7Kisha Yehova akamwambia Noa: “Ingia ndani ya safina, wewe pamoja na nyumba yako yote,+ kwa maana nimekuona wewe kuwa mwadilifu mbele zangu kati ya kizazi hiki.+
14 “ ‘Na kama watu hawa watatu wangekuwa katikati yake, Noa,+ Danieli+ na Ayubu,+ wao wenyewe kwa sababu ya uadilifu+ wao wangeikomboa nafsi yao,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”+
7 Kwa imani Noa,+ baada ya kupewa onyo la kimungu la mambo ambayo yalikuwa bado hayajaonekana,+ alionyesha woga wa kimungu na kujenga safina+ kwa ajili ya kuiokoa nyumba yake; na kupitia imani hiyo aliuhukumu ulimwengu+ kuwa wenye hatia, naye akawa mrithi wa uadilifu+ unaolingana na imani.
20 ambao wakati fulani hawakuwa watiifu+ wakati subira ya Mungu+ ilipokuwa ikingoja katika siku za Noa, safina ilipokuwa ikijengwa,+ ambayo ndani yake watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.+
5 naye hakujizuia kuuadhibu ulimwengu wa kale,+ bali alimlinda Noa, mhubiri wa uadilifu,+ akiwa salama pamoja na wengine saba+ alipoleta gharika+ juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu;