17 Naye akamwambia Adamu: “Kwa sababu uliisikiliza sauti ya mke wako ukala matunda ya mti ambao nilikupa amri+ hii kuuhusu, ‘Usile matunda yake,’ udongo umelaaniwa kwa sababu yako.+ Kwa maumivu utakula mazao yake siku zote za maisha yako.+
29 Naye akamwita jina lake Noa,+ akisema: “Huyu atatuletea faraja katika kazi yetu na katika maumivu ya mikono yetu yanayoletwa na udongo ambao Yehova amelaani.”+