5 Basi Yethro, baba-mkwe wa Musa, pamoja na wanawe na mke wake wakamjia Musa huko nyikani ambako alikuwa amepiga kambi, kwenye mlima wa Mungu wa kweli.+
1Naye Yehova akasema na Musa katika nyika ya Sinai,+ kwenye hema la mkutano,+ siku ya kwanza ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili wa kutoka kwao nchini Misri,+ naye akamwambia:
4 Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa mbele za Yehova walipotoa moto haramu+ mbele za Yehova katika nyika ya Sinai; nao hawakuwa na wana wowote. Lakini Eleazari+ na Ithamari+ waliendelea kutumikia wakiwa makuhani pamoja na Haruni baba yao.
9Na Yehova akasema na Musa katika nyika ya Sinai katika mwaka wa pili baada ya kuondoka kwao katika nchi ya Misri, katika mwezi wa kwanza,+ na kumwambia: