Muziki wa kutoa shukrani.+
100 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+
Njooni mbele zake kwa vigelegele vya shangwe.+
3 Jueni kwamba Yehova ni Mungu.+
Yeye ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.+
Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+
4 Ingieni katika malango yake mkiwa na shukrani,+
Katika nyua zake mkiwa na sifa.+
Mtoleeni shukrani, libarikini jina lake.+
5 Kwa maana Yehova ni mwema;+
Fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,+
Na uaminifu wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+