Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 2
“Watu wengi wanaelewa kama ni Ibilisi ndiye anayechochea ubaya duniani. Lakini wanajiuliza: ‘Ibilisi alitoka wapi? Je, aliumbwa na Mungu?’ Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo tunalosoma hapa.” Umuonyeshe habari iliyo kwenye ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, na muzungumuzie fungu la kwanza na andiko lililo katika fungu hilo. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/02/13
“Tungependa kujua maoni yako kuhusu mutu fulani anayeheshimiwa sana na Wakristo, Wayahudi, na hata Waislamu. Mutu huyo ni Musa. Wewe unafikiria kwanza nini unaposikia jina Musa? [Acha mutu ajibu.] Ijapokuwa Musa alifanya makosa, inafurahisha kuona namna Biblia inavyosema juu yake. [Soma Kumbukumbu la Torati 34:10-12.] Gazeti hili linazungumuzia sifa zake tatu na namna tunavyoweza kumuiga.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Leo ni jambo la kawaida watu kuhamia katika inchi nyingine ili kutafuta maisha mazuri. Unawaza kama wanapata kabisa kile wanachotafuta? [Acha mutu ajibu.] Jambo la kuhamia katika inchi nyingine halikuanza leo. Tuone mufano mumoja katika kitabu cha kwanza cha Biblia. [Soma Mwanzo 46:5, 6.] Gazeti hili linazungumuzia maulizo haya.” Onyesha musikilizaji maulizo yaliyo mwishoni mwa ukurasa wa 6.