbalimbali za Biblia za Kiingereza, Kifaransa na Kijerumani zinatafsiri hii andiko karibu sawa-sawa na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, ni kusema, zinatoa wazo ya kama “Neno” alikuwa “mungu; wa kimungu; wa hali fulani ya kimungu; wa aina fulani ya mungu; alifanana na Mungu.” Watafsiri wa zamani wa Injili ya Yohana wa luga ya Kisahidi (luga ndogo yenye kutokana na luga ya Kikoptiki), Injili yenye ilitolewa pengine mu miaka ya 300 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, inatafsiri neno the·osʹ mahali linapatikana kwa mara ya kwanza mu Yohana 1:1, tofauti na mahali linapatikana kwa mara ya pili. Kutafsiri namna hiyo kunakazia sifa ya “Neno,” kwa kusema kama alikuwa wa aina ya Mungu, lakini hawaseme kama alikuwa sawasawa na Baba yake, Mungu Mweza-Yote. Kol 2:9 inategemeza pia hii andiko wakati inasema kama “ujazo wote wa sifa ya Mungu unakaa” ndani ya Kristo. Na kulingana na 2Pe 1:4, hata wale wenye watariti pamoja na Kristo watakuwa “washiriki katika asili ya Mungu.” Kwa kuongezea, mu tafsiri ya Septante, neno la Kigiriki the·osʹ ni neno lile-lile lenye kutumiwa ili kutafsiri maneno ya Kiebrania ʼel na ʼelo·himʹ yenye kutafsiriwa “Mungu,” maneno yenye wanawaza inaleta wazo kubwa la “Mweza-Yote; Mwenye-Nguvu.” Maneno ya Kiebrania ʼel na ʼelo·himʹ inatumiwa ili kuzungumuzia Mungu Mweza-Yote, miungu mingine, na wanadamu. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 10:34.) Kumuita Yesu “mungu,” ao “mwenye nguvu,” kunategemeza unabii wa Isaya 9:6, wenye ulisema kama Masiya angeitwa “Mungu Mwenye Nguvu” (hapana “Mungu Mweza-Yote”) na kama angekuwa “Baba wa Milele” kwa wote wenye watapata pendeleo la kuwa raia wa utawala wake. Bidii ya Baba yake mwenyewe, “Yehova wa majeshi,” itatenda mambo hayo.​—Isa 9:7.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 1:29

Mwana-Kondoo wa Mungu: Kisha Yesu kubatizwa na kutoka kujaribiwa na shetani, Yohana mubatizaji alimutaja kuwa “Mwana-Kondoo wa Mungu.” Hii maneno inapatikana tu mu Yoh 1:36. Kufananisha Yesu na mwana-kondoo kunafaa kabisa. Mu Biblia, kondoo walitolewa ili kukubali zambi na kumukaribia Mungu. Kufanya vile kulionyesha mbele ya wakati zabihu yenye Yesu angefanya kwa kutoa uzima wake mukamifu kwa ajili ya wanadamu. Maneno “mwana-kondoo wa Mungu” inakumbusha Maandiko mengi ya Maandishi yenye kuongozwa na roho takatifu. Kwa sababu Yohana Mubatizaji alijua muzuri Maandiko ya Kiebrania, pengine maneno yake ilitokana na mambo kama vile: mwana-kondoo mwenye Abrahamu alitoa pa nafasi ya Isaka mutoto wake (Mwa 22:13), mwana-kondoo wa Pasaka mwenye walichinja ili kukombelewa mu utumwa wa Misri. (Kut 12:1-13), ao mwana-kondoo dume mwenye alitolewa kwenye mazabahu ya Mungu kule Yerusalemu kila asubuhi na kila mangaribi. (Kut 29:38-42). Pengine tena Yohana alikuwa anafikiria unabii wa Isaya; mwenye mutu mwenye Yehova anaita “mutumishi wangu,” “alipelekwa kama kondoo mwenye anaenda kuchinjwa.” (Isa 52:13; 53:5, 7, 11) Wakati mutume Paulo aliandika barua yake ya kwanza kwa Wakorinto, alimutaja Yesu kuwa “kondoo wetu wa Pasaka.” (1Kor 5:7) Mutume Petro alizungumuzia damu ya Kristo na kusema kama ilikuwa “yenye samani, kama ile ya mwana-kondoo mwenye hana kasoro na mwenye hana doa.” (1Pe 1:19) Na zaidi ya mara 25 mu kitabu cha Ufunuo, kisha kutukuzwa, Yesu anatajwa kuwa “Mwana-Kondoo” wa mufano.​—Kwa mufano, ona: Ufu 5:8; 6:1; 7:9; 12:11; 13:8; 14:1; 15:3; 17:14; 19:7; 21:9; 22:1.

TAREHE 10-16/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 3-4

“Yesu Anahubiria Mwanamuke Musamaria”

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 4:6

kwa kuwa alikuwa amechoka: Mu Maandiko yote, ni hapa tu imeandikwa kama Yesu “alikuwa amechoka.” Ilikuwa karibu 12h00 ya muchana, na asubui ya ile siku, pengine Yesu alitembea safari kutoka Bonde la Yordani kule Yudea mupaka Sikari kule Samaria, eneo lenye kuinuka kwenye urefu wa metre 900 ao zaidi.​—Yoh 4:3-5.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 3:29

rafiki ya bwana-arusi: Zamani, rafiki ya bwana-arusi alikuwa anamusimamia mbele ya serikali na alikuwa wa maana ili kupanga ndoa. Watu waliona kama ni yeye alifanya mipango ili bibi na bwana-arusi wakutane. Siku ya arusi, bibi na bwana-arusi pamoja na watu wenye waliwasindikiza walikuwa wanafikia kwa bwana-arusi, ao kwa baba yake, kwenye arusi ingefanywa. Wakati wa karamu ya ndoa, rafiki ya bwana-arusi, alikuwa mwenye furaha sana wakati alikuwa anasikia sauti ya bwana-arusi anazungumuza na bibi-arusi, kwa sababu ile ilikuwa inamufanya ajisikie kama ametimiza muzuri daraka lake. Yohana mubatizaji alijifananisha na “rafiki ya bwana-arusi.” Ni kusema, Yesu alikuwa bwana-arusi na wanafunzi walikuwa kikundi chenye kufanyiza bibi arusi wa mufano. Kwa kumutayarishia Masiya njia, Yohana Mubatizaji alipendekeza kwa Yesu Kristo watu wa kwanza-kwanza wenye kufanyiza “bibi-arusi.” (Yoh 1:29, 35; 2Ko 11:2; Efe 5:22-27; Ufu 21:2, 9) “Rafiki ya bwana-arusi” alitimiza muzuri daraka lake kwa sababu pendekezo lake lilikubaliwa; hakukuwa tena mutu wa maana sana. Ndiyo sababu Yohana alisema hivi juu yake mwenyewe na juu ya Yesu: “Huyo anapaswa kuendelea kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupunguka.”​—Yoh 3:30.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 4:10

maji ya uzima: Neno la Kigiriki lenye kutumiwa hapa halitumiwe kwa njia ya mufano, linamaanisha kabisa maji yenye kuteremuka, ao maji ya chemchemi, ao maji ya kisima chenye kujazwa na chemchemi fulani. Ni tofauti na maji yenye kuwa tu ndani ya kisima yenye haiteremuke. Mu Law 14:5, neno la Kiebrania lenye kumaanisha “maji yanayotiririka” ao “maji yenye yalishotwa kwenye muto” linatafsiriwa neno kwa neno “maji ya uzima.” Mu Yer 2:13 na 17:13, Yehova anatajwa kuwa “chemchemi ya maji ya uzima,” ni kusema, maji ya mufano yenye kuleta uzima. Wakati alikuwa anazungumuza na mwanamuke Musamaria, Yesu alitumia neno maji ya uzima kwa njia ya mufano, lakini inaonekana kama ule mwanamuke alifikiri kama Yesu anazungumuzia maji ya kweli.​—Yoh 4:11; ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 4:14.

TAREHE 17-23/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 5-6

“Umufuate Yesu na Nia ya Muzuri”

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:10

wanaume wakakaa, walikuwa karibu elfu tano (5 000): Ni Matayo tu anaongeza maneno “bila kuhesabia wanamuke na watoto wadogo” wakati anazungumuzia huu muujiza. (Mt 14:21) Inawezekana watu wenye walikulishwa kwa njia ya muujiza walikuwa zaidi ya 15 000.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:14

Nabii: Wayahudi wa wakati wa mitume walikuwa wanangojea nabii kama Musa, mwenye kutajwa mu Kum 18:15, 18, na angekuwa Masiya. Kwa hiyo, pengine maneno kuja katika ulimwengu inahusu kuja kwa Masiya mwenye walikuwa wanangojea. Ni Yohana tu alizungumuzia mambo yenye kutajwa mu hii andiko.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:27, 54

chakula chenye kinaharibikaka . . . chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele: Yesu alielewa kama watu fulani walikuwa wanamufuata yeye na wanafunzi wake ili tu awatimizie mahitaji yao ya kimwili. Chakula cha kimwili kinasaidia watu waishi kila siku, lakini “chakula” chenye kutoka katika Neno la Mungu kitasaidia wanadamu waishi milele. Yesu anaomba watu wafanye kazi kwa ajili ya “chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele,” ni kusema, wanapaswa kufanya nguvu ili kutimiza mahitaji yao ya kiroho, na kuamini mambo wanajifunza.​—Mt 4:4; 5:3; Yoh 6:28-39.

anakula mwili wangu na kunywa damu yangu: Hapa, watu wanakula na kunywa kwa njia ya mufano kwa kumuamini Yesu Kristo. (Yoh 6:35, 40) Yesu alisema hii maneno mu mwaka wa 32; kwa hiyo hatuwezi kusema kama alikuwa anazungumuzia Chakula cha Bwana cha Mangaribi chenye angeanzisha kisha mwaka moja. Alisema hii maneno wakati fulani tu mbele ya “Pasaka, sikukuu ya Wayahudi” (Yoh 6:4); kwa hiyo, pengine wasikilizaji wake walikumbuka sikukuu yenye ilikuwa karibu kufika na walikumbuka namna damu ya mwana-kondoo iliokoa uzima wa watu wengi usiku wenye Waisraeli walitoka Misri (Kut 12:24-27). Yesu alikuwa anakazia kama damu yake pia ingekuwa ya maana sana ili iwezeshe wanafunzi wake wapate uzima wa milele.

w05 1/9 uku. 21 fu. 13-14

Tutatembea Katika Jina la Yehova Mungu Wetu

Hata hivyo, kama vile Yohana anasema, wale watu walifanya yao yote ili kumufuata Yesu na wakamupata “ngambo ya bahari.” Juu ya nini walimufuata kisha yeye kukataa wamufanye kuwa mufalme wao? Wengi walikuwa wanaona mambo kwa njia ya kimwili tu, waliendelea kuzungumuzia waziwazi chakula chenye Yehova alitolea watu wake mu jangwa wakati wa Musa. Ni kama vile walitaka Yesu aendelee kuwapatia chakula cha kimwili. Wakati Yesu alitambua nia yao ya mubaya, alianza kuwafundisha kweli za kiroho zenye zingeweza kubadilisha mawazo yao. (Yohana 6:17, 24, 25, 30, 31, 35-40) Njo maana, wengine walianza kumunungunikia, zaidi sana wakati alisema hivi: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kama hamukule mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamuna uzima ndani yenu wenyewe. Kila mutu mwenye anakula mwili wangu na kunywa damu yangu iko na uzima wa milele, na mimi nitamufufua katika siku ya mwisho.”​—Yohana 6:53, 54.

Mara nyingi mifano ya Yesu ilichochea watu waonyeshe kama kweli kabisa walipenda kutembea pamoja na Mungu. Hii mufano ilitimiza pia ile kusudi. Iliumiza wamoja kati yao. Tunasoma hivi: “Wengi kati ya wanafunzi wake wakasema: ‘Maneno hayo ni yenye kuchukiza; ni nani mwenye anaweza kuyasikiliza?’” Kisha Yesu akawaelezea kama wanapaswa kuelewa maneno yake kwa njia ya kiroho. Alisema: “Roho ndiyo inatoa uzima; mwili hauna faida hata kidogo. Maneno yenye nimewaambia ni roho na ni uzima.” Lakini wengi hawakutaka kusikiliza. Ile habari inasema: “Kwa sababu ya jambo hili, wengi kati ya wanafunzi wake wakaenda kwenye mambo yenye yalikuwa nyuma na hawakutembea tena pamoja naye.”​—Yohana 6:60, 63, 66.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:44

amuvute: Hata kama tendo la Kigiriki lenye kutafsiriwa “amuvute” linatumiwa kwa ajili ya wavu (makila) ya kuvua samaki (Yoh 21:6, 11), halimaanishe kama Mungu anawavuta watu kwa kuwakaza. Tendo hilo linaweza pia kumaanisha “kuvuta,” na maneno ya Yesu inaweza pia kutumiwa kuhusu Yer 31:3, mwenye Yehova anaambia watu wake wa zamani: “Nimekuvuta kwangu kwa upendo mushikamanifu” (Tafsiri ya Septante inatumia neno lilelile la Kigiriki mu hii andiko.) Yoh 12:32 inaonyesha hivyo pia, Yesu anavuta kwake watu wa namna zote. Maandiko inatuambia kama Yehova amepatia wanadamu uhuru wa kuchagua. Kila mutu iko huru kuchagua kumutumikia ao hapana. (Kum 30:19, 20) Kwa upole Mungu anavuta kwake watu wenye kuwa na moyo wenye mwelekeo wenye kufaa. (Zab 11:5; Mez 21:2; Mdo 13:48) Yehova anafanya vile kupitia ujumbe wa Biblia na kupitia roho yake takatifu. Unabii wa Isa 54:13, wenye kutajwa mu Yoh 6:45, unahusu wale wenye kuvutiwa na Baba.​—Linganisha na Yoh 6:65.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:64

Yesu alijua . . . ule mwenye angemusaliti: Yesu alikuwa anazungumuzia Yuda Iskariote. Yesu alisali Baba yake usiku muzima mbele achague mitume wake 12. (Lu 6:12-16) Kwa hiyo, ku mwanzo Yuda alikuwa muaminifu kwa Mungu. Lakini, Yesu alijua kupitia Maandiko ya Kiebrania kama rafiki yake wa sana angemutoa. (Zab 41:9; 109:8; Yoh 13:18, 19) Wakati Yuda alianza kuwa na mwelekeo mubaya Yesu, mwenye iko na uwezo wa kusoma ndani ya moyo na mawazo, aliona namna Yuda anaanza kubadilika. (Mt 9:4) Mungu alitumia uwezo wake wa kujua mambo mbele ya wakati ili kuona namna mutu fulani mwenye Yesu alikuwa anaaminia angemutoa. Lakini kulingana na sifa za Mungu na namna yake ya kutenda tangu zamani, hatuwezi kusema kama alikuwa amepanga tangu zamani kama ni Yuda alipaswa tu kumutoa Yesu.

tangu mwanzo: Hii maneno haimaanishe wakati Yuda alizaliwa ao wakati alichaguliwa kuwa mutume kisha Yesu kusali usiku muzima. (Lu 6:12-16) Lakini inamaanisha wakati Yuda alianza kutenda kwa udanganyifu, jambo lenye Yesu alitambua mara moja. (Yoh 2:24, 25; Ufu 1:1; 2:23; ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 6:70; 13:11.) Hii jambo inaonyesha pia kama Yuda alipanga kutenda mambo yake na alitenda kwa makusudi, haikuwa matokeo ya moyo kubadilika tu haraka. Maana ya neno “mwanzo” (Kigiriki, ar·kheʹ) mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inategemea habari yenye kuzungumuziwa. Kwa mufano, kwenye 2Pe 3:4, neno “mwanzo” linamaanisha mwanzo wa uumbaji. Lakini mara nyingi linatumiwa katika maana kidogo. Kwa mufano, Petro alisema kama roho takatifu iliangukia juu ya Watu wa Mataifa “kama vile ilituangukia pale mwanzo” (Mdo 11:15) Petro hakukuwa anazungumuzia mwanzo wa kuzaliwa kwake ao wakati walimuita akuwe mutume. Lakini alikuwa anazungumuzia siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, ni kusema, “mwanzo” wa kushuka kwa roho takatifu kwa kusudi la pekee. (Mdo 2:1-4) Mifano ingine yenye kuonyesha namna maana ya neno “mwanzo” inategemea habari yenye kuzungumuziwa inapatikana mu Lu 1:2; Yoh 15:27; na 1Yo 2:7.

TAREHE 24-30/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 7-8

“Yesu Alitukuza Baba Yake”

cf uku. 100-101 fu. 5-6

“Imeandikwa”

Yesu alitaka watu wajue kwenye ujumbe wake ulitoka. Alisema: “Mambo yenye ninafundisha haiko yangu, lakini ni ya ule mwenye alinituma.” (Yohana 7:16) Wakati mwingine, alisema: “Sifanye jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe; lakini kama vile Baba alinifundisha, ni vile ninasema mambo haya.” (Yohana 8:28) Pia, alisema: “Mambo yenye ninawaambia ninyi, siyaseme kwa kujitungia mimi mwenyewe, lakini Baba mwenye anakaa katika umoja na mimi anafanya kazi zake.” (Yohana 14:10) Njia moja yenye Yesu alionyesha ukweli wa hii maneno ni kwa kurudilia tena na tena Neno la Mungu lenye liliandikwa.

Kuchunguza kwa uangalifu maneno ya Yesu yenye iliandikwa kunafunua kama alirudilia moja kwa moja ao kwa njia yenye haiko ya moja kwa moja zaidi ya nusu ya vitabu vya Maandiko ya Kiebrania vyenye kukubaliwa. Pengine hauone hapa jambo la kushangaza. Pengine unajiuliza, mu kazi yake ya kufundisha na kuhubiri waziwazi, yenye alifanya kwa miaka tatu na nusu, sababu gani hakurudilia vitabu vyote vyenye viliongozwa na roho vyenye vilikuwa ile wakati? Lakini, pengine alifanya vile. Usisahau kama waliandika tu sehemu kidogo ya maneno na matendo ya Yesu. (Yohana 21:25) Unaweza hata kutumia saa fulani tu ili kusoma kwa sauti maneno yote ya Yesu yenye iliandikwa. Sasa, wazia unazungumuza juu ya Mungu na Ufalme wake kwa saa kidogo na wakati unazungumuza, unarudilia zaidi ya nusu ya vitabu vya Maandiko ya Kiebrania! Tena, mara nyingi Yesu hakukuwa na vitabu vya kukunjwa. Wakati wa Mahubiri yake ya ku Mulima, yenye inajulikana sana, alitaja moja kwa moja ao kwa njia yenye haiko ya moja kwa moja Maandiko mengi ya Kiebrania yenye alikuwa anachunga mu akili!

w11 15/3 uku. 11 fu. 19

Pokea Roho ya Mungu, Hapana Roho ya Ulimwengu

Umutii Yehova kabisa. Sikuzote Yesu alifanya mambo yenye ilimupendeza Baba yake. Wakati fulani, alikuwa na mawazo tofauti na Baba yake juu ya namna ya kutenda mu hali fulani. Lakini, alimuambia Baba yake hivi bila kusita: “Lakini, mapenzi yako ndiyo yatendeke, hapana yangu.” (Luka 22:42) Ujiulize hivi: ‘Ninamutii Mungu hata wakati haiko mwepesi?’ Kumutii Mungu ni jambo la maana ili kupata uzima. Tunapaswa kumutii kabisa yeye Mutengenezaji wetu, Chanzo na Mutegemezaji wa uzima wetu. (Zab. 95:6, 7) Hakuna jambo lenye linaweza kuchukua nafasi ya utii. Mungu hawezi kutukubali kama hatuna utii.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w07 1/2 uku. 6 fu. 4

Sababu Gani Tuzoee Kusema Kweli?

Yesu Kristo alionyesha mufano gani juu ya kusema kweli? Wakati moja, alikuwa anazungumuza na watu fulani wenye hawamuamini wenye walitaka kujua mipango yake ya kusafiri. Walimushauria hivi: “Toka hapa uende Yudea.” Yesu aliwaambia nini? “Ninyi muende [Yerusalemu] kwenye sikukuu; mimi sitapanda sasa kuenda kwenye sikukuu hiyo, kwa sababu wakati wangu haujafika kabisa.” Lakini, kisha muda mufupi, Yesu alisafiri kuenda Yerusalemu kwa ajili ya ile sikukuu. Juu ya nini aliwaambia vile? Hawakustahili kujua mahali alikuwa. Kwa hiyo, hata kama hakusema uongo, hakuwapatia habari zote pengine ili kuwazuia wasimutendee mubaya ao wasitendee mubaya wanafunzi wake. Hakusema uongo kwa sababu mutume Petro aliandika hivi juu ya Kristo: “Yeye hakufanya zambi, na udanganyifu haukupatikana katika kinywa chake.”​—Yohana 7:1-13; 1 Petro 2:22.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 8:58

mimi nilikuwa: Wayahudi wapinzani walitafuta kumupiga Yesu majiwe kwa sababu, namna walisema, Yeye [Yesu] mwenye hajakuwa “hata na miaka makumi tano (50),” anasema kama ‘amekwisha kumuona Abrahamu.’ (Yoh 8:57) Ili kuwajibia, anawaelezea juu ya maisha yake mbele azaliwe mwanadamu, anasema alikuwa kiumbe wa roho mwenye nguvu mbinguni mbele Abrahamu azaliwe. Watu fulani wanasema hii andiko inaonyesha wazi kama Yesu ni Mungu. Ili kujitetea wanasema kama neno la Kigiriki lenye kutumiwa hapa, e·goʹ ei·miʹ (lenye mu Biblia fulani linatafsiriwa “Mimi niko”), linatokana na tafsiri ya Septante mwenye andiko ya Kutoka 3:14 inatafsiriwa vile pia, na wanasema kama ile maandiko ingine ilipaswa pia kutafsiriwa vile. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 4:26.) Lakini, mu hii andiko, tendo la Kigiriki ei·miʹ lilianza “mbele Abrahamu azaliwe” na lilikuwa linaendelea. Kwa hiyo, kulitafsiri “Mimi nilikuwa” ni muzuri kuliko “Mimi niko,” na tafsiri fulani za zamani na za sasa zinatumia maneno yenye kufanana “Mimi nilikuwa.” Kwa mufano, mu Yoh 14:9, ile namna ya tendo la Kigiriki ei·miʹ inatumiwa ili kutafsiri hii maneno ya Yesu: “Hata kisha mimi kuwa pamoja na ninyi kwa wakati murefu vile, Filipo, bado haujanijua?” Tafsiri nyingi zinatumia maneno ya namna vile, jambo lenye kuonyesha wazi kama, kulingana na habari yenye kuzungumuziwa, sarufi haikataze kutafsiri ei·miʹ kuwa “mimi nilikuwa,” (Mifano ingine ya kutafsiri tendo la Kigiriki kwa kutumia tendo la wakati wenye ulipita na lenye kuendelea sasa inapatikana mu Lu 2:48; 13:7; 15:29; Yoh 1:9; 5:6; 15:27; Mdo 15:21; 2Ko 12:19; 1Yo 3:8.) Tena, maneno ya Yesu yenye kupatikana mu Yoh 8:54, 55 inaonyesha kama hakutafuta kujionyesha kuwa sawa na Baba yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine