Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr25 Mwezi wa 3 uku. 1-15
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 3-9/3
  • TAREHE 10-16/3
  • TAREHE 17-23/3
  • TAREHE 24-30/3
  • TAREHE 31/3–6/4
  • TAREHE 7-13/4
  • UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 8
  • Sikiliza Hekima ya Yesu
  • cf uku. 131 fu. 7
  • “Ninamupenda Baba”
  • TAREHE 14-20/4
  • TAREHE 21-27/4
  • TAREHE 28/4–4/5
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2025
mwbr25 Mwezi wa 3 uku. 1-15

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 3-9/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 3

Onyesha Kama Unamutumainia Yehova

ijwbv habari ya 14 fu. 4-5

Mezali 3:5, 6​—“Usitegemee Uelewaji Wako Mwenyewe”

“Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote.” Tunaonyesha kama tunamutegemea Mungu wakati tunafanya mambo yenye anapenda. Tunapaswa kumutegemea Mungu kwa moyo wetu wote. Mu Biblia, mara mingi moyo inamaanishaka hali ya mutu ya ndani, kutia ndani hisia, nia, mawazo, na mutazamo wa mutu. Njo maana, kumutegemea Mungu kwa moyo wetu wote haiko tu kujisikia kuwa tunamutumainia kabisa. Ni uamuzi wenye tunafanya juu tuko hakika kama Muumbaji wetu anajua namna ya muzuri ya kuishi juu tukuwe na furaha.​—Waroma 12:1.

“Usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Tunapaswa kumutegemea Mungu juu hatukamilike na hatuwezi kutegemea mawazo yetu. Kama tunajitegemea siye benyewe ao tunategemea hisia zetu, tunaweza kukamata maamuzi yenye inaweza kuonekana kuwa ya muzuri ku mwanzo, lakini ku mwisho itakuwa na matokeo ya mubaya. (Mezali 14:12; Yeremia 17:9) Hekima ya Mungu inapita yetu. (Isaya 55:8, 9) Kama tunamuacha Yehova atuongoze, tutapata faida.​—Zaburi 1:1-3; Mezali 2:6-9; 16:20.

ijwbv habari ya 14 fu. 6-7

Mezali 3:5, 6​—“Usitegemee Uelewaji Wako Mwenyewe”

“Umutambue katika njia zako zote.” Tunapaswa kutafuta mawazo ya Mungu mu mambo yote yenye tuko nafanya na mbele ya kukamata maamuzi ya maana mu maisha yetu. Tunafanya vile kwa kusali juu ya kumuomba atuongoze, na kwa kutii mambo yenye anatuambia mu Neno yake Biblia.​—Zaburi 25:4; 2 Timoteo 3:16, 17.

“Atanyoosha mapito yako.” Mungu iko nanyoosha mapito yetu kwa kutusaidia kuishi kulingana na kanuni zake za haki. (Mezali 11:5) Ile inatusaidiaka kuepuka matatizo yenye haiko ya maana na kuwa na maisha yenye furaha.​—Zaburi 19:7, 8; Isaya 48:17, 18.

be uku. 76 fu. 5

Fanya Maendeleo

Kama mutu alishakapata magumu ya mingi mu maisha, anaweza kufikia kuwaza hivi: ‘Nilishakapata magumu ya hivi. Najua jambo ya kufanya.’ Unaona kama ni hekima kuwaza vile? Mezali 3:7 inatuambia hivi: “Usikuwe mwenye hekima mbele ya macho yako mwenyewe.” Bila shaka, uzoefu unapaswa kufungula akili yetu wakati tunapambana na magumu mu maisha. Na kama tunafanya maendeleo ya kiroho, uzoefu unapaswa kusaidia akili yetu na moyo wetu kuelewa kama tuko na lazima ya baraka ya Yehova juu tufanikiwe. Tunaonyesha kama tuko nafanya maendeleo kwa kumuomba Yehova atuongoze mu maisha kuliko kujitegemea siye benyewe wakati tuko napambana na magumu. Tunaonyesha pia maendeleo yetu kwa kuwa hakika kama hakuna jambo yenye inaweza kutokea kama Yehova hairuhusu, na kwa kufanya uhusiano wetu wenye upendo pamoya na Baba yetu wa mbinguni ukuwe nguvu.

Mali ya Kiroho

w06 15/9 uku. 17 fu. 7

Mambo Makubwa ya mu Kitabu ya Mezali

3:3. Tunapaswa kuona upendo mushikamanifu na uaminifu kuwa bya maana sana na kubionyesha waziwazi sawa shenete ya mu shingo ya bei sana. Na tunapaswa kubiandika mu moyo wetu, kwa kufanya bikuwe sehemu ya maana ya maisha yetu.

Hotuba: Umutumainie Mungu Wakati Batu Habafurahie Ujumbe Wetu

w11 15/3 uku. 14 fu. 7-10

Mtegemee Yehova Kadiri Mwisho Unavyokaribia

7 Ndugu zetu wengi wanatumika katika maeneo ambako ni vigumu sana kuvumilia. Nabii Yeremia alitumikia katika mazingira kama hayo, wakati ufalme wa Yuda ulipokuwa katika siku zake za mwisho zenye misukosuko. Kila siku imani yake ilijaribiwa kwa sababu alitangaza kwa utii ujumbe mbalimbali wa hukumu ya Mungu. Pindi fulani, hata mwandishi wake mshikamanifu, Baruku, alilalamika kwamba amechoka. (Yer. 45:2, 3) Je, Yeremia alivunjika moyo? Mara kwa mara, alishuka moyo. Alisema hivi: “Na ilaaniwe ile siku nilipozaliwa! Kwa nini nimetoka ndani ya tumbo la uzazi ili kuona kazi ngumu na huzuni na ili siku zangu zifikie mwisho wake katika aibu tupu?”​—Yer. 20:14, 15, 18.

8 Hata hivyo, Yeremia hakukata tamaa. Aliendelea kumtegemea Yehova. Kwa hiyo, nabii huyo mwaminifu aliona utimizo wa maneno haya ya Yehova kwenye Yeremia 17:7, 8: “Amebarikiwa yule mtu hodari anayemtegemea Yehova, na ambaye Yehova amekuwa uhakika wake. Na hakika yeye atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, unaopeleka mizizi yake kando ya mto; naye hataona joto linapoingia, bali kwa kweli majani yake yatakuwa mengi. Na katika mwaka wa ukame hatahangaika, wala hataacha kuzaa matunda.”

9 Kama mti wa matunda wenye majani mengi “uliopandwa kando ya maji” au shamba la miti ya matunda linalomwagiliwa maji, Yeremia ‘hakuacha kamwe kuzaa matunda.’ Alikataa kushawishiwa na wadhihaki waovu waliomzunguka. Badala yake, alishikamana na yule aliye Chanzo cha “maji” yanayoendeleza uhai na akatii kila jambo ambalo Yehova alimwambia. (Soma Zaburi 1:1-3; Yer. 20:9) Yeremia ni kielelezo kizuri kwetu kama nini, hasa kwa wale ambao wanamtumikia Mungu katika maeneo magumu! Ikiwa unakabili hali kama hiyo, endelea kumtegemea sana Yehova, ambaye atakupatia uvumilivu unapoendelea ‘kulifanyia jina lake tangazo la hadharani.’​—Ebr. 13:15.

10 Kwa kweli, Yehova ametupatia vitu vingi vya kiroho ili kutusaidia kupambana na maisha katika siku hizi za mwisho. Kwa mfano, ameandaa Neno la Mungu lililo kamili, ambalo linatafsiriwa kwa usahihi katika lugha nyingi zaidi. Ameandaa chakula kingi cha kiroho kwa wakati unaofaa kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Na ametupatia ushirika wa umati mkubwa wa waamini wenzetu kwenye mikutano na makusanyiko ambao wanatutegemeza. Je, unatumia kikamili maandalizi hayo? Wote wanaofanya hivyo “watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo.” Hata hivyo, wale ambao hawamsikilizi Mungu, ‘watalia kwa sababu ya maumivu ya moyo na watapiga mayowe kwa sababu ya mvunjiko kabisa wa roho.’​—Isa. 65:13, 14.

TAREHE 10-16/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 4

“Linda Moyo Wako”

w19.01 uku. 15 fu. 4

Unaweza Kufanya Nini ili Kulinda Moyo Wako?

4 Mu Mezali 4:23, neno “moyo” linatumiwa ili kumaanisha “mutu wa ndani” ao “mutu mwenye kuwa katika siri.” (Soma Zaburi 51:6 na maelezo ya chini.) Katika maneno ingine, neno “moyo” maana yake, mawazo yetu ya siri, namna tunajisikia, nia zetu, na tamaa zetu. Ni namna tuko kabisa ndani yetu, haiko tu namna tunaonekana kwa inje.

w19.01 uku. 17 fu. 10-11

Unaweza Kufanya Nini ili Kulinda Moyo Wako?

10 Ili tuweze kulinda moyo wetu, tunapaswa kuwa na uwezo wa kutambua hatari na kutenda haraka ili kujilinda. Neno lenye kutafsiriwa “linda” mu Mezali 4:23, linatukumbusha kazi ya mulinzi. Mu siku za Mufalme Sulemani, walinzi walikuwa wanasimama kwenye ukuta wa muji ili kulinda muji na wangetumia chombo fulani ili kutoa mulio ikiwa wangeona hatari inakaribia. Kuona picha ya jambo hilo mu akili yetu kunatusaidia kuelewa mambo yenye tunapaswa kufanya ili kumuzuia Shetani asipotoshe mawazo yetu.

11 Wakati wa zamani, walinzi walitumika pamoja na walinzi wa milango mikubwa ya muji. (2 Sa. 18:24-26) Walitumika pamoja ili kusaidia kulinda muji kwa kuhakikisha kama milango mikubwa ilifungwa kila mara wakati adui alikaribia. (Ne. 7:1-3) Zamiri yetu yenye kuzoezwa na Biblia inaweza kutenda kama mulinzi wetu na kutuonya wakati Shetani anajaribu kushambulia moyo wetu, ni kusema, wakati anajaribu kuchochea mawazo yetu, namna yetu ya kujisikia, nia zetu, na tamaa zetu. Kila wakati zamiri yetu inatoa sauti ya kutuonya tunapaswa kuisikiliza na kufunga mulango, ni kusema, kufanya nguvu yetu yote ili kuepuka hatari.

w19.01 uku. 18 fu. 14

Unaweza Kufanya Nini ili Kulinda Moyo Wako?

14 Ili kulinda moyo wetu, tunapaswa kuufunga ili mambo ya mubaya isiingie ndani, lakini pia tunapaswa kuufungua ili mambo ya muzuri iingie ndani. Fikiria tena mufano wa muji wenye kuzungukwa na ukuta. Mulinzi wa mulango mukubwa alikuwa anafunga milango mikubwa ya muji ili kuzuia adui asiingie ndani, lakini wakati mwingine alikuwa anafungua milango mikubwa ili kuruhusu chakula na mambo ingine ya lazima viingizwe ndani ya muji. Kama milango mikubwa haingefunguliwa hata siku moja, wakaaji wa muji wangekufa na njaa. Vilevile tunapaswa kufungua moyo wetu kwa ukawaida ili mawazo ya Mungu iingie ndani.

w12 1/5 uku. 32 fu. 2

“Linda Moyo Wako!”

Kwa nini tunapaswa kulinda moyo wetu wa mfano? Mungu alimwongoza Mfalme Sulemani kuandika maneno haya: “Linda moyo wako kuliko vitu vingine vyote vinavyopaswa kulindwa, kwa maana ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.” (Methali 4:23) Hali ya moyo wetu wa mfano ndiyo inayoamua ikiwa tutakuwa na maisha bora sasa na tumaini letu la kupata uzima wa milele wakati ujao. Kwa nini? Kwa sababu Mungu anaona yale yaliyo ndani ya mioyo yetu. (1 Samweli 16:7) Kwa hiyo, maoni ya Mungu kutuelekea yanategemea jinsi tulivyo kwa ndani, yaani, sisi ni watu wa aina gani katika “mtu wa siri wa moyoni.”​—1 Petro 3:4.

Mali ya Kiroho

w21.08 uku. 8 fu. 4

Uko Tayari Kumungojea Yehova?

4 Mezali 4:18 inatuambia kama “njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubui wenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.” Hii maneno inaonyesha waziwazi kama Yehova anasaidia watu wake waelewe kusudi yake hatua kwa hatua. Lakini, ile andiko inatusaidia pia kuelewa namna Mukristo anafanya mabadiliko mu maisha yake na namna anamukaribia Yehova zaidi. Inaomba wakati juu mutu afikie kumukaribia Yehova zaidi. Kama tunajifunza kwa uangalifu na kutumikisha mashauri yenye tunapata kupitia Neno ya Mungu na tengenezo yake, tutaendelea hatua kwa hatua kuwa na sifa sawa za Kristo. Tena tutamujua Mungu muzuri zaidi. Ona namna Yesu alizungumuzia ile jambo.

Onyesho: Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Habafanyake Fete ya Pasaka

ijwfq habari ya 19

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka

Mawazo ya watu wengi

▪ Uongo: Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka juu hawako Wakristo.

Ukweli: Tunaamini kama Yesu Kristo ni Mukombozi wetu, na tunafanya yetu yote ili ‘kufuata hatua zake kwa ukaribu.’​—1 Petro 2:21; Luka 2:11.

▪ Uongo: Hamuamini kama Yesu alifufuliwa.

Ukweli: Tunaamini kama Yesu alifufuliwa; tunajua kama ile njo musingi wa imani ya Kikristo na tunaikaziaka sana wakati tuko nahubiri.​—1 Wakorinto 15:3, 4, 12-15.

▪ Uongo: Hamuhangaikie kuona watoto wenu wanakosa ile furaha ya sherehe ya Pasaka.

Ukweli: Tunapenda watoto wetu, na tunatumia wakati mingi juu ya kuwazoeza na kuwasaidia wakuwe na furaha.​—Tito 2:4.

Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka?

▪ Sherehe ya Pasaka haitegemee Biblia.

▪ Yesu alitupatia amri ya kukumbuka kifo yake, hapana ufufuo wake. Tunafanyaka ile ukumbusho kila mwaka mu tarehe ya kifo yake kulingana na kalendari ya miezi ya Biblia .​—Luka 22:19, 20.

▪ Tunaamini kama mambo yenye watu wanafanyaka wakati wa kusherehekea Pasaka, inatokana na desturi zenye watu walikuwa wanafuata zamani juu wapate nguvu ya uzazi; kwa hiyo Mungu hapende watu wake wakuwe wanasherehekea Pasaka. Anapenda watu “washikamane na yeye tu,” na anachukia ibada yenye iko amo matendo yenye haimupendeze.​—Kutoka 20:5; 1 Wafalme 18:21.

Tunaamini kama uamuzi wetu wa kukatala kusherehekea Pasaka unategemea kabisa Biblia, yenye inatutia moyo tukuwe na “hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri” kuliko tu kufuata desturi za wanadamu. (Mezali 3:21; Matayo 15:3) Hata kama tunaambiaka watu wengine kuhusu imani yetu juu ya Pasaka, kama wanatuuliza, tunaheshimiaka haki ya kila mutu ya kujiamulia ikiwa ataisherehekea ao hapana.​—1 Petro 3:15.

TAREHE 17-23/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 5

Kimbia Busharati

w00 15/7 uku. 29 fu. 2

Unaweza Kuendelea Kuwa na Mwenendo Safi mu Dunia Yenye Kupotoka

Mu hii mezali, mutu mwenye kupotoka anafananishwa na “mwanamuke mugeni”​—kahaba. Maneno yenye anatumikishaka juu ya kutongozana iko butamu sawa asali na maneno yake iko laini sawa mafuta. Haiko vile njo batu banazoeaka kutongozana? Kwa mufano, fikiria mambo yenye ilimufikiaka sekretere moya mwanamuke mwenye kupendeza wa miaka 27 mwenye kuitwa Amy. Anasema hivi: “Mwanaume moya hivi mwenye tunatumikaka naye ananihangaikiaka sana na anakuwaka nanisifu kila wakati. Kila mutu anajisikiaka tu muzuri kama banamuhangaikia. Lakini namna ananihangaikiaka inaonekanaka tu wazi kama anapendaka njo kulala na miye.” Maneno ya mwenye kutongoza inakuwaka tu ya butamu akose tu kama unajua nia yake. Njo maana tunapaswa kuzoeza uwezo wetu wa kufikiri.

w00 15/7 uku. 29 fu. 3

Unaweza Kuendelea Kuwa na Mwenendo Safi mu Dunia Yenye Kupotoka

Matokeo ya busharati inakuwaka buchungu sawa pakanga na inakuwaka makali sawa upanga yenye makali ngambo na ngambo. Inaweza kuleta maumivu na hata kifo. Mara mingi ile tabia inafanyaka mutu akuwe na zamiri ya mubaya, apate mimba yenye hakutazamia, ao magonjwa yenye inaambukizwaka kupitia ngono. Zaidi ya ile, kuishi na bibi ao bwana mwenye haiko muaminifu inaletaka uchungu sana. Tendo moya tu ya kukosa uaminifu inaweza kuleta huzuni mu maisha yote. Kusema kweli, busharati bunaletaka matokeo ya mubaya sana.

w00 15/7 uku. 29 fu. 6

Unaweza Kuendelea Kuwa na Mwenendo Safi mu Dunia Yenye Kupotoka

Tunapaswa pia kuwa mbali na batu benye banaweza kutufanya tuangukie mu busharati. Ni hatari sana kujiingiza mu manjia yabo kwa kusikiliza miziki yenye kukosa adabu, kuangalia mambo yenye haiko sawa, ao kuangalia pornografia. (Mezali 6:27; 1 Wakorinto 15:33; Waefeso 5:3-5) Na ni upumbavu sana kama tunaanza kubavutia kupitia mwenendo wetu ao namna yetu ya kuvala na kujipamba​—1 Timoteo 4:8; 1 Petro 3:3, 4.

Mali ya Kiroho

w11 1/2 uku. 20 fu. 2

Ufundishe Batoto Yako Mwenendo Muzuri

Biblia inaweza kutusaidia, juu iko na amri zenye kuwa na maneno yenye inaonyesha waziwazi matokeo ya kufanya mambo ya mubaya. Kwa mufano, andiko ya Mezali 5:8, 9 inaagiza kijana aepuke busharati ‘juu asipatie bengine heshima yake.’ Vile tu ile andiko inaonyesha, mutu mwenye anafanya ngono mbele ya kuoa ao kuolewa anajiharibishia sifa, anaharibu burafiki yake pamoya na Yehova, na anapoteza heshima yake. Na ile inaweza kukimbiza mutu mwenye angependa kumuoa ao kuolewa naye. Kufikiria hii matokeo ya kimwili, kiakili, na kiroho juu tu ya kutokutii sheria za Mungu kunaweza kumusaidia mutoto wako kijana akimbie busharati.

TAREHE 24-30/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 6

Siafu Inaweza Kutufundisha Nini?

it-1 uku. 927 fu. 10-uku. 928 fu. 1

Siafu

‘Hekima.’ ‘Hekima ya siafu haitokane na akili ya batu, lakini inatokana njo na akili yenye Muumbaji alizipatia. Wakati Biblia inazungumuzia siafu, inasema kama siafu inakuwaka ‘natayarisha chakula yake wakati wa kipindi ya joto, na kukusanya chakula yake wakati wa mavuno.’ (Mez 6:8) Aina moya ya siafu yenye kujulikana sana mu Palestine ni siafu yenye inavunaka ao siafu ya mu mashamba (Messor semirufus). Inakuwaka naweka chakula ya mingi mu madepo wakati hakuna joto ao baridi, na pia wakati wa joto sana. Na itakula ile chakula mu baridi ya nguvu wakati inakuwa nguvu kupata chakula. Mara mingi hii aina ya siafu inapatikanaka karibu ya biwanja bya kupigia-pigia nafaka, kwenye mbegu inakuwaka mingi sana. Kama mvula inalobanisha ile mambegu, siafu ya mu mashamba itaitosha inje juu ikauke na jua. Na tena inajulikana kama siafu inatoshaka mu mbegu kitu yenye inaisaidiaka kuota juu isiote mu depo mwenye iliiweka. Bikundi bya siafu ya mu mashamba binajulikanaka kupitia alama yenye binaachaka na kupitia maganda ya mbegu yenye binaachaka fasi kwenye binaingiliaka.

Mambo Yenye Tunaweza Kuiga. Batu fulani benye balichunguza siafu kwa kifupi banahakikisha hii maneno: “Uende kwa siafu, wewe muvivu; chunguza njia zake na ukuwe na hekima.” (Mez 6:6) Ni kweli kama siafu inajulikana juu ya namna inajitayarishaka kwa ajili ya wakati wenye kuya, lakini inajulikana pia juu ya namna inatumikaka kwa bidii. Mara mingi siafu inaweza kubeba kitu yenye iko na buzito ya kuipita mara mbili ao hata zaidi. Siafu inafanyaka yake yote juu itimize kazi yenye inapaswa kufanya, na haivunjikake moyo hata kama inatereza ao kuanguka. Siafu inatumikaka kwa umoja, inasafishaka fasi kwenye inakuwaka naishi, na inahangaikianaka sana na hata kusaidia siafu yenye inaumia ao yenye inachoka juu irudie fasi kwenye inakuwaka naishi.

w00 15/9 uku. 26 fu. 3-4

Linda Jina Yako

Hauone kama na siye tunapaswa kutumika kwa bidii kama siafu? Ni muzuri tujikaze kutumika kwa bidii na kufanya kazi muzuri zaidi, ikuwe kuko mutu iko natuona ao hapana. Ikuwe ku masomo, ku kazi ao wakati tuko nafanya mambo mbalimbali ya kiroho, tunapaswa kutumika kwa uwezo wetu wote. Vile tu siafu inafaidikaka na kazi ya bidii yenye inafanyaka, njo vile Mungu anapendaka na siye ‘tufurahie kazi yetu yote ya nguvu.’ (Muhubiri 3:13, 22; 5:18) Kuwa na zamiri ya muzuri na kutosheka njo faida yenye tunapataka wakati tunatumika kwa bidii.​—Muhubiri 5:12.

Sulemani anatumia maulizo mbili yenye inaweza kusaidia mutu aache buvivu. Anauliza hivi: “Wewe muvivu, utaendelea kulala pale mupaka wakati gani?Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?” Kisha anasema mambo yenye muvivu anafanyaka: “Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kukunja mikono kidogo ili kupumuzika, na umaskini wako utakuja kama munyanganyi, na uhitaji wako kama mwanaume mwenye silaha.” (Mezali 6:9-11) Wakati muvivu iko nalala, bumaskini bunamufikiaka tu kwa urahisi sawa munyanganyi, na uhitaji unamushambuliaka sawa mutu mwenye iko na silaha. Shamba ya muvivu haikawiake kuyala mayani ya mubaya na bilulu. (Mezali 24:30, 31) Hakawiake kupoteza mu biashara yake. Mutu wa vile hata mu kazi hawezi kukawia. Na kama ni mwanafunzi hawezi kupata matokeo ya muzuri ku masomo.

Mali ya Kiroho

w00 15/9 uku. 27 fu. 3

Linda Jina Yako

Makosa saba yenye mezali inazungumuzia inahusu aina yote ya mambo ya mubaya. “Macho yenye majivuno” na “moyo wenye kufanya mipango ya uovu,” ni zambi zenye mutu anafanya mu mawazo yake. “Ulimi wa uongo” na “shahidi wa uongo mwenye kusema uongo kila wakati anapumua,” ni zambi zenye mutu anafanya mu maneno. “Mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa” na “miguu yenye kukimbilia haraka kwenye uovu,” ni matendo ya mubaya. Na kitu yenye Yehova anachukiaka sana ni mutu mwenye anafurahiaka tu kuachanisha batu benye bangeishi pamoya kwa amani. Namna hesabu inaongezeka kutoka ku sita kuenda ku saba inaonyesha kama hii liste haitaye bitu byote byenye Mungu anachukiaka, juu bubaya bwa batu bunaongezekaka tu.

TAREHE 31/3–6/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 7

Epuka Kuangukia mu Mutego

w00 15/11 uku. 29 fu. 5

‘Ushike Amri Zangu Juu Uendelee Kuishi’

Dirisha kwenye Sulemani iko naangalilia inje iko na byuma byenye binaingiana-ingiana. Mu barabara munakuwa giza wakati busiku inaanza kuingia. Anaona kijana moya mwenye iko najiingiza mu hatari. Ule kijana anakosa utambuzi. Inawezekana kama anajua hali ya eneo yenye iko natembelea na mambo yenye inaweza kumufikia. Ule kijana mwanaume anafika karibu na nyumba ya mwanamuke moya hivi. Ule mwanamuke ni nani? Na anapenda kufanya nini?

w00 15/11 uku. 30 fu. 3-5

‘Ushike Amri Zangu Juu Uendelee Kuishi’

Midomo ya ule mwanamuke iko laini. Kwa ujasiri, anaanza kusema maneno yake bila mashaka. Byote byenye iko nasema ni juu tu ya kumushawishi ule kijana mwanaume. Juu ya kujionyesha kama iko mutu muzuri na kama anamupenda Mungu, anamuambia ule kijana kama alishatoa zabihu za ushirika na alishatimiza naziri zake. Zamani, zabihu zenye batu balikuwaka natoa ku hekalu Yerusalemu zilikuwaka njo nyama, bunga, mafuta, na divai. (Mambo ya Walawi 19:5, 6; 22:21; Hesabu 15:8-10) Juu mwenye anatoa ile zabihu alikuwaka nabeba sehemu fulani ya byenye anatoa kwa ajili yake na familia yake. Njo maana, wakati ule mwanamuke anamuambia ule kijana kama alitoa zabihu za ushirika, anapenda kusema kama kwake kuko chakula mingi na divai. Anapenda tu kumuonyesha kama atafurahia kupitisha wakati pamoya naye. Anasema kama alitoka inje ya nyumba yake juu tu ya kukutana naye. Ile inaweza kugusa sana moyo wa mutu mwenye anaaminia maneno ya vile. Mutu fulani mwenye kujifunza mambo ya Biblia anasema kama “ni kweli ule mwanamuke alitoka inje ya nyumba yake juu alikuwa natafuta mutu fulani. Lakini kweli alikuwa natafuta njo ule kijana mwanaume? Ni mupumbavu tu sawa ule kijana njo anaweza kumuaminia.”

Ule mwanamuke amechochea macho ya ule kijana kupitia namna yake ya kujipamba, amechochea masikio yake kupitia maneno yenye kushawishi, amemugusa kwa kumukumbatia, na amemufanya asikie butamu ya midomo yake kwa kumubusu. Sasa anapenda kuchochea pua yake kwa kusema hivi: “Nimetandika matandiko ya muzuri kwenye kitanda changu, kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali. Nimenyunyiza manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.” (Mezali 7:16, 17) Ametandika muzuri kitanda yake kwa kutumia nguo fulani ya Misri yenye kuwa na rangi mbalimbali na amemwanga marashi ya manemane, udi, na mudalasini.

Anasema tena hivi: “Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui,” kisha anaongezea hivi: “tujifurahishe pamoja kwa mapendo.” Hamualike tu juu ya kukula pamoya. Anamuahidi kama batafurahia kufanya ngono. Bila shaka, ile wazo ilimufurahisha ule kijana! Juu ule kijana asikuwe na wasiwasi, ule mwanamuke anamuambia tena hivi: “Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;ameenda safari ya mbali. Alibeba mufuko wa feza, na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.” (Mezali 7:18-20) Anamuhakikishia kama hakutakuwa shida, juu bwana yake alienda mu safari na atafanya masiku fulani kule. Ule mwanamuke anajua kabisa kushawishi mutu! “Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.” (Mezali 7:21) Inaomba kuwa nguvu kiroho sawa Yosefu juu ya kupinga ile kishawishi. (Mwanzo 39:9, 12) Sasa huyu kijana ataweza?

w00 15/11 uku. 31 fu. 1

‘Ushike Amri Zangu Juu Uendelee Kuishi’

Ule kijana hakuweza kukatala ile kishawishi. Bila kufikiri muzuri, anamufuata ule mwanamuke ‘kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa.’ Vile tu mutu mwenye kufungwa hawezi kukimbia malipizi yake, njo vile ule kijana anaangukia mu zambi. Anashindwa kuona hatari mupaka wakati ‘mushale unatobola maini yake,’ ni kusema, mupaka wakati anapata kilonda yenye inaweza kumufikisha ku kifo. Inaweza kuwa kifo tu ya kwelikweli juu pengine aliambukizwa magonjwa yenye inaambukizwaka kupitia ngono. Inaweza pia kuwa kilonda yenye inaweza kumufikisha ku kifo ya kiroho. “Uzima wake” uko mu hatari kabisa na amemukosea Mungu sana. Anajipeleka mbio mu kifo sawa ndege mwenye anaingia mu mutego!

Mali ya Kiroho

w00 15/11 uku. 29 fu. 1

‘Ushike Amri Zangu Juu Uendelee Kuishi’

Sulemani anaendelea kusema hivi: ‘Uzifunge [amri za Mungu] kuzunguka vidole vyako; uziandike kwenye kibao cha moyo wako.’ (Mezali 7:3) Vile tu tunaonaka bidole yetu saa yote na binatusaidiaka kutimiza kazi mbalimbali za maana mu maisha, njo vile tunapaswa kukumbuka mambo yenye tunajifunza mu Biblia na kuiacha ituongoze mu kila kitu yenye tunafanya mu maisha yetu. Tunapaswa kuiandika ku kibao ya moyo wetu, ni kusema kuifanya ikuwe sehemu ya maisha yetu.

TAREHE 7-13/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 8

Sikiliza Hekima ya Yesu

cf uku. 131 fu. 7

“Ninamupenda Baba”

7 Mu mustari wa 22, hekima inasema hivi: “Yehova aliniumba nikiwa mwanzo wa njia yake, mwanzo kabisa wa kazi zake za zamani sana.” Haiko hekima njo inazungumuziwa hapa, juu hekima ni sifa yenye ‘haikuumbwa’. Hekima haikuwake na mwanzo juu Yehova naye hakuwake na mwanzo na anakuwaka tu mwenye hekima. (Zaburi 90:2 ) Lakini, Mwana wa Mungu iko “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” Aliumbwa; yeye njo kiumbe wa kwanza mwenye Yehova aliumba. (Wakolosai 1:15) Kulingana na Mezali, Mwana alikuwa hata mbele ya dunia na mbingu kuumbwa. Na tena, juu yeye ni Neno, Musemaji wa Mungu, alikuwa mufano wa kweli kabisa wa hekima ya Yehova.​—Yohana 1:1.

cf uku. 131-132 fu. 8-9

“Ninamupenda Baba”

8 Mwana alikuwa na kazi gani mu ile wakati ya murefu mbele ya kuya ku dunia? Mustari wa 30 unatuambia kama alikuwa karibu na Mungu akiwa “fundi wa kazi.” Ile inamaanisha nini? Wakolosai 1:16 inafasiria hivi: “Kupitia yeye vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani . . . Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye na kwa ajili yake.” Ile inamaanisha kama Yehova Muumbaji alitumika pamoya na Mwana wake, mwenye ni Fundi wa Kazi, juu ya kuumba bitu byote​—kuanzia biumbe bya kiroho ku mbingu mupaka ulimwengu na bitu byenye biko ndani, sawa vile miti, banyama na kiumbe wa kushangaza zaidi: mwanadamu. Mu mambo fulani, uhusiano wa Baba na Mwana uko sawa vile uhusiano kati ya mujenzi na musaidizi wake. Musaidizi anafuataka mawazo ya mujenzi juu ya kutimiza kazi. Ni kweli kama wakati kitu fulani ya uumbaji inatushangaza, tunamupatiaka njo Muumbaji mukubwa utukufu. (Zb 19:1) Lakini tunaweza pia kukumbuka namna muumbaji na “fundi [wake] wa kazi” balifurahia kutumika pamoya kwa miaka mingi.

9 Wakati batu bawili benye habakamilike biko natumika pamoya, kunakuwaka tu kukosana. Lakini haiko vile kwa Yehova na Mutoto wake! Mwana alitumika kwa miaka mingi sana pamoya na Baba yake na anasema hata hivi: “Nilifurahi mbele yake wakati wote.” (Mezali 8:30) Ni kweli kama alifurahia kutumika pamoya na Baba yake, na Baba yake naye alifurahia pia. Vile Yesu alikuwa naiga sifa za Baba yake, ni vile pia alimufanana. Njo maana haishangaze kuona kama uhusiano kati ya Baba na Mwana ulifikia kuwa nguvu sana! Ile njo uhusiano ya upendo ya zamani sana na ya nguvu sana mu ulimwengu.

w09 15/4 uku. 31 fu. 14

Kutambua Daraka ya Yesu Akiwa Daudi Mukubwa Zaidi na Sulemani Mukubwa Zaidi

14 Ni mutu moya tu njo alikuwa na hekima kupita Sulemani. Ule mutu ni Yesu Kristo, mwenye alijitambulisha mwenyewe kuwa “kitu kikubwa kuliko Sulemani.” (Mt. 12:42) Yesu alikuwa nasema “maneno ya uzima wa milele.” (Yohana 6:68) Kwa mufano, mu Mahubiri ya ku Mulima, Yesu alifasiria makanuni fulani yenye Sulemani aliandika mu kitabu ya Mezali. Sulemani alitaya mambo fulani yenye inaleteaka muabudu wa Yehova furaha. (Mez. 3:13; 8:32, 33; 14:21; 16:20) Yesu alikazia kama kumuabudu Yehova na kuamini kama ahadi zake zitatimia njo jambo yenye inaleteaka mutu furaha ya kweli. Alisema: “Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho, kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wao.” (Mt. 5:3) Bale benye kutumikisha makanuni yenye kuwa mu mafundisho ya Yesu biko namukaribia sana Yehova, mwenye ni, “chemchemi ya uzima.” (Zb. 36:9; Mez. 22:11; Mt. 5:8) Kristo anafananisha “hekima ya Mungu.” (1 Ko. 1:24, 30) Juu yeye njo Mufalme mwenye alichaguliwa na Mungu, Yesu Kristo iko na “hekima ya Mungu.”​—Isa. 11:2.

Mali ya Kiroho

g 5/14 uku. 16

‘Hekima Inapaaza Sauti’ Unaweza Kuisikia?

▪ Kitabu kimoja kinasema hivi: Biblia ni “kitabu chenye kimegawanywa sana katika historia. Kimetafsiriwa mara nyingi na katika luga nyingi kuliko kitabu kingine chochote.” (The World Book Encyclopedia) Biblia inapatikana sasa katika luga karibu 2600, ikiwa nzima ao kwa sehemu, na hilo linafanya watu zaidi ya 90 juu ya 100 katika dunia waipate.

▪ Hekima ‘inaendelea kulia kwa sauti kubwa’ kwa njia ya kwelikweli. Katika andiko la Mathayo 24:14, tunasoma hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho [wa ulimwengu huu] utakapokuja.”

Hotuba: Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

ijwbq habari ya 160

Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Jibu ya Biblia

Mara mingi Biblia inaita Yesu “Mwana wa Mungu.” (Yohana 1:49) Maneno “Mwana wa Mungu” inaonyesha kama Mungu njo aliumba vitu vyote vyenye uzima, na hata Yesu. (Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11) Biblia haifundishe kama Mungu alizalaka Yesu sawa vile baba wanadamu wanazalaka watoto.

Biblia inaita malaika pia kuwa “wana wa Mungu wa kweli.” (Yobu 1:6) Na Biblia inasema kama mwanadamu wa kwanza, ni kusema, Adamu, alikuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Biblia inaita Yesu Mwana wa pekee wa Mungu juu yeye njo Mungu aliumbaka mbele aumbe vitu vingine vyote, na yeye tu njo Mungu aliumbaka moja kwa moja.

Yesu aliishi mbinguni mbele azaliwe ku dunia?

Ndiyo. Yesu alikuwa kiumbe wa roho mbinguni mbele azaliwe hapa ku dunia. Yesu yeye peke alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni.”​—Yohana 6:38; 8:23.

Mungu aliumba Yesu mbele aumbe kitu ingine yoyote. Biblia inasema hivi juu ya Yesu:

▪ “Yeye ni . . . muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.”​—Wakolosai 1:15.

▪ Yeye ni “mwanzo wa uumbaji wa Mungu.”​—Ufunuo 3:14.

Yesu alitimiza unabii wenye kuzungumuzia ule mwenye “asili yake ni ya kuanzia nyakati za zamani, kuanzia siku za zamani sana.”​—Mika 5:2; Matayo 2:4-6.

Yesu alikuwa nafanya nini mbele akuye ku dunia?

Alikuwa na cheo ya juu mbinguni. Yesu alizungumuzia cheo yenye alikuwa nayo wakati alisali hivi: “Baba, unitukuze . . . kwa utukufu wenye nilikuwa nao pembeni yako mbele ya ulimwengu kuwa.”​—Yohana 17:5.

Alisaidia Baba yake kuumba vitu vingine vyote. Yesu alitumika na Mungu ‘akiwa fundi wa kazi.’ (Mezali 8:30) Biblia inasema hivi juu ya Yesu: “Kupitia yeye vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani.”​—Wakolosai 1:16.

Mungu alimutumia Yesu juu ya kuumba vitu vingine vyote. Kwa mufano, alimutumia juu ya kuumba viumbe vya roho, na ulimwengu. (Ufunuo 5:11) Tunaweza kusema kama Mungu alitumika pamoya na Yesu sawa vile mutu mwenye kufanya plani ya majengo anatumikaka na mujenzi. Mutu mwenye kufanya plani, analetaka plani, kisha mujenzi anaitumia juu ya kujenga.

Alikuwa Neno. Wakati Biblia inazungumuzia maisha ya Yesu mbele akuwe mwanadamu, inamuita “Neno.” (Yohana 1:1) Ni kusema, Mungu alikuwa namutumia juu ya kujulisha viumbe vingine vya roho habari fulani na maagizo yake.

Inaonekana pia kama Mungu alikuwa natumia Yesu juu ya kujulisha wanadamu ku dunia habari fulani na maagizo yake. Inawezekana Mungu alimutumia Yesu juu ya kujulisha Adamu na Eva maagizo yake mu bustani ya Edeni. (Mwanzo 2:16, 17) Inawezekana Yesu njo ule malaika mwenye aliongozaka Waisraeli wa zamani mu jangwa na mwenye Waisraeli walipaswa kutii kabisa.​—Kutoka 23:20-23.

TAREHE 14-20/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 9

Ukuwe Mutu Mwenye Hekima, Hapana Mwenye Zihaka

w22.02 uku. 9 fu. 4

“Usikilize Maneno ya Wenye Hekima”

4 Kusema kweli, inaweza kuwa nguvu kwetu kukubali shauri ya moja kwa moja. Tunaweza hata kukwazika. Juu ya nini? Hata kama tunajua kama hatukamilike, inaweza kuwa nguvu kwetu kukubali shauri wakati mutu fulani anatuambia kuhusu kosa fulani yenye tulifanya. (Soma Muhubiri 7:9.) Pengine tunaweza kutoa visababu. Pengine tunaweza kujiuliza nini njo ilimuchochea akuye kutushauria ao tunaweza kukasirika juu ya namna alitutolea shauri. Na pengine tunaweza hata kutafuta makosa kwa ule mwenye alitushauria na kusema hivi: ‘Alijiona mbele ya kuya kunishauria? Naye anafanyaka makosa!’ Na kama hatupende shauri yenye wanatutolea pengine tunaweza tu kuipuuza ao kuomba mutu mwingine atupatie shauri juu tunatumainia kama yeye njo atatuambia mambo yenye tunapenda kusikia.

w22.02 uku. 12 fu. 12-14

“Usikilize Maneno ya Wenye Hekima”

12 Ni mambo gani inaweza kutusaidia kukubali shauri? Ni muzuri kuwa wanyenyekevu na kukumbuka kama hatukamilike na wakati fulani tunaweza kutenda mubaya. Sawa vile tumesha zungumuzia, Yobu alikuwa na mawazo ya mubaya lakini alibadilisha mawazo yake na Yehova alimubariki. Juu ya nini? Juu Yobu alikuwa munyenyekevu. Alionyesha unyenyekevu wake kwa kukubali shauri yenye Elihu alimupatia, hata kama Elihu alikuwa mudogo sana kuliko yeye. (Yob. 32:6, 7) Unyenyekevu utatusaidia pia kutumikisha shauri hata kama tunaona kuwa hatustahili kuipewa ao mwenye anatutolea ile shauri ni mudogo sana kuliko siye. Muzee moya wa Kanada anasema hivi: “Vile hatuwezi kujiona sawa vile wengine wanatuonaka namna gani tunaweza kufanya maendeleo kama hakuna mutu wa kutushauria?” Siye wote tuko na lazima ya kukomalisha tunda ya roho na kufikia kuwa muhubiri na mwalimu muzuri zaidi wa habari njema​—Soma Zaburi 141:5.

13 Uone shauri kuwa njia ya Mungu ya kutuonyesha upendo. Yehova anatutakia mambo ya muzuri zaidi. (Mez. 4:20-22) Wakati anatushauria kupitia Neno yake, kichapo fulani yenye inategemea Biblia, ao kupitia muamini fulani mukomavu, ni njia ya kutuonyesha upendo. Waebrania 12:9, 10 inasema: “Yeye anafanya vile kwa faida yetu.”

14 Ukazie akili shauri, hapana namna ilitolewa. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama, hawakututolea shauri mu njia ya muzuri zaidi. Kusema kweli, kila mutu mwenye anatoa shauri anapaswa kujikaza kufanya ile shauri ikuwe mwepesi kadiri inawezekana juu ikubaliwe. (Gal. 6:1) Lakini kama ni siye njo wanatushauria tunapaswa kufikiria mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia ile shauri hata kama tunawaza kuwa mutu mwenye alitutolea ile shauri angepaswa kufanya vile mu njia ya muzuri zaidi. Pengine tunaweza kujiuliza hivi: ‘Hata kama sikupenda namna shauri ilitolewa kuko jambo fulani naweza kujifunza kupitia mambo yenye ilisemwa? Je, naweza kutia pembeni makosa ya mutu mwenye alinitolea shauria na kujifunza mambo fulani kupitia shauri yake?’ Ni jambo ya hekima kwetu kutafuta njia fulani ya kupata faida kupitia shauri yoyote yenye wanatutolea.​—Mez. 15:31.

w01 15/5 uku. 30 fu. 1-2

‘Hekima Itafanya Siku Zetu Zikuwe Nyingi’

Namna mutu mwenye hekima anatendaka wakati banamukaripia ni tofauti na namna mutu mwenye zihaka anatendaka. Sulemani anasema hivi: “Karipia mwenye hekima, naye atakupenda. Patia mwenye hekima, na atakuwa mwenye hekima zaidi.” (Mezali 9:8b, 9a) Mutu mwenye hekima anajuaka kama “hakuna nizamu yenye inaonekana kwa sasa kuwa yenye kufurahisha, lakini inaumiza; lakini kisha, inazaa tunda lenye amani la haki kwa wale wenye wamezoezwa nayo.” (Waebrania 12:11) Hata kama shauri inaweza kuonekana kuwa yenye kuumiza, lakini kama tunaifuata tunaweza kuwa na hekima zaidi. Njo maana wakati tunapata shauri hatupaswe kumusema kwa ukali mutu mwenye anatushauria ao kuanza kujitetea.

Mufalme mwenye hekima anaendelea kusema hivi: “Fundisha mwenye haki, na elimu yake itaongezeka.” (Mezali 9:9b) Hata kama tuko na hekima mingi ao tuko na miaka mingi, hatuwezi kusema kama siye hatuna tena lazima ya kujifunza. Inafurahishaka sana kuona hata batu benye kuzeeka banaitika kweli na kujitoa kwa Yehova! Tujikaze pia kuwa na hamu ya kujifunza na kuendelea kuwa na akili ya mwepesi.

w01 15/5 uku. 30 fu. 5

‘Hekima Itafanya Siku Zetu Zikuwe Nyingi’

Hakuna mutu mwenye anaweza kututafutia hekima; kila mutu anapaswa kujikaza. Juu ya kukazia ile, Sulemani anasema hivi: “Kama unakuwa mwenye hekima, unakuwa mwenye hekima kwa faida yako mwenyewe,lakini kama uko mwenye zihaka, utabeba zihaka hiyo peke yako.” (Mezali 9:12) Hekima inasaidiaka mwenye iko nayo, na mwenye zihaka anajitafutiaka magumu yeye mwenyewe. Ile ni kweli juu byenye tunapanda njo byenye tunavunaka. Njo maana tunapaswa ‘kutega sikio yetu ili tusikilize hekima.’​—Mezali 2:2.

Mali ya Kiroho

w06 15/9 uku. 17 fu. 5

Mambo Makubwa ya mu Kitabu ya Mezali

9:17​—‘Mayi yenye mutu anaiba’ njo nini, na juu ya nini inakuwaka ‘butamu’? Juu mu Biblia ngono kati ya bibi na bwana inafananishwa na mayi ya kunywa ya kutokea mu kisima, mayi yenye iliibwa inafananisha busharati. (Mezali 5:15-17) Ile mayi iko butamu juu mwenye kufanya busharati anawazaka kama hakuna mutu mwenye atajua byenye anafanyaka mu siri.

TAREHE 21-27/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 10

Namna Gani Tunaweza Kupata Furaha ya Kweli?

w01 15/7 uku. 24 fu. 8-uku. 25 fu. 1-2

‘Baraka kwa Waadilifu’

Mutu mwenye haki atabarikiwa mu njia ingine. “Mikono yenye uvivu italeta umaskini, lakini mikono yenye bidii inaleta utajiri. Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto, lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.”​—Mezali 10:4, 5.

Maneno yenye mufalme anasema inahusu zaidi sana bafanyakazi ya mavuno. Wakati ya mavuno haiko wakati ya kuwa muvivu. Ni wakati ya kutumika kwa bidii kwa masaa mingi. Kusema kweli, ni wakati ya kutumika haraka sana.

Wakati Yesu alisema maneno yenye kufuata, alikuwa nafikiria mavuno ya batu, hapana ya mbegu. Alisema hivi: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo. Kwa hiyo, mumuombe Bwana wa mavuno [Yehova Mungu] atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Matayo 9:35-38) Mu mwaka wa 2000, batu zaidi ya milioni 14, balihuzuria Ukumbusho wa Kifo ya Yesu​—ile ni hesabu ya Mashahidi wa Yehova zaidi ya mara mbili. Nani hataitika kama ‘mashamba iko mweupe juu ya mavuno’? (Yohana 4:35) Batumishi ba kweli biko namuomba Bwana wa mavuno juu abaongezee bafanyakazi bamingi na biko najitoa kwa bidii sana mu kazi ya kufanya banafunzi juu ya kutenda kulingana na sala yabo. (Matayo 28:19, 20) Na Yehova amebariki sana kazi yabo! Mu mwaka wa utumishi wa 2000, batu zaidi ya 280000 balibatizwa. Bale batu nabo biko najikaza kufundisha Neno ya Mungu. Mu hii kipindi ya mavuno, kila mumoya wetu apate furaha kwa kujitoa kwa bidii mu kazi ya kufanya banafunzi.

w01 15/9 uku. 24 fu. 3-4

Tembea mu ‘Njia ya Unyoofu’

Sulemani anakazia faida ya kuwa mwenye haki. Anasema hivi: “Mali ya tajiri ni muji wake wenye ngome. Uharibifu wa maskini ni umaskini wao. Kazi ya mwenye haki inaongoza kwenye uzima; lakini mazao ya muovu yanaongoza kwenye zambi.”​—Mezali 10:15, 16.

Wakati fulani, utajiri unaweza kusaidia mutu apiganishe magumu fulani ya maisha yenye hakutazamia, sawa vile munara unalindaka maisha ya benye kuishi ndani. Na bumaskini bunaweza kuleta magumu mingi wakati mambo yenye haitazamiwe inatokea. (Muhubiri 7:12) Lakini, inawezekana mufalme mwenye hekima alikuwa napenda kusema kama byote biwili, bumaskini na butajiri, binaweza kuleta hatari. Inawezekana tajiri aanze kutumainia tu utajiri wake na kuwaza kama utajiri wake uko “kama ukuta wa ulinzi.” (Mezali 18:11) Na maskini naye anaweza kuwaza kama juu iko maskini hana tumaini. Na ile inaweza kufanya bote bashindwe kujifanyia jina ya muzuri mbele ya Mungu.

it-1 294

Baraka

Yehova Anabariki Banadamu. “Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri, naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo.” (Mez 10:22) Yehova anakuwaka nabariki bale benye anakubali kwa kubalinda, kubasaidia bapate matokeo ya muzuri mu mambo yenye biko nafanya, kubaongoza, na kubatimizia mahitaji yabo. Ile yote inabaleteaka faida.

