Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/7 uku. 4-6
  • Musikiaji wa Sala Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Musikiaji wa Sala Ni Nani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yanayohakikisha Kama Muumbaji Iko
  • Musikiaji wa Sala Iko Namna Gani?
  • Tumusifu Yehova, Musikiaji wa Sala
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Umukaribie Musikiaji wa Sala
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Endelea Kusali juu Ukubaliwe na Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/7 uku. 4-6

Musikiaji wa Sala Ni Nani?

IKIWA kuna Musikiaji wa sala, kwa kweli yeye ndiye anayepaswa kuwa Muumbaji. Kwa sababu ni yeye aliyeumba ubongo wa mwanadamu, hauone kama ni yeye pekee anayeweza kujua mawazo yetu? Hauone kama ni yeye pekee anayeweza kusikia sala za wanadamu na kuwatolea musaada wanaohitaji? Lakini unaweza kujiuliza, ‘Mutu mwenye akili anaweza kabisa kuamini kama kuna Muumbaji?’

Watu wengi wanawaza kama ili kuamini kwamba kuna Muumbaji, inaomba kukataa mambo ya sayansi ya leo. Lakini wazo la kusema kwamba kuamini kama Mungu iko hakupatane na sayansi, si wazo la kweli. Fikiria mufano unaofuata.

◼ Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni juu ya walimu wa sayansi 1646 kwenye universités 21 nzuri zaidi huko États-Unis ulionyesha kama walimu karibu 550 kati yao ndio waliosema kwamba hawaamini kama Mungu iko ili kueleza maoni yao.

Ukweli ni kwamba wanasayansi wengi wanaamini kama Mungu iko.

Mambo Yanayohakikisha Kama Muumbaji Iko

Je, tunapaswa kuamini tu kama Musikiaji wa sala iko bila kuwa na mambo yenye kutusadikisha? Hapana. Wazo la kusema kama imani ni kukubali tu kile wanachokuambia bila ushuhuda si wazo la kweli. Biblia inasema kama imani ni ‘usibitisho ulio wazi wa mambo halisi ingawa hayaonekane.’ (Waebrania 11:1) Tafsiri nyingine inasema kama imani inatufanya tusadiki sana mambo ya kweli yasiyoonekana. Kwa mufano, hatuwezi kuona sauti ya radio inayopeperushwa hewani, lakini kwa sababu tunasikia radio inasema, tuna ushuhuda kabisa kama sauti hiyo iko. Vilevile, hata ikiwa hatuwezi kumuona Musikiaji wa sala, tunaweza kuchunguza mambo tuliyo nayo yanayotusadikisha kama yeye iko.

Tunaweza kupata wapi mambo ya kutusadikisha kama Mungu iko? Tuangalie tu vitu vinavyotuzunguka. Biblia inasema hivi: ‘Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mutu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.’ (Waebrania 3:4) Je, unakubali maneno hayo? Labda unapoona namna vitu vilivyo katika ulimwengu, vitu kama dunia, nyota vinatembea kwa utaratibu, unapowaza namna uzima ulianza, ao namna ubongo wa mwanadamu ulitengenezwa kwa ajabu kuliko vitu vingine vyote, unaona kama kunapaswa kuwa na mutu fulani wa hali ya juu zaidi kuliko wanadamu.a

Lakini viumbe vinavyotuzunguka haviwezi kutufundisha mambo yote juu ya Mungu. Kujua kama Mungu iko kwa kutazama uumbaji ni sawa vile kusikia tu vishindo vya miguu ya mutu fulani anayekaribia inje na wewe umo ndani ya nyumba. Kwa kweli, utajua kama mutu fulani iko pale, lakini hauwezi kujua ni nani. Ili kujua ni nani, unapaswa kufungua mulango. Vilevile, ili kumujua yule aliyeumba vitu vyote, tunapaswa kufanya jambo fulani kama hilo.

Biblia ni mulango unaotusaidia kumujua Mungu vizuri. Unapofungua mulango huo na kuchunguza unabii fulani ulio ndani na kuona namna ulivyotimizwa, unaweza kusadiki kama Mungu iko.b Zaidi ya hilo, habari zinazoeleza namna Mungu alivyowatendea watu zinatusaidia kabisa kujua ikiwa Musikiaji wa sala ni Mungu wa namna gani.

Musikiaji wa Sala Iko Namna Gani?

Biblia inaonyesha kama Musikiaji wa sala ni mutu​—ambaye unaweza kujua. Kwa kweli, ni mutu tu ndiye anayeweza kutusikiliza na kutuelewa. Ndiyo sababu maneno haya yenye kupatikana katika zaburi ni yenye kutia moyo sana: ‘Ee musikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.’ (Zaburi 65:2) Mungu anasikiliza sala za wale wanaomuomba kwa imani. Na tena ana jina. Biblia inasema: ‘Yehova yuko mbali sana na waovu, lakini anasikia sala ya waadilifu.’​—Methali 15:29.

Yehova anaweza kufurahi ao kuhuzunika. Yeye ni “Mungu wa upendo” na anaitwa “Mungu mwenye furaha.” (2 Wakorintho 13:11; 1 Timotheo 1:11) Biblia inasema kama wakati uovu uliongezeka sana duniani, ‘aliumia moyoni mwake.’ (Mwanzo 6:5, 6) Kwa hiyo, kusema kama Mungu analetea watu mateso ili kuwajaribu ni uongo. Biblia inasema hivi: ‘Haiwezekane Mungu kutenda lolote lisilo sawa.’ (Ayubu 34:10; Verbum Bible) Lakini, labda unaweza kujiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni Muumbaji mweza yote, sababu gani anawaacha watu waendelee kuteseka?’

Yehova ametupatia sisi wanadamu uhuru wa kujichagulia, kwa kufanya hivyo, ametuonyesha heshima. Je, unafurahia uhuru huo wa kuchagua namna ya kutumia maisha yako? Jambo la kuhuzunisha, watu wengi wanatumia vibaya uhuru huo na wanajiletea mateso wao wenyewe na hata watu wengine. Sasa, ona ulizo unalopaswa kujiuliza: Namna gani Mungu anaweza kuondoa mateso yote bila kunyanganya watu uhuru wao wa kuchagua? Tutapata jibu la ulizo hilo katika habari inayofuata.

[Maelezo ya chini]

a Ili kupata habari zingine zinazosadikisha kama Mungu iko, soma broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai na kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

b Broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? vimechapishwa na Mashahidi wa Yehova ili kukuonyesha mambo fulani yanayosadikisha kama Biblia iliongozwa na Mungu.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Je, Matendo Mabaya ya Dini Yanakufanya Usiamini Kama Mungu Iko?

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba matendo mabaya ya dini ndiyo yanawafanya watu wengi wasiamini kama kuna Mungu mwenye huruma anayesikiliza sala. Kwa sababu dini inajiingiza katika mambo ya vita, mambo ya terrorisme (mauaji na mashambulizi yenye makusudi fulani ya politike), na inaruhusu tabia ya kuwatendea watoto vibaya kingono, hilo linawafanya hata watu wanaosali waseme kama hawaamini kama Mungu iko.

Sababu gani mara nyingi dini inawasukuma watu wafanye mambo mabaya? Kwa kifupi: Watu wabaya wametumia dini ili kufanya mambo mabaya. Biblia ilitabiri kama walimu wa uongo wangeingia katika dini ya Kikristo na kuitumia ili kutenda mambo mabaya. Mutume Paulo aliwaandikia waangalizi Wakristo hivi: “Kutoka katikati yenu ninyi wenyewe watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.”​—Matendo 20:29, 30.

Mungu anachukizwa sana na dini za uongo. Ndiyo maana Biblia, Neno la Mungu, inaonyesha kama “damu . . . ya wale wote ambao wameuawa juu ya dunia” iko juu ya vichwa vya dini za uongo. (Ufunuo 18:24) Kwa sababu dini za uongo hazifundishe watu juu ya Mungu wa kweli, anayeongozwa na upendo katika kila jambo analotenda, machoni pa Mungu, dini hizo zina deni la damu.​—1 Yohana 4:8.

Musikiaji wa sala anasikia sala za wale wanaoteswa kwa sababu ya dini hizo. Hivi karibuni, upendo wake kwa wanadamu utamusukuma ahukumu dini zote zenye unafiki kupitia Yesu. Yesu alisema hivi: “Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako?’ . . . Hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.”​—Mathayo 7:22, 23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine