Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
122 Nilishangilia walipokuwa wakiniambia:+
“Na twende+ katika nyumba ya Yehova.”+
2 Miguu yetu ilisimama+
Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+
3 Yerusalemu limejengwa kama jiji+
Ambalo limeunganishwa pamoja kwa umoja,+
4 Ambalo makabila wamepanda kuelekea humo,+
Makabila ya Yah,+
Kama kikumbusho kwa Israeli+
Ili kulishukuru jina la Yehova.+
5 Kwa maana huko viti vya ufalme vya hukumu vimewekwa,+
Viti vya ufalme kwa ajili ya nyumba ya Daudi.+
6 Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu.+
Wanaokupenda, Ee jiji, hawatakuwa na wasiwasi.+
7 Amani na iendelee kuwa ndani ya boma lako,+
Ukosefu wa wasiwasi ndani ya minara ya makao yako.+
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema sasa:+
“Amani na iwe ndani yako.”+
9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu+
Nitaendelea kutafuta mema kwa ajili yako.+