Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w17 Mwezi wa 3 uku. 32
  • Jina Lenye Kuwa Katika Biblia Linapatikana Kwenye Mutungi wa Zamani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jina Lenye Kuwa Katika Biblia Linapatikana Kwenye Mutungi wa Zamani
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Jina la Mungu—Je, Inafaa Tulitumie? Maana ya Jina Hilo Ni Nini
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Jina la Mungu Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Habari Fulani za Ulimwengu—Habari Fulani Juu ya Mashariki ya Kati
    Amuka!—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
w17 Mwezi wa 3 uku. 32
Maandishi ya zamani ya Wakanaani kwenye mutungi wa udongo wenye kuwa na miaka 3000 yanafunua jina fulani lenye kuwa katika Biblia

Jina Lenye Kuwa Katika Biblia Linapatikana Kwenye Mutungi wa Zamani

Mutungi wa udongo wenye kuwa na miaka 3000

Katika mwaka wa 2012, wachimbuaji wa vitu vya zamani walivumbua vipande vya mutungi wenye kutengenezwa na udongo vyenye viko na miaka 3000. Watu wenye kutafuta habari walifurahi sana. Sababu gani? Haiko kwa sababu ya vipande vya mutungi huo lakini kwa sababu ya maandishi yenye yalikuwa kwenye vipande hivyo.

Wakati wachimbuaji wa vitu vya zamani waliweka vipande vyote pamoja, waliweza kusoma maandishi fulani ya Wakanaani kwenye mutungi huo. Yalisema hivi: “Eshba’al Ben Beda,” maana yake, “Eshba’al, mutoto mwanaume wa Beda.” Hiyo ni mara ya kwanza wachimbuaji wa vitu vya zamani wamevumbua jina hilo lenye kuandikwa kwenye chombo fulani cha zamani.

Biblia inazungumuzia mutu mwengine mwenye kuitwa Eshbaali. Alikuwa mumoja kati ya watoto wanaume wa Mufalme Sauli. (1 Mambo ya Nyakati 8:33; 9:39) Profesa Yosef Garfinkel, mutu mumoja kati ya wale wenye walivumbua mutungi huo, alisema hivi: “Ni jambo lenye kufurahisha kuona kwamba jina Eshba’al linapatikana katika Biblia, wakati wa utawala wa Mufalme Daudi tu, na sasa pia katika habari za vitu vya zamani vyenye vimechimbuliwa.” Huu ni mufano mwengine wenye kuonyesha kuwa habari za vitu vya zamani vyenye vimechimbuliwa zinaunga Biblia mukono!

Katika Biblia, Eshbaali, mutoto mwanaume wa Sauli anaitwa pia Ish-boshethi. (2 Samweli 2:10) Sababu gani neno “baali” lilibadilishwa na neno “boshethi”? Wachunguzi wanasema kuwa pengine muandikaji wa kitabu cha Pili cha Samweli aliepuka kutumia jina Eshbaali kwa sababu lilikumbusha Waisraeli Baali, mungu wa upepo mukali mwenye Wakanaani walikuwa wanaabudu. Hata hivyo, jina Eshbaali linaendelea kupatikana katika kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine