17 Wakati huohuo wale makuhani waliolichukua sanduku la agano la Yehova wakaendelea kusimama bila kusonga kwenye nchi kavu+ katikati ya Yordani, huku Israeli wote wakivuka juu ya nchi kavu,+ mpaka taifa zima lilipokuwa limemaliza kuvuka Yordani.
14 Ndipo akachukua lile vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga yale maji+ na kusema: “Yuko wapi Yehova Mungu wa Eliya, naam, Yeye?”+ Alipoyapiga maji, ndipo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba Elisha akavuka.
15 Na Yehova hakika ataukata ulimi wa bahari ya Misri,+ na kuutikisa mkono wake juu ya Mto+ katika mng’ao wa roho yake. Naye ataupiga katika mito yake saba, naye atawafanya watu watembee wakiwa wamevaa viatu vyao.+