Zaburi 114 Israeli alipotoka Misri,+Nyumba ya Yakobo kutoka kwenye kikundi cha watu wanaosema maneno yasiyoeleweka,+ 2 Yuda ikawa mahali pake patakatifu,+Israeli miliki yake kuu.+ 3 Bahari iliona na kukimbia;+Yordani nao ulianza kurudi nyuma.+ 4 Milima ilirukaruka kama kondoo-dume,+Vilima kama wana-kondoo. 5 Ulikuwa na nini, Ee bahari, hata ukakimbia,+Ee Yordani, hata ukaanza kurudi nyuma?+ 6 Enyi milima, hata mkarukaruka kama kondoo-dume;+Enyi vilima, kama wana-kondoo?+ 7 Kwa sababu ya Bwana uwe na maumivu makali, Ee dunia,+Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo. 8 Ambaye anabadili mwamba kuwa dimbwi la maji lenye matete,+Jiwe gumu kuwa bubujiko la maji.+