2“‘Sasa ikiwa nafsi fulani itamtolea Yehova toleo la nafaka,+ toleo lake litakuwa la unga laini;+ naye atamimina mafuta juu yake na kutia ubani juu yake.
4 “‘Na ikiwa utatoa toleo la nafaka la kitu kilichookwa jikoni, kinapaswa kuwa cha unga laini, keki za mviringo+ zilizotiwa mafuta zisizo na chachu, au mkate mwembamba uliotiwa mafuta+ usio na chachu.+
11 “‘Hakuna toleo lolote la nafaka ambalo mtamtolea Yehova litakalofanywa kuwa kitu kilichotiwa chachu,+ kwa sababu hamtafukiza unga wowote uliokandwa wenye chachu wala asali yoyote, kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
13 “‘Na kila toleo kati ya toleo lako la nafaka utalikoleza kwa chumvi;+ wala usikubali chumvi ya agano+ la Mungu wako ikosekane kwenye toleo lako la nafaka. Pamoja na kila toleo lako utatoa chumvi.