Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora+ juu ya Wanawali. Wimbo.
46 Kwetu Mungu ni kimbilio na nguvu,+
Msaada unaopatikana kwa utayari wakati wa
taabu.+
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika+
Na hata milima ikitikisika na kuingia katika moyo wa bahari kuu;+
3 Hata maji yake yakiwa na msukosuko, na kutoa povu,+
Hata milima ikitikiswa na ghasia yake.+ Sela.
4 Kuna mto ambao vijito vyake hulifanya jiji la Mungu lishangilie,+
Maskani kuu takatifu zaidi ya Aliye Juu Zaidi.+
5 Mungu yuko katikati ya jiji;+ halitatikisika.+
Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko ya asubuhi.+
6 Mataifa yakawa na msukosuko,+ falme zikatikisika;
Akavumisha sauti yake, dunia ikayeyuka.+
7 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+
Mungu wa Yakobo ni kilele chetu salama.+ Sela
8 Njooni, tazameni matendo ya Yehova,+
Jinsi ambavyo ameweka matukio ya kushangaza duniani.+
9 Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.+
Upinde anauvunja na kuukata mkuki vipande-vipande;+
Magari ya kukokotwa anayateketeza motoni.+
10 “Salimuni amri, na mjue ya kwamba mimi ni Mungu.+
Nitatukuzwa kati ya mataifa,+
Nitatukuzwa duniani.”+
11 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+
Mungu wa Yakobo ni kilele chetu salama.+ Sela.