Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/12 uku. 3
  • Sababu Gani Inaomba Kuelewa Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Inaomba Kuelewa Biblia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Namna ya Kuwasaidia Watu Ambao Hawako Tayari Kujifunza Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Unatumia Broshua Hizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/12 uku. 3

HABARI KUBWA | Unaweza Kuelewa Biblia

Sababu Gani Inaomba Kuelewa Biblia?

“Biblia ni kitabu cha dini chenye kujulikana sana. Lakini ni kitabu chenye hakijulikane kwa Wachina na hakina maana kwao.”—LIN, INCHI YA CHINA.

“Siwezi hata kuelewa vitabu vitakatifu vya dini yangu ya Kihindu. Kwa hiyo, namna gani ninaweza kuelewa Biblia Takatifu?”—AMIT, INCHI YA INDIA.

“Ninaheshimia Biblia kwa sababu ni kitabu cha zamani na nimesikia kama ndicho kitabu chenye kuuzishwa sana. Lakini mimi mwenyewe sijaiona hata siku moja.”—YUMIKO, INCHI YA JAPANI.

Watu wengi katika dunia wanaheshimia Biblia sana. Lakini, pengine hawajue mengi juu ya mambo yenye kuwa katika Biblia ao hawajue jambo lolote. Mamilioni ya watu hao wanaishi Asia, na wengine wengi wanaishi katika inchi kwenye Biblia inapatikana sana.

Mwanamuke mwenye kusoma Biblia

Lakini, unaweza kujiuliza, ‘Sababu gani nihangaikie kuelewa Biblia?’ Kuelewa mambo yenye kitabu hicho kitakatifu kinasema kunaweza kukusaidia:

  • Utosheke na ukuwe na furaha

  • Upambane na magumu ya familia

  • Upiganishe mahangaiko

  • Ufanye urafiki wako na watu wengine ukuwe muzuri

  • Utumie feza kwa hekima

Fikiria mufano wa Yoshiko, wa inchi ya Japani. Alijiuliza ikiwa Biblia inazungumuzia nini na akaamua kuisoma. Matokeo yalikuwa nini? Alisema hivi: “Biblia ilinisaidia kupata kusudi katika maisha na tumaini juu ya wakati unaokuja.” Aliongeza hivi: “Sasa ninajisikia kuwa mwenye furaha.” Amit, mwenye tumekwisha kutaja, aliamua kuchunguza Biblia yeye mwenyewe. Anasema hivi: “Nilishangaa. Biblia iko na habari zenye zinaweza kusaidia kila mutu.”

Biblia imesaidia watu wengi sana katika maisha yao. Sababu gani usiichunguze wewe mwenyewe na uone namna inaweza kukuletea faida?

Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha

Ili kupata habari zingine juu ya namna Biblia inaweza kukuletea faida, soma broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine