Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 57 1-5
  • Unapaswa Kufanya Nini Kama Unaangukia mu Zambi Nzito?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unapaswa Kufanya Nini Kama Unaangukia mu Zambi Nzito?
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • ‘Ita Bazee’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Namna ya Kuonyesha Watenda-zambi Upendo na Rehema
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Namna Kutaniko Inapangwa
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna Wazee Wanaweza Kusaidia Wenye Wanaondolewa mu Kutaniko
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 57 1-5
Somo ya 57. Ndugu kijana anatubu zambi nzito mbele ya wazee wawili ku Jumba ya Ufalme.

SOMO YA 57

Unapaswa Kufanya Nini Kama Unaangukia mu Zambi Nzito?

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Hata kama unamupenda Yehova sana na unajikazaka sana juu usifanye jambo fulani yenye inaweza kumuumiza, wakati fulani utafanya makosa. Lakini, zambi fulani ziko nzito kuliko zingine. (1 Wakorinto 6:9, 10) Kama unafanya zambi nzito, ukumbuke kama Yehova angali anakupenda; iko tayari kukusamehe na kukusaidia.

1. Tunapaswa kufanya nini juu Yehova atusamehe?

Watu wenye wanamupenda Yehova wanahuzunikaka sana wakati wanatambua kama wamefanya zambi nzito. Lakini, hii maneno ya Yehova inawapatiaka nguvu: “Hata kama zambi zenu ziko na rangi nyekundu yenye kungaa, zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji.” (Isaya 1:18) Kama tunatubu kwa moyo wote, Yehova atatusamehe kabisa. Tunapaswa kufanya nini ili kuonyesha kama tunatubu? Tunapaswa kuhuzunikia sana mambo yenye tulifanya, kuacha kufanya ile mambo, na kumulilia Yehova atusamehe. Kisha tunapaswa kujikaza kubadilisha mawazo ao tabia za mubaya zenye zilifanya tuangukie mu ile zambi. Na tunapaswa kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yetu.​—Soma Isaya 55:6, 7.

2. Kama tunaangukia mu zambi nzito, wazee wanafanyaka nini juu ya kutusaidia?

Kama tunafanya zambi nzito, Yehova anatuambia ‘tuite wazee wa kutaniko.’ (Soma Yakobo 5:14, 15.) Wale wazee wanamupenda Yehova na wanapenda watu wake. Wamefundishwa namna wanaweza kutusaidia juu tukuwe tena na urafiki muzuri na Yehova.​—Wagalatia 6:1.

Wazee wanaweza kufanya nini juu ya kutusaidia kama tunaangukia mu zambi nzito? Wazee wawili ao watatu watatumia mashauri yenye iko mu Biblia juu ya kuturekebisha. Na watatuambia mambo yenye tunaweza kufanya juu tuepuke kuangukia tena mu zambi. Kama mutu anafanya zambi nzito lakini hatubu, wazee watamuondoa mu kutaniko juu asichochee wengine kufanya mambo ya mubaya.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna Yehova anatusaidiaka kama tunafanya zambi nzito.

3. Kutubu kunatusaidiaka tukuwe tena na urafiki muzuri na Yehova

Kila zambi yenye tunafanya inaumizaka Yehova. Njo maana tunapaswa kutubu kwake. Musome Zaburi 32:1-5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini hatupaswe kuficha zambi zetu, lakini tunapaswa kutubu zambi zetu kwa Yehova?

Kisha kutubu zambi zetu kwa Yehova, tutajisikia muzuri zaidi kama tunaomba wazee watusaidie. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

VIDEO: “Wale Wenye Yehova Anapenda Anawatia Nizamu” (3:01)

  • Vile uliona mu video, wazee walifanya nini juu ya kumusaidia Canon amurudilie Yehova?

Tunapaswa kuambia wazee mambo yote waziwazi, bila kuwaficha kitu. Wako pale juu ya kutusaidia. Musome Yakobo 5:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini ni mwepesi kwa wazee kutusaidia kama tunawaambia mambo waziwazi?

Picha: 1. Ndugu anahuzunika sana na anajikamata ku kichwa. 2. Ule ndugu anasali kwa Yehova. 3. Ule ndugu anaongea na muzee ku telefone. 4. Ule ndugu anakutana na wazee watatu. 5. Ule ndugu anafurahi juu iko sasa na zamiri safi.

Tubu zambi yako, usifiche wazee kitu, na ukubali musaada wa Yehova wenye upendo

4. Yehova anaonyesha rehema watenda-zambi

Kama mutu mwenye alifanya zambi nzito anakatala kufuata kanuni za Yehova, anaondolewa mu kutaniko, na hatutapitisha tena wakati pamoya naye. Musome 1 Wakorinto 5:6, 11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Sawa vile chachu inachachishaka donge lote, kupitisha wakati na mutenda-zambi mwenye hapendi kutubu, kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya ndugu na dada mu kutaniko?

Wazee wanaiga rehema yenye Yehova anaonyesha watenda-zambi kwa kutafuta na kusaidia wale wenye wameondolewa mu kutaniko. Wengi kati ya wenye waliondolewa mu kutaniko walifikia kumurudilia Yehova. Juu ya nini? Juu hata kama kuondolewa mu kutaniko kunaumizaka sana, kunasaidiaka mutu atambue makosa yake.​—Zaburi 141:5.

Namna Yehova anatendea watenda-zambi inaonyesha namna gani kama iko na usawaziko, rehema, na upendo?

5. Yehova anatusamehe wakati tunatubu

Yesu alitumia mufano fulani juu ya kutusaidia kuelewa namna Yehova anajisikiaka wakati mutu anatubu. Musome Luka 15:1-7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Hii habari inakufundisha nini juu ya Yehova?

Musome Ezekieli 33:11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Tunapaswa kufanya nini juu ya kuonyesha kama tumetubu kabisa?

Muchungaji iko anafunga kwa huruma kondoo mwenye ameumia.

Sawa vile muchungaji, Yehova anahangaikiaka sana kondoo wake

WATU FULANI WANASEMAKA: “Niko naogopa kuambia wazee zambi yenye nilifanya juu wasiniondoe mu kutaniko.”

  • Kama mutu iko na ile mawazo, utamuambia nini?

KWA KIFUPI

Kama tunafanya zambi nzito, lakini tunatubu kabisa na kuacha kufanya mambo ya mubaya, Yehova atatusamehe.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini tunapaswa kutubu zambi zetu kwa Yehova?

  • Tunapaswa kufanya nini juu Yehova atusamehe?

  • Kama tunafanya zambi nzito, juu ya nini tunapaswa kuomba wazee watusaidie?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Yehova alionyesha mwanaume fulani rehema yenye kuzungumuziwa mu Isaya 1:18.

Usikuwe na Mashaka Juu ya Rehema ya Yehova Hata Kidogo (5:02)

Namna gani wazee wanajikaza kusaidia wenye wamefanya zambi nzito?

“Namna ya Kuonyesha Watenda-zambi Upendo na Rehema” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 8, 2024)

Ona namna ya kuonyesha upendo na rehema watenda-zambi wenye hawatubu.

“Namna Wazee Wanaweza Kusaidia Wenye Wanaondolewa mu Kutaniko” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 8, 2024)

Mu habari “Nilipaswa Kumurudilia Yehova,” ona juu ya nini mwanaume mwenye alikuwa alishaacha kweli aliona kama Yehova alipenda amurudilie.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2012)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine