Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.
47 Enyi vikundi vyote vya watu, pigeni makofi.+
Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.+
2 Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha,+
Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+
3 Atatiisha vikundi vya watu chini yetu+
Na vikundi vya mataifa chini ya miguu yetu.+
4 Atatuchagulia urithi wetu,+
Fahari ya Yakobo, ambaye amempenda.+ Sela.
5 Mungu amepanda juu kwa vigelegele vya shangwe,+
Yehova kwa sauti ya baragumu.+
6 Mpigieni Mungu muziki, pigeni muziki.+
Mpigieni Mfalme wetu muziki, pigeni muziki.
7 Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+
Pigeni muziki, mkitenda kwa busara.+
8 Mungu amekuwa mfalme juu ya mataifa.+
Mungu mwenyewe ameketi juu ya kiti chake kitakatifu cha ufalme.+
9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja,+
Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.+
Kwa maana ngao za dunia ni za Mungu.+
Yeye amepanda juu sana.+