Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/07
“Kwa kuwa hatujue mambo yenye inaweza kutufikia katika maisha, unawaza nini juu ya maneno haya ya Yesu kuhusu mahangaiko? [Soma Mathayo 6:25 na uache mutu ajibu.] Munara wa Mulinzi huu unaonyesha namna gani kutumia kanuni za Biblia kunatusaidia kupunguza mahangaiko ya makuta, magumu ya familia, na matatizo ya pekee.”
Amuka! Mwezi wa 7
“Watu wengi wanasumbuliwa sana na matatizo mbalimbali katika maisha. Unakubali jambo hilo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inaonyesha kwamba namna yetu ya kuona mambo ni ya maana wakati tunapata magumu. [Soma Methali 24:10.] Gazeti hili linatoa mashauri yenye kufaa kuhusu namna ya kupambana na magumu na linaeleza maisha ya watu fulani wenye wanaendelea kutumikisha mashauri hayo.”