MAISHA YA MUKRISTO
Unaweza Kuhubiri na Kufundisha!
Ku mwanzo, wakati Yehova alimupatia kazi ya kufanya, Musa aliwaza kama hataiweza. (Kut 4:10, 13) Na wewe ulishaka jisikia vile? Unajifunzaka Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova? Unajiulizaka kama kuko siku utaweza kuhubiri nyumba kwa nyumba? Ao pengine uko kijana na uko unaogopa kuhubiri kwenye masomo. Ao pengine unaogopa kuhubiri kupitia telefone ao kufanya aina fulani ya mahubiri ya mahali pa watu wengi. Usali kwa Yehova na umuombe akupatie roho yake takatifu ili ikutie nguvu. (1Pe 4:11) Ukuwe hakika kama anaweza kukusaidia ili utimize mugao wowote wenye anakupatia.—Kut 4:11, 12.
MUANGALIE VIDEO UKUWE HODARI . . . MUHUBIRI, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Dada Aoyama alipambana na magumu gani?
Nini njo ilimusaidia akuwe na nguvu na akuwe na uhodari?—Yer 20:7-9
Alipata faida gani kwa sababu alijikaza kufanya mengi mu kazi ya Yehova?
Yehova anaweza kukusaidia upambane na magumu gani mu mahubiri?