Zaburi
78 Sikilizeni sheria* yangu, enyi watu wangu;
Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.
2 Nitakifungua kinywa changu kwa methali.
Nitafumbua mafumbo ya zamani za kale.+
3 Mambo ambayo tumesikia na tunayojua,
Ambayo baba zetu wametusimulia,+
4 Hatutawaficha wana wao;
Tutakisimulia kizazi kijacho mambo hayo+
Matendo ya Yehova yanayostahili sifa na nguvu zake,+
Mambo yanayostaajabisha aliyotenda.+
5 Alianzisha kikumbusho katika Yakobo
Na kuweka sheria katika Israeli;
Aliwaamuru mababu zetu
Wawajulishe watoto wao mambo hayo,+
6 Ili kizazi kijacho,
Watoto ambao hawajazaliwa, wayajue.+
Kisha wao watawasimulia watoto wao.+
7 Halafu watoto hao watamtumaini Mungu.
8 Kisha hawatakuwa kama mababu zao,
Kizazi chenye ukaidi na uasi,+
Kizazi kilichokuwa na moyo unaoyumbayumba*+
Na ambacho hakikuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.
9 Waefraimu walijihami kwa upinde,
Lakini walikimbia siku ya vita.
14 Aliwaongoza kwa wingu wakati wa mchana
Na usiku kucha kwa mwangaza wa moto.+
15 Aliipasua miamba nyikani,
Akawanywesha maji ya kutosha kana kwamba yanatoka vilindini.+
16 Alivitoa vijito kutoka kwenye jabali
Na kufanya maji yatiririke chini kama mito.+
17 Lakini waliendelea kumtendea dhambi
Kwa kumwasi jangwani yule Aliye Juu Zaidi;+
18 Walimjaribu* Mungu moyoni mwao+
Walidai wapewe chakula walichotamani.*
19 Kwa hiyo wakalalamika kumhusu Mungu,
Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza nyikani?”+
20 Tazama! Aliupiga mwamba
Hivi kwamba maji yakatiririka na vijito vikafurika.+
“Je, anaweza pia kutupatia mkate,
Au je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”+
21 Yehova alipowasikia, alikasirika sana;+
Moto+ ukawaka dhidi ya Yakobo,
Na hasira yake ikawaka dhidi ya Israeli+
22 Kwa sababu hawakudhihirisha imani katika Mungu;+
Hawakuutumaini uwezo wake wa kuwaokoa.
23 Basi akaliamuru anga lililo juu lenye mawingu,
Naye akaifungua milango ya mbingu.
24 Akaendelea kuwanyeshea mana ili wale;
Akawapa nafaka ya mbinguni.+
26 Aliuvumisha upepo wa mashariki mbinguni
Na kwa nguvu zake akaufanya upepo wa kusini uvume.+
27 Naye akawanyeshea nyama kama mavumbi,
Ndege kama mchanga kwenye ufuo wa bahari.
28 Aliwaangusha katikati ya kambi yake,
Pande zote kuzunguka mahema yake.
29 Nao wakala na kujilazimisha kula zaidi;
Aliwapa walichotamani.+
30 Lakini kabla hawajatosheleza kikamili tamaa yao,
Chakula kilipokuwa kingali kinywani mwao,
31 Ghadhabu ya Mungu ikawaka dhidi yao.+
Akawaua wanaume wenye nguvu zaidi;+
Aliwaangamiza wanaume vijana wa Israeli.
32 Licha ya hayo walizidi kutenda dhambi+
Nao hawakudhihirisha imani katika kazi zake zinazostaajabisha.+
33 Basi akazikatisha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+
Na miaka yao kwa matukio ya ghafla yenye kutisha.
34 Lakini kila mara alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta;+
Walirudi na kumtafuta Mungu,
35 Wakikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+
36 Lakini walijaribu kumdanganya kwa kinywa chao
Na kumwambia uwongo kwa ulimi wao.
Mara nyingi aliizuia hasira yake+
Badala ya kuichochea ghadhabu yake yote.
42 Hawakuzikumbuka nguvu zake,*
Siku ambayo aliwaokoa* kutoka kwa adui,+
43 Jinsi alivyoonyesha ishara zake kule Misri+
Na miujiza yake katika eneo la Soani,
44 Na jinsi alivyobadili mifereji ya Nile kuwa damu+
Hivi kwamba hawangeweza kunywa maji kutoka katika vijito vyake.
46 Mazao yao aliwapa parare wanaokula sana,
Matunda ya kazi yao ngumu akayapa makundi ya nzige.+
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe+
Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.
49 Aliwamwagia hasira yake inayowaka,
Hasira kali na ghadhabu na taabu,
Makundi ya malaika yanayoleta msiba.
50 Alitayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.
Hakuwalinda wasife;*
Naye aliwaua kwa ugonjwa hatari.
51 Mwishowe aliwaangamiza wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.
52 Kisha akawatoa nje watu wake kama kundi la kondoo+
Na kuwaongoza nyikani kama kundi la mifugo.
54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+
Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulilitwaa.+
55 Aliyafukuza mataifa kutoka mbele yao;+
Akawagawia urithi kwa kamba ya kupimia;+
Aliyafanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+
56 Lakini waliendelea kumjaribu* Mungu Aliye Juu Zaidi, na kumwasi;+
Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+
57 Pia walipotoka na kutenda kwa hila kama mababu zao.+
Hawakutegemeka kama upinde uliolegea usivyotegemeka.+
58 Waliendelea kumkasirisha kwa mahali pao pa juu,+
Nao wakachochea hasira yake kali* kwa sanamu zao za kuchongwa.+
59 Mungu alisikia na kuwaka hasira,+
Kwa hiyo akaikataa kabisa Israeli.
61 Aliacha ishara ya nguvu zake ipelekwe utekwani;
Fahari yake itiwe mikononi mwa adui.+
62 Aliwatoa watu wake wauawe kwa upanga+
Naye akaukasirikia vikali urithi wake.
63 Moto uliwateketeza kabisa vijana wake wa kiume,
Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za harusi.*
65 Kisha Yehova akaamka kana kwamba anatoka usingizini,+
Kama mwanamume hodari+ aamkavyo baada ya divai kumtoka.
66 Naye akawakimbiza maadui wake;+
Akawatia aibu ya kudumu.
67 Alilikataa hema la Yosefu;
Hakulichagua kabila la Efraimu.
69 Alipafanya mahali pake patakatifu pawe mahali pa kudumu kama mbingu,*+
Kama dunia ambayo ameiimarisha milele.+