12 Baadaye Isaka akaanza kupanda mbegu katika nchi hiyo,+ na mwaka huo alikuwa akipata kufikia vipimo mia moja kwa kimoja,+ kwa kuwa Yehova alikuwa anambariki.+
8 Yehova atakuagizia baraka kwenye maghala yako ya chakula+ na kila kazi unayofanya,+ naye hakika atakubariki katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.
10 Leteni ghalani sehemu zote za kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ nanyi, tafadhali, mnijaribu kwa njia hii,”+ Yehova wa majeshi amesema, “kama sitawafungulia ninyi malango ya mbinguni+ na kuwamwagia baraka hata kusiwe na uhitaji tena.”+