2 Wafalme
2 Na ikawa kwamba Yehova alipokuwa karibu kumchukua Eliya+ katika dhoruba ya upepo kwenda juu kuelekea mbinguni,+ Eliya na Elisha+ wakaondoka Gilgali.+ 2 Na Eliya akaanza kumwambia Elisha: “Keti hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma niende mpaka Betheli.” Lakini Elisha akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ mimi sitakuacha.”+ Basi wakashuka kwenda Betheli.+ 3 Ndipo wana wa manabii+ waliokuwa katika Betheli wakamjia Elisha na kumwambia: “Je, kweli unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kichwa juu yako?”+ Naye akasema: “Mimi pia najua vema jambo hilo.+ Kaeni kimya.”
4 Sasa Eliya akamwambia: “Elisha, tafadhali keti hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yeriko.”+ Lakini yeye akasema: “Kama Yehova anavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi, mimi sitakuacha.” Basi wakaenda mpaka Yeriko. 5 Ndipo wana wa manabii waliokuwa katika Yeriko wakamkaribia Elisha na kumwambia: “Je, kweli unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kichwa juu yako?” Naye akasema: “Mimi pia najua vema jambo hilo. Kaeni kimya.”+
6 Sasa Eliya akamwambia: “Tafadhali, keti hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yordani.”+ Lakini akasema: “Kama Yehova anavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi, mimi sitakuacha.”+ Basi wote wawili wakaendelea mbele. 7 Na palikuwa na watu 50 wa wana wa manabii walioenda na kuendelea kusimama wakiwa umbali wa kuonekana;+ lakini wale wawili wakasimama kando ya Yordani. 8 Ndipo Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akalifunga, akapiga maji, nayo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba wote wawili wakavuka juu ya nchi kavu.+
9 Na ikawa kwamba mara walipokuwa wamevuka, Eliya akamwambia Elisha: “Omba lile ninalopaswa kukutendea kabla sijachukuliwa kutoka kwako.”+ Naye Elisha akasema: “Tafadhali, sehemu mbili+ za roho+ yako zije kwangu.”+ 10 Kwa hiyo akasema: “Umeomba+ jambo gumu. Ukiniona wakati nitakapochukuliwa kutoka kwako, itakuwa hivyo kwako; lakini kama sivyo, haitakuwa hivyo.”
11 Na ikawa kwamba walipokuwa wanatembea, wakizungumza huku wakitembea, tazama! gari+ la vita lenye moto na farasi wenye moto, nao wakawatenganisha hao wawili; na Eliya akaanza kupanda katika ile dhoruba ya upepo kuelekea mbinguni.+ 12 Wakati huo wote Elisha alikuwa akiona jambo hilo, naye alikuwa analia hivi: “Baba yangu, baba+ yangu, gari la vita la Israeli na wapanda-farasi wake!”+ Naye hakumwona tena. Basi akachukua mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili.+ 13 Kisha akalichukua lile vazi+ rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akarudi na kusimama kando ya ukingo wa Yordani. 14 Ndipo akachukua lile vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga yale maji+ na kusema: “Yuko wapi Yehova Mungu wa Eliya, naam, Yeye?”+ Alipoyapiga maji, ndipo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba Elisha akavuka.
15 Wakati wana wa manabii waliokuwa katika Yeriko walipomwona akiwa umbali fulani, wakaanza kusema: “Roho+ ya Eliya imetua juu ya Elisha.” Basi wakaja kumpokea, wakamwinamia.+ 16 Nao wakamwambia: “Tazama, sasa, watumishi wako wanao wanaume 50 mashujaa. Tafadhali acha waende, wamtafute bwana wako. Labda roho+ ya Yehova imemwinua na kisha ikamtupa juu ya mmoja wa milima au katika moja la mabonde.” Lakini akasema: “Msiwatume.” 17 Nao wakaendelea kumsihi mpaka akaona haya, hivi kwamba akasema: “Watumeni.” Sasa wakawatuma watu 50; nao wakaendelea kutafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata. 18 Waliporudi kwake, alikuwa anakaa katika Yeriko.+ Ndipo akawaambia: “Je, sikuwaambia, ‘Msiende’?”
19 Baada ya muda watu wa jiji lile wakamwambia Elisha: “Tazama, mahali lilipo jiji hili ni pazuri,+ kama bwana wangu anavyoona; lakini maji+ ni mabaya, na nchi inasababisha mimba ziharibike.”+ 20 Kwa hiyo akasema: “Nileteeni bakuli dogo jipya, mweke chumvi ndani yake.” Basi wakalileta kwake. 21 Kisha akatoka na kwenda kwenye chemchemi ya yale maji, akatupa chumvi ndani yake+ na kusema: “Yehova amesema hivi, ‘Ninafanya maji haya kuwa yenye afya.+ Hayatatokeza tena kifo wala kuharibika mimba.’” 22 Na maji yale yangali yameponywa mpaka leo hii,+ kulingana na neno alilosema Elisha.
23 Naye akapanda kutoka hapo mpaka Betheli.+ Alipokuwa akipanda njiani, tazama, palikuwa na wavulana+ wadogo waliotoka katika jiji, nao wakaanza kumdhihaki,+ wakazidi kumwambia: “Nenda juu, wewe kipara!+ Nenda juu, wewe kipara!” 24 Mwishowe akageuka nyuma, akawaona, naye akawalaani+ katika jina la Yehova. Ndipo dubu-jike+ wawili wakatoka katika vichaka, wakaanza kuwararua vipande-vipande watoto 42 kati yao.+ 25 Naye akaendelea kutoka hapo mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka hapo akarudi Samaria.