Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/10 uku. 8-9
  • Ufalme wa Mungu—Utakuletea Faida Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufalme wa Mungu—Utakuletea Faida Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu—Sababu Gani Yesu Anauona Kuwa wa Maana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Ufalme Wa Mungu
    Amuka!—2013
  • Chagua Kuunga Mukono Ufalme wa Mungu Leo!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/10 uku. 8-9
Bibi na bwana wanajifunza juu ya Ufalme wa Mungu kupitia Funzo la Biblia

KICHWA | UFALME WA MUNGU—UNAWEZA KUKULETEA FAIDA GANI?

Ufalme wa Mungu Utakuletea Faida Gani?

Labda ulielewa kupitia habari zilizotangulia kwamba Mashahidi wa Yehova wanaona Ufalme wa Mungu kuwa wa maana sana. Na labda ulipendezwa na baraka fulani za Ufalme wa Mungu za wakati unaokuja zenye zilizungumuziwa katika habari hizo. Na wakati huohuo, labda unajiuliza ikiwa ahadi hizo zitatimia kwelikweli.

Ni jambo la hekima kuwa muangalifu kuliko kuamini kila jambo unalosikia. (Methali 14:15) Kwa njia fulani, uangalifu wako unaweza kulinganishwa na ule wa Waberoyaa wa zamani. Wakati waliambiwa juu ya habari njema ya ufalme, Waberoya walikubali mambo walisikia, si kwa sababu tu walipenda mambo hayo yakuwe ya kweli. Lakini, walichunguza Maandiko kwa uangalifu “ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Kwa maneno mengine, Waberoya walilinganisha habari njema waliyosikia na mambo Maandiko yanasema. Kisha wakati fulani, walifikia kusadiki kwamba habari njema ilitegemea kabisa Neno la Mungu.

Mashahidi wa Yehova wanakuomba kwa furaha ufanye pia hivyo. Kupitia programu yetu ya kujifunza Biblia na watu bila kulipa, tunakutolea nafasi ya kulinganisha mambo sisi Mashahidi wa Yehova tunaamini juu ya Ufalme wa Mungu na mambo Biblia inafundisha.

Zaidi ya kujifunza juu ya Ufalme wa Mungu, funzo lako la Biblia linaweza kukusaidia upate majibu ya maulizo fulani ya maana sana katika maisha.

  • Tulitoka wapi?

  • Kusudi la maisha ni gani?

  • Sababu gani Mungu anaacha watu wateseke?

  • Ni jambo gani linatupata tunapokufa?

  • Dunia hii itaharibishwa?

  • Mutu anapaswa kufanya nini ili familia yake ikuwe na furaha?

Zaidi ya yote, kujifunza Biblia kutakusaidia ‘umukaribie Mungu.’ (Yakobo 4:8) Na ukimukaribia Mungu zaidi, utaelewa zaidi namna Ufalme wa Mungu unaweza kukuletea mambo mazuri, leo na hata milele. Yesu mwenyewe alimuambia Baba yake hivi katika sala: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.

Mashahidi wa Yehova wanaweza kutumia kitabu hiki ili kujifunza Biblia na wewe.

Ili kuomba funzo la Biblia bila kulipa, ambia Shahidi mumoja wa Yehova ao ujaze nafasi ya kuomba funzo kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.(Fungua kichwa OMBA FUNZO LA BIBLIA kwenye ukurasa wa mwanzo)

a Beroya ulikuwa muji katika Makedonia ya zamani.

Anaona Ufalme wa Mungu Kuwa wa Maana

Folake

Hivi karibuni, kijana mwanamuke mwenye miaka kumi anayeitwa Folake aliombwa kwenye masomo atunge habari juu ya kichwa “Mambo Ninayopenda Sana Katika Dunia Hii.” Folake alichagua kuandika juu ya sababu inayomufanya afurahie kuwaambia wengine juu ya Ufalme wa Mungu.

Folake alieleza hivi: “Ufalme wa Mungu ni serikali ya kwelikweli. Lakini haiwezi kuonekana, kwa hiyo hauwezi kuiona, hata kama unavaa miwani (lunettes)!”

Folake aliendelea kusema juu ya baraka za Ufalme huo zenye anangojea zaidi sana. Alitaja magumu fulani yenye Ufalme huo utamaliza. Aliandika, “Ninahuzunika sana wakati ninaona watu wasio na nyumba wakiishi katika barabara” na pia “watoto wanaokufa na njaa katika sehemu mbalimbali za dunia.” Aliongeza, “Ninafurahi tena wakati ninasoma andiko la Isaya 65:21.” Kuhusu watu wenye watatawaliwa na Ufalme wa Mungu, andiko hilo linaahidi hivi: “Watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.”

Folake alisema pia kwamba anangojea wakati Mungu ataondoa magonjwa yote, kupitia Ufalme wake. Katika habari yake, alitia maneno ya andiko la Ufunuo 21:4, linalosema kwamba Mungu ‘atafuta [atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwa tena.’ Alimalizia kwa kurudilia tena kwamba kusema juu ya Yehova na Ufalme wake ndilo jambo anapenda sana katika dunia hii. Kwa kweli, Ufalme wa Mungu una nafasi ya pekee katika moyo wa kijana huyo mwanamuke!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine