Zaburi Wimbo wa Mipando. 126 Yehova alipowakusanya tena mateka wa Sayuni,+Tulikuwa kama wale waliokuwa wanaota ndoto.+ 2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko,+Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+Wakati huo walianza kusema kati ya mataifa:+“Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo amewafanyia.”+ 3 Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo ametufanyia.+Tumekuwa na shangwe.+ 4 Ee Yehova, uirudishe jamii yetu ya mateka,+Kama sakafu za vijito katika Negebu.+ 5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi+Watavuna kwa vigelegele vya shangwe.+ 6 Yule ambaye bila shaka anaenda, naam, akilia,+Akiwa amechukua mfuko uliojaa mbegu,+Bila shaka ataingia kwa vigelegele vya shangwe,+Akiwa amechukua miganda yake.+