24 Naye mtumishi wangu Kalebu,+ kwa sababu roho iliyo tofauti ilionekana kuwa pamoja naye, naye aliendelea kunifuata kikamilifu,+ nitamwingiza katika nchi ambamo ameenda, na wazao wake wataimiliki.+
9 Na ikawa kwamba mara walipokuwa wamevuka, Eliya akamwambia Elisha: “Omba lile ninalopaswa kukutendea kabla sijachukuliwa kutoka kwako.”+ Naye Elisha akasema: “Tafadhali, sehemu mbili+ za roho+ yako zije kwangu.”+
17 Pia, atakwenda mbele zake kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo+ ya akina baba kwa watoto na wale wasiotii kwenye hekima inayotumika ya waadilifu, ili kuweka tayari kwa ajili ya Yehova+ watu waliotayarishwa.”+