Mali ya Kiroho

w06 15/5 uku. 30 fu. 18

Furaha ya Kutembea kwa Uaminifu-Mushikamanifu

18 Ni “Baraka ya Yehova”​—njo inasaidia batumishi yake bapate matokeo ya muzuri mu mambo yenye biko nafanya. Na Biblia inatuhakikishia kama Mungu ‘haongezake maumivu yoyote pamoya nayo.’ (Mezali 10:22) Sasa, juu ya nini batu ya Mungu banapataka magumu mingi na kuteswa? Kuko masababu tatu yenye inafanyaka tuteseke. (1) Kutokukamilika. (Mwanzo 6:5; 8:21; Yakobo 1:14, 15) (2) Shetani na mashetani wake. (Waefeso 6:11, 12) (3) Ulimwengu wa batu babaya. (Yohana 15:19) Hata kama Yehova anaacha ile magumu itufikie, haiko yeye njo iko natuletea ayo. Tofauti na ile, “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu, inashuka kutoka kwa Baba wa miangaza ya mbinguni.” (Yakobo 1:17) Baraka za Yehova hazikuwake na maumivu.

TAREHE 28/4–4/5

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU MEZALI 11

Usiseme!

w02 15/5 uku. 26 fu. 4

Uaminifu-Mushikamanifu Unaongoza Batu Benye Haki

Uaminifu-mushikamanifu wa mutu mwenye haki unaweza kuletea bengine matokeo ya muzuri na uovu wa mutu mwenye anafanyaka mambo ya mubaya unaweza kuletea batu bengine matokeo ya mubaya. Mufalme wa Israeli anasema hivi: “Kwa kinywa chake muasi-imani anamuharibu jirani yake, lakini wenye haki wanaokolewa kwa ujuzi.” (Mezali 11:9) Nani hatakubali kama kusingizia mutu, kusema maneno ya kuumiza, na maneno machafu inaumizaka bengine? Lakini maneno ya mutu mwenye haki inakuwaka safi na anaifikiriaka mbele ya kusema. Ujuzi unamuokoa juu uaminifu-mushikamanifu wake uko namusaidia aonyeshe kama mambo yenye kusemewa juu yake ni ya bongo.

w02 15/5 uku. 27 fu. 2-3

Uaminifu-Mushikamanifu Unaongoza Batu Benye Haki

Batu ba mu muji mukubwa benye banafuataka sheria ya haki banaletaka amani na banafanyaka bengine bajisikie muzuri kati ya batu. Na ile inafanyaka mugini iendelee. Batu benye banasemaka maneno ya kusingizia bengine, ya kuumiza, na maneno ya mubaya banaletaka fujo na banafanyaka bengine bakose amani na bagawanyike. Ile inakuwaka mubaya zaidi kama batu bengine banapendaka kubaiga. Mu muji wa vile munakuwaka fujo, kata-midomo, mwenendo wa mubaya na hata makuta inapatikanaka kwa nguvu sana.

Kanuni yenye kuwa mu Mezali 11:11 inahusu batumishi ya Yehova benye kukusanyika mu makutaniko yenye inafananishwa na miji. Kutaniko yenye kuwa na batu ba kiroho, benye haki juu biko natembea kwa uaminifu-mushikamanifu, ni kutaniko ya batu benye kuwa na furaha, benye kuwa na bidii, benye kusaidia bengine, na banamutukuzaka Yehova. Yehova anakuwaka nabariki ile kutaniko na inakuwaka nguvu kiroho. Wakati fulani, batu kiloko benye banakuwaka nahuzunika na benye habakuwake nafurahia na kusema mubaya juu ya namna mambo iko nafanyika, biko sawa “muzizi wenye sumu” wenye unaweza kuambukiza bengine benye ku mwanzo balikuwa na mawazo ya muzuri. (Waebrania 12:15) Batu ba vile banapendaka sana mamlaka na kuonekana mbele ya batu. Banafanyaka batu baanze kuwaza kama bazee ao batu bengine mu kutaniko biko natenda bila haki, kwa ubaguzi, ao mambo ingine ya vile. Kusema kweli, maneno yabo inaweza kugawanya kutaniko. Hauone kama ni muzuri tusisikilize maneno yabo na kujikaza kuwa batu ba kiroho benye kusaidia kutaniko iendelee kuwa na umoja na amani?

w02 15/5 uku. 27 fu. 5

Uaminifu-Mushikamanifu Unaongoza Batu Benye Haki

Mutu mwenye hana akili ya muzuri, ao mwenye “iko katika ukosefu wa moyo” anaumizaka bengine sana! Anasemaka sana mupaka kufikia kuanza kusingizia bengine na kubatukana. Bazee banapaswa kutenda kwa haraka juu ya kumaliza ile tabia ya vile. Tofauti na mutu mwenye “iko katika ukosefu wa moyo,” mutu mwenye kuwa na utambuzi anajuaka wakati wa kubakia kimya. Anajizuiaka kufunua mambo ya siri. Mutu mwenye iko na utambuzi anajuaka kama kukosa kuzuia ulimi kunaweza kuumiza sana bengine, njo maana anakuwaka “mwenye kutumainika.” Anakuwaka mushikamanifu ku bandugu yake na hafunuake mambo ya siri yenye inaweza kubaletea magumu. Batu ba vile, benye kuonyesha uaminifu-mushikamanifu, banakuwaka baraka mu kutaniko!

Mali ya Kiroho

g20.1 uku. 11, kisanduku

Namna ya Kupambana na Mukazo

“KUWA MWENYE FAZILI KUNAWEZA KUKUSAIDIA UPUNGUZE MUKAZO”

“Mutu mwenye fazili anajiletea faida, lakini mutu mwenye hana huruma anajiletea shida.”​—MEZALI 11:17.

Kitabu Overcoming Stress kiko na sura yenye kichwa “Kuwa Mwenye Fazili Kunaweza Kukusaidia Upunguze Mukazo.” Kulingana na mutungaji wa kitabu hicho, Doktere Tim Cantopher, kutendea wengine kwa fazili kunaweza kukusaidia ukuwe na afya ya muzuri na furaha. Kwa upande mwingine, mutu mukali anajikosesha furaha kwa sababu anafanya wengine wamuepuke.

Tunaweza pia kupata kitulizo kwa kujitendea kwa fazili. Kwa mufano, hatupaswe kujilazimisha kufanya mambo yenye kupita uwezo wetu. Hatupaswe pia kujizarau. Yesu alisema “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.”​—Marko 12:31.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine