11 Hata hivyo, Farao pia aliwaita watu wenye hekima na walozi;+ na makuhani wa Misri wenye kufanya uchawi nao pia wakafanya jambo hilo hilo kwa ufundi wao wa uchawi.+
22 Hata hivyo, makuhani wa Misri wenye kufanya uchawi wakafanya jambo hilo hilo kwa ufundi wao wa siri;+ hivi kwamba moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi,+ naye hakuwasikiliza, kama vile Yehova alivyokuwa amesema.+
18 Nao makuhani wenye kufanya uchawi wakajaribu kufanya vivyo hivyo kwa ufundi wao wa siri,+ ili kutokeza chawa, lakini hawakuweza.+ Na chawa hao wakawa juu ya wanadamu na wanyama.
8 Basi katika njia ambayo Yane na Yambre+ walimpinga Musa, vivyo hivyo hawa pia wanaendelea kuipinga kweli,+ watu walioharibika kabisa akilini,+ waliokataliwa kwa habari ya imani.